Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa sababu ya tabia yako ya udokozi...Niliwahi kukaa kwa MTU wiki mbili nilihisi nimekaa miaka miwili.
Haha safi,nimekupenda mama wa mabinti.Hhahaha sio binti tena ni mama mwenye mabinti!!
Scenario No 2... Kwanini umfukuze mdogo wako wakati nyumba ni ya wazazi wenu?KUNA TWO SCENARIOS!
Baada ya wazazi kufariki, mimi na mdogo wangu tulichukuliwa na baba yetu mkubwa!
Life wasn't tht okey but Yatima hadeki ujue! maisha yakasonga!
Siku moja ilikuwa mkesha wa pasaka, mdogo wangu na watoto wa baba yangu mkubwa (walikuwa wakubwa zaidi yangu)
Wakaenda kanisani mkesha! mi nilikuwa naumwa sikutaka kusali usiku.
Walikuwa wadada watatu,Mmoja akaona ndio wakati wa kwenda kuchachua ,wanarudi nyumbani bila yeye!
Baba yangu mkubwa anamfokea mdogo wangu(ninayemzidi miaka 5, anaaambiwa arudi alikotoka na asirudi mpk atakapompata yule asiyerudi home). Yule baba alifunga mlango ,nje bariki kali nyumba ipo milimani flan hvi!He was asthmatic, hata kama asingekuwa asthmatic ,how on earth unamwambia mwingine asilale mpk aliyeenda kwenye starehe zake arudi!
Nilikaa ndani kama nusu saa hivi nikiwa nalia!
Nilipotoka nilienda subeleni unapokaa funguo haukuwepo!means ameingia nao kulala!
Nilliingia jikoni nikachukua shoka lile nafikir ,Nililinyanyua juuu kushuka chini kishindo kiliamsha mpk sisimizi!
wakaamka, ananitishia kunipiga!NIKAMWAMBIA NEXT STEP AFTER WHERE YU ARE NAKUPASUA!
nilifunguliwa mlango nikamfuata mdogo wangu alipo nikamwingiza ndani!
kesho yake asbh kabla hajasema ondoka au baki nilikuwa nje na mabegi na mdogo wangu namwambia tunarudi kwenye nyumba ya wazazi!
2. Huko kwenye nyumba ya wazazi alikuwepo mama yetu mdogo na wanae!
NAKO MAISHA YALIKUWA YA KIWEHU TU KWA DOGO!!
huko nilifukuza mimi!
Nikamwambia unajua nini, HII NYUMBA NI YA MAMANGU, isingekuwepo wewe ungekuwa unalipa kodi!
SASA FANYA HIVI!
NAENDA KUMALIZA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA! nikirudi uwe umetafuta pa kukaa!
ilikuwa ni likizo ya mwezi wa nne ,pepa ya necta mwezi wa tano!
Niliporudi nilimkumbusha!
MPAKA KESHO I AM THE LAST PERSON KWENYE FAMILIA KUAMBIWA TAARIFA YOYOTE INAYOHITAJI MAAMUZI YA PAMOJA
Mwanangu huna ndugu.. Bora Mimi sina shobo nao na wakileta shobo nawatia sipendi ujingaKUNA TWO SCENARIOS!
Baada ya wazazi kufariki, mimi na mdogo wangu tulichukuliwa na baba yetu mkubwa!
Life wasn't tht okey but Yatima hadeki ujue! maisha yakasonga!
Siku moja ilikuwa mkesha wa pasaka, mdogo wangu na watoto wa baba yangu mkubwa (walikuwa wakubwa zaidi yangu)
Wakaenda kanisani mkesha! mi nilikuwa naumwa sikutaka kusali usiku.
Walikuwa wadada watatu,Mmoja akaona ndio wakati wa kwenda kuchachua ,wanarudi nyumbani bila yeye!
Baba yangu mkubwa anamfokea mdogo wangu(ninayemzidi miaka 5, anaaambiwa arudi alikotoka na asirudi mpk atakapompata yule asiyerudi home). Yule baba alifunga mlango ,nje bariki kali nyumba ipo milimani flan hvi!He was asthmatic, hata kama asingekuwa asthmatic ,how on earth unamwambia mwingine asilale mpk aliyeenda kwenye starehe zake arudi!
Nilikaa ndani kama nusu saa hivi nikiwa nalia!
Nilipotoka nilienda subeleni unapokaa funguo haukuwepo!means ameingia nao kulala!
Nilliingia jikoni nikachukua shoka lile nafikir ,Nililinyanyua juuu kushuka chini kishindo kiliamsha mpk sisimizi!
wakaamka, ananitishia kunipiga!NIKAMWAMBIA NEXT STEP AFTER WHERE YU ARE NAKUPASUA!
nilifunguliwa mlango nikamfuata mdogo wangu alipo nikamwingiza ndani!
kesho yake asbh kabla hajasema ondoka au baki nilikuwa nje na mabegi na mdogo wangu namwambia tunarudi kwenye nyumba ya wazazi!
2. Huko kwenye nyumba ya wazazi alikuwepo mama yetu mdogo na wanae!
NAKO MAISHA YALIKUWA YA KIWEHU TU KWA DOGO!!
huko nilifukuza mimi!
Nikamwambia unajua nini, HII NYUMBA NI YA MAMANGU, isingekuwepo wewe ungekuwa unalipa kodi!
SASA FANYA HIVI!
NAENDA KUMALIZA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA! nikirudi uwe umetafuta pa kukaa!
ilikuwa ni likizo ya mwezi wa nne ,pepa ya necta mwezi wa tano!
Niliporudi nilimkumbusha!
MPAKA KESHO I AM THE LAST PERSON KWENYE FAMILIA KUAMBIWA TAARIFA YOYOTE INAYOHITAJI MAAMUZI YA PAMOJA
Shida tuHivi kwanini ukakae kwa mtu?
Siku tunafukuzwa kwa ndugu tena mvua ikinyesha siwezi sahau alituambia "MNAKULA KUKU KWA MRIJA SODA KWA UMA" tulihamia kwnye chumba kimoja, tukawa na kitanda kimoja hakifai hata kulala watu wawili ila mm na ndugu yangu tukawa tunabanana hapo, mama analala kwenye mfuko wa sandarusi chini....!! ngoja niishie hapa.
MUNGU HUYU SI ATHUMANI Leo nimekuwa mtu kwenye watu.
Bora ufukuzwe kwa haki!! Ila ukiwa umeonewa asee!!!! HAKIJAWAHI KUNITOKA ROHONI, sasa hivi tumekuwa wakubwa hawawezi kuniangalia machoni.Sipatii picha mnavochukiana na huyo aliewafukuza, hata kama mnasalimiana, nahis mnasalimiana kinafiki, kufukuzwa inauma sana jurist
Si umkumbusheKwa watu hakufai...nimezaliwa miaka mingi iliyopita...ila nilisimuliwa nilipozaliwa mama alikuwa akiishi kwa kaka yake...ile kukojoa kwangu kama kichanga kitandani mama akatimuliwa...nilisimuliwa hadi leo huyo mjomba namwona Hitila....yeye amesahau mimi nakumbuka!
Namashaka wewe usije kua ndo yule Kijana Emma aliye saidiwa vyombo umu aka aanza kujisifu [emoji23][emoji23][emoji23]Mimi nikitoa story yangu nahisi kuna ndugu wanapita humu nikagundulika. Ila kukaa kwa watu sijui huyo ndugu yukoje kwangu na ndio sababu nalichukia jiji la DSM.
Babu umekunywa ngapi sa hiz? Soma tenaScenario No 2... Kwanini umfukuze mdogo wako wakati nyumba ni ya wazazi wenu?
We ni mkolomije wa mChattle?
😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀Nakumbuka ilikuwa Dar mitaa ya Sinza Vatican, nilimtembelea ndugu yangu, asee jamaa alikuwa mkorofi balaa. Akirudi toka kazini lazima aguse li TV lake la uchogo, kama limechemka huo moto wake hata kwa gari la zima moto hauzimiki!!
Siku ikipikwa nyama anahesabia jikoni. Mkishakula lazima ahesabu zilizobaki.
Vitimbi vilikuwa vingi na alikuwa anatusurubu ka vile si ni wafungwa!! Siku moja nilitoka nduki kali, sikuwahi kurudi huu ni mwaka wa 11.
Nilipofika home mkoani nilimsimulia mama, siku hiyo alinipikia kilo nzima ya wali, akapakua kwa sinia kubwa na juu kasimika bakuli kubwa la nyama za kuku! Nilivua shati kuanza kutupia nyali tumboni huku nikijisemea, "ewe ndugu mchoyo wa Dar, njoo uhesabu minyama inayoshuka tumboni"