Tuliowahi kuoa wa darasa la saba na kufanikiwa hali ya kuwa siye ni graduates njooni tupeane uzoefu

Mimi nikioa sio kwamba natafuta bussiness partner nahitaji na huduma za mke hujulikana, kama nataka kujenga biashara ntatafuta bussiness partner au economic consultant au taenda benki wanipe ushauri, hiyo sio kazi ya mke.
Nilishawahi kusema humu kitu hiki hiki, mimi naoa mwanamke anaejua majukumu yake ya nyumbani ni nn, na hata kama nina duka huko dukani hatowahi kwenda kuhudumia labda muuzaji wangu awe anapeleka tu mahesabu nyumbani kama mm sipo. Kazi kuu ya meanamke ni kumuwakilisha mme wake kwenye jamii na ndo maana hata makanisani wanawake wanakua wengi sababu wao ndio kiwakilishi cha familia.

Kutarajia mke akupe ushauri wa biashara sijui kiuchumu huko ni kuanza kumuaharibu pia, atajiona anaweza sana na siku moja atajichukulia maamuzi ya kifedha kwa fedha/mali zako hadi utashangaa
 
Kwan wanawake wote wenye kipato na wasomi nchini unawajua hali zao za ndoa,wapo wanawake wanaojitambua achana na hao takataka.
Hayupo mwanamke mwenye kipato cha maana akajitambua na kuwa mtiifu kwa mume. Labda awe na kipato cha kawaida. Nimefanya kazi na wabunge na mawaziri, hiyo imekuwa sample yangu nzuri kabisa
 
Ishu ni ujitambuzi wa mwanamke mwenyewe
Pana ndoa ni askari wote mama mkubwa kazini mme umpigia salute mkewe na kutii maagizo kazini wakirudi home mama uvaa umama ndani ya nyumba anamtii mmewe ndie boss.
Ishu ni mwanamke kafata nini kwenye ndoa watoto,heshima,pesa,Bata,ngono,familia Bora kesho,nk.
Waliofata kesho ya watoto wao ndio ujitambua
 
Hayupo mwanamke mwenye kipato cha maana akajitambua na kuwa mtiifu kwa mume. Labda awe na kipato cha kawaida. Nimefanya kazi na wabunge na mawaziri, hiyo imekuwa sample yangu nzuri kabisa
Kujitambua ni matokeo ya hofu ya Mungu na kutii maagizo ya mafunfisho ya dini husika kuhusu ndoa.
 
Tunafanya hivyo ili kuwajenga, waweze kusimama hata bila sisi. Kuna kuanguka bado mwanamke akasimama, kuna kufa mwanaume bado utakuwa umeacha watoto kwa mwanamke imara
 
Nilijaribu Kutongoza Graduates wenzangu kwa muda mrefu niliambulia Matusi, maneno ya Kejeli, kudhalilishwa mpaka nikaona kama nina mikosi.

Baadae nikafikiria sasa hawa wasomi wenzangu wazuri wananifanyia hivi sasa nitapata faida gani?

Basi Bwana miaka hiyo nikazama uswazi.

Nikakutana na Demu mmoja hivi amazing

Nikamchana mistari for about 2weeks tukaanza mahusiano.

Yule mwanamke hakuamini na siku zote hakujua kama nitamuoa.

Akidhani namdanganya.

Ukweli ni kuwa Maisha yangu yalibadilika sana kuanzia pale. Nikawa mtu mwenye furaha kama wengine.

Nikawa napata usingizi.

Nikamuoa tukaanza maisha, alikuwa mchapa kazi, mwenye heshima na anapenda sana Kutom.....wa.

Nikamnunulia Gari, nikamjengea Nyumba akanizalia Watoto wawili wa kiume na Kike.

Ninaye hadi leo.
 
Mkuu hii paragraph ya Kwanza umeongea ukweli 100%
 
Hili la kuwakilisha kwenye Jamii ni kweli.

Mtaani mimi niko bize na siasa za kina Tundu Lissu na Chadema na shughuli zingine za Kijamii hivyo sipatikani sana.

Ananiwakilisha na kunipa heshima sana.
 
Pana wanawake Wana PhD,Wana pesa kuliko waume zao na wao ndio usimamia familiar lakini wanawaheshimu na kujua nafasi ya mume ni ipi kwa faida ya watoto.
Ukubwa wao wanauacha nje ya geti
Hizi ni hadithi sio uhalisia
 
Kuoa ni bahati tu kumpata mnaoendana na sio high emotional intelligence Mzee.
 
Kuoa ni bahati tu kumpata mnaoendana na sio high emotional intelligence Mzee.
Mkuu uko sahihi ila pia uwe na uvumilivu na akili kiasi kupata matunda ya ndoa some time requires minimum patience and inttelegency sio bahati tu.
 
Nimpe kitu gani mkuu, mimi kama mwanaume ninavo oa kuna vitu na vihitaji hivyo kwa 90% I settle down, mimi sio shirika la msalamba mwekundu kusaidia watu, jua pia ndoa is a struggle between two parties for dominance, so nilazima nipate ntakae tumia nguvu ndogo kumdominant.......kwahiyo niko sahihi kwa upande wangu.
 
Najua umefikiria ukukuta huna jibu πŸ˜‚ πŸ˜‚, zaidi ya kuongelea watu hamnaga cha kuongealea

Jibu swali πŸ˜‚
Teh teh teh teh teh dogoo,haya ni maisha bro.
Kwanza wapo wengi ambao hata hawajui mlango wa darasa,maisha yao mazuri kuliko ya kwako mwenye vyeti feki. Vyeti vyenyewe vinachokusaidia,ni kupata mkopo benki tu.
Af,tueleze. Tofauti yako wewe na mtu wa darasa la saba ni nini?
 
Kuna uhalisia juu ya ulichokiongea nakuunga mkono
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…