Tuliowahi kupata ajali na kunusurika tukutane hapa

Tuliowahi kupata ajali na kunusurika tukutane hapa

Tarehe 24.12.2014 Niko na shynrey yangu nafuata kuku wa kufuga sibwesa barabara ya kwenda Karema, nashuka kigongo napandisha, Mara kabinti kanaendesha baiskeli kako upande wa kulia kwangu, kwa mwendo 80 km/h nikataka kupita kushoto kwangu... Duuuuuuu nafika nakenyewe kakahama kuja left....... Paaaaaaaaa.... Ajali mbaya sana, suruali ikawa kaptula upande mmoja, binti anajaribu kuinuka anaanguka..... Watu wanaanza kujaaa... Nikajua wataniua... Nikajaribu kutoroka Kwa pkpk, tairi la mbele nimenasa kwenye shokapu.... Nasukuma pkpk had nyumba iliyokuwa jirani na barabara, upande wa kushoto jicho halioni Kwa uvimbe na tayari na la kulia linaanza kufunga... Napata lift had district hospital..... Nalazwa ck 3 na Baada ya uvimbe kuisha nagundua jicho la kushoto limekuwa dogo kutokana na mbonyeo wa fuvu left side.... Duuuuuuu kweli hujafa hujaumbika... Nilikuwa nikiuona muonekano wangu Mpya Nashindwa kuelewa how will I stand in front of my students.... Safari had Ikonda hospital Dr akanambia no way they can return my skull to normal.....Hadi Leo najiuliza kwa nn skufa.... God is love.....
Kweli ndo maana jicho lako moja dogo
 
Nilikuwa nimechukuwa likizo ninaenda kuoa mkoani Kigoma.

Siku niliyoenda kukabidhi ofisi ili kesho yake nianze rasmi likizo yangu nikiwa njiani nilipata ajali mbaya sana nilikuja kustuka siku ya tatu nikiwa hospital ya Muhimbili ,taya imevunjika mpaka leo siwezi kula muwa.

Nililala Muhimbili miezi mitatu kabla ya kuruhusiwa nikiwa nimewekwa nyaya kwenye meno ili kuzuia kinywa kisifunge kuruhusu mifupa ya taya kuunga vizuri na jicho langu la upande wa kushoto ni dogo sana .

Yaani nilipozinduka nilikuwa kwenye wodi ya SEWAHAJI pale Muhimbili nikaenda chooni kujisaidia haja ndogo nilipojiangalia kwenye kioo cha kule chooni sikuamini kama ile ni sura yangu maana ilikuwa imevimba sana na jicho langu la kushoto halioni kabisa.


Sipandi pikipiki mpaka leo kwa jinsi nilivyonusurika.
 
Nakumbuka mwaka jana mwezi wa saba natoka dar na CITY BOY tulipokaribia manyoni basi likagongana uso kwa uso na CITY BOY ya kutoka mwanza zaidi ya watu 30 walipoteza maisha nashudia Mungu saidia skuumia hata kidogo.sitaisahau sku hyo maishani
 
26/12/2014 jion samojaa kasoro moshi 2arusha tumetoka kulaa skukuu tupo na korola familia ya wanaume 4 na mwanamke mmoja mchepu wa mmoja wetu. Me nmekamatia steling wengine wamekamatia kata za kitu pendwa cha moshi, tumekaribia kia sasa magari simengi mchepu wenyewe umetoroka kwao. Imagine unapigiwa cm kwao unasema upo round about ya kijenge afu kwao ninjiro na sisi ndo hataa KIA hatujafikaa. Ile jam jam yamagari ikatokea jamaa aliyeko mbele yangu anaprimio new model akatanua kihere changu name nikafuata shughuli ikaanzia hapoo. Nkakanyagaa zutu weee nkicheki kushoto magari mengi yako spid sioni hata gap lakujichomeka nikajipa moyo tuu. Bahati Nzuri walevi wangu nao wakakaa kimya tuu yule waprimio akajitahid akamaliza msururu kama gari nane hivii kama sikosei akarud kushoto. Nikabaki mimi pakuchomeka cpaoni gari pulling hainaa nkasema hapaa nimekwisha. Nikakazaa nikabakiza fuso sasa ndo lamwisho honiii nyingi hataa nihurumiwe nipate kagap wap ghaflaa kuna escudo inakujaa mbelee nikasemaa tumeishaa sasaa jamaa anaekuja namuwashia taa japo atanue kidogo nipenye ndo kwanza kaweka gari yake katikat ya chaki na taaa kawasha fulu. Kucheki kushoto niko usawa wa tairi lambele la fuso nikawaza nikibana kushoto tumeisha nikasema ngoja nimkazie anaekujaa atapisha chaaaaa!!!!! Jamaaa kakomaaa kitendo chakufumba macho nakufumbua huyu hapaa sikuweza kuangalia fuso tenaa ila nadhan alituhurumia akapunguza mwendo. Jamaa wa escudo nikapindisha usukan kichele tuu alivyopita na huo ubavu nakwakuwa nilikata kushoto gari ikavuta upande kuirudisha kuliaa tairi ya nyuma kushoto ikaliaa gari ikatoka nje ya bara baraa nikajaribu kushika brake ikanyanyuka upande nikaachia,nikagusa zutu kidogo ile fuso ikasimama na msururu wote nao ukapaki wanatizama kitakachojiri waje kuokota mizoga ya binadamu. Namshukuru MUNGU mpaka Leo kwa anaepajua lile eneo la kia kwa nyuma kuko tambarare kiasi na hakuna miti wala ngema yoyote nikacheza nayo nikairudisha lami nikasimama pembeni ya bara baraa. Ile mawenge tukashuka wote tunalikimbia gari tumeloa mbegee vumbi lakutoshaa. Watu wanashangaa tumeponaje yule wa escudo hatukumuona tena. Tukabadil tairi tukaendelea tukapita KIA salama hapoo me nimegoma kuendesha akachukua mwenzangu nae alikuwa yuko mafuta kidogo kichwani. Ndo tunaanza panda kamlima cha pale katiti gari ikapoteza nguvu mwisho ikazima. Tukahangaika bila kujua kumbe kwenye purukushani ya mwazo kulitoboka uko chin oil ikaisha na gari ilikuwa ingine imechemka na maji yaliisha mawenge yetu tukajua rejeta ndo imezingua tukaijaza mbegee piga start kitu ikanock ingine kilichofuata kuomba msaada kutoka town wakuvutwa. ishaingia sanne kasoro ucku Magar hayasimami ovyo kuofia wakora. Wakaja washkaji na rvr kutuvuta shughuli ingine ikaanzia hapo kwanza wamelewa wanatuvuta sisi wanakimbiaa balaa na wana over take ni ucku gari yetu inategemea hand brake ndo isimame yan pombe zilikata zote. Kufika usa kidogo tuvae daraja kuchezesha gari yetu inayovutwa tari ya nyuma kushoto ikajibamiza kwenye kingo za daraja na kamba ikakatikaa wanao tuvuta hawajua wanatembea tuu. Tukawapigia cm wakapiga cha nyoro kutufuata kumbe ile tairi ilojibamiza rim ikapinda ikawa inatoa upepo kichele bwanaa wee walev wanaotuvuta wakasema tufunge kamba shala shalaa tuwahi tufike mjini kablaa haijaisha upepo mziki ukaanzaa tenaa satano unusu tunaingiza gari gerij sakina tumechoka. Sitokaa nisahu nilikaa mwezi siwez kuendesha gari na mpaka Leo niko na heshima na gari bora niendeshwe
Inasikitisha poleni Ila nimecheka sana
 
Ajali njia ya MSATA bagamoyo karibia kabisa na geti la maliasili SAA NNE usiku, nikielekea Dar, kwenye zile daraja zisizo na kingo niliona kabisa daraja linahama na katika kulikwepa .......ne next moment nilijikuta chini ya daraja gari ikiwa imegeuka juu chini
Nilitoka mzima bila jeraha kutokana na aina ya gari niliyokuwa nayo... Ingekuwa mjep sijui kama ningesalimika
Ilikuwa 2013 siku masaa machache kabla ya IDD
Ni siku ambayo asubuhi yake kuna NOAH ilipata ajali njia hiyohiyo na kuondoka na roho nane hapohapo
Pole sana
 
Mi nakumbuka tukiwa njiani hamadi semi trela hii hapa! Hadi leo sijui kilichoendelea...
 
Ilikuwa mwaka 1997 tunasafirisha maiti toka Dar kwenda Iramba mkoani Singida tulifika salama Dada akaniambia tushukuru tumefika salama pale pale nikawa mnyonge sana nikajikuta namwambia ila wakati wa kurudi tutaanguka na gari sijui kwa nini nilisema hivyo Dada akanikataza nisiseme hivyo Mimi nikamjibu kweli Dada. Tukazika na kuanza safari ya kurudi ile tunaanza safari nikamwambia Dada laaaah tunakwenda kuanguka masikini sijui tufanye nini? Dada akaniambia usimsemee hivyo nikamwambia kweli. Kutoka Singida tukafika pale ambapo ukinyoosha unakwenda Arusha ukikata kulia unapitia Dodoma mkuu wa msafara akamwambia driver nyoosha tupite ya usandawe ilikuwa ni jioni Mimi nilikuwa kiti cha pili nyuma ya driver nikamwambia driver kwa sauti kata kulia pita ya Dodoma, driver akauliuliza nimsikilize nani? Nikamwambia Mimi, mkuu wa msafara akasema nyoosha halafu akaniuliza kwanini umesema hivyo ile sauti ya kufoka nikamjibu Barabara zote mbili tutaanguka hii ya Dodoma tutapata msaada hii ya usandawe nani atatusaidia? Kanijibu hoja dhaifu driver nyoosha, nikamwambia Dada naogopa ajali Mimi nalala nisione tunavyoanguka, Dada akasema usiseme hivyo mdogo wangu nikamwambia kweli dada, nikalala muda mrefu baadae nikastuka nikamuuliza Dada hatujaanguka? Akaniambia wewe, nikamuomba nikae upande wa dirishani aliponipisha nikamwambia nalala Mungu atunusuru jamani, nikalala kama saa tatu usiku hivi nikastuka usingizini gari inayumba vibaya sana mara tukaanguka ni kiza kinene, mvua inanyesha na tupo porini peke yetu watu wakatokea madirishani maana mlango upo kwa chini Mimi nikawa nimebanwa kidogo na kiti cha mbele yangu halafu na ule usingizi nikaamua nilale tu, kule nje wakagundua sipo ikabidi waanze kuniita kuchungulia Giza nikawaambia sitoki wakanibembeleza nikatoka nina hasira ile mbaya siongei na mtu. Mkuu wa msafara akamfuata driver anataka kumpiga Mimi nikamwambia nilikwambia tukiwa Singida ukanidharau hakuna msaada hapa nyanyueni gari tuondoke, ikabidi wafanye hivyo huku wanalalamika maumivu Bahati nzuri iliwaka tukaondoka kweli Mungu ni Mkubwa yaani ukiona hiyo gari huwezi Kuamini kama itatembea na haikuua Ila majeruhi, kufika Dodoma tukabadilishiwa usafiri. baada ya muda nikawa na maumivu ya mgongo, hizi zingine ambazo ni mbaya zaidi kwangu nazihifadhi Ila Mungu ni Mkubwa kisichokuwa kikupate hakikupati
 
nimepata ajali nyingi ikiwemo za pikipiki na sababu kubwa ni ulevi!ila ajali iliyonitia akili ni mwaka huu siku ya juma3 ya pasaka niko na mshkaji wangu tumelewa ile chapachapa baada ya kuendeleza gambe toka pasaka!tuko na haria kufika sehemu flani ilikuwa mida ya saa 8 mchana jamaa alikosa kumgonga mtu wa bodaboda mi sikuwa na habari ya chochote wakati huo nimelala kwenye siti wale bodaboda wakaanza kufkuza gari huku wamebeba mawe ili wavunje vioo jamaa wangu akapata wenge na zile akaweka mafuta ya kutosha ilikuwa spidi 130 hivi kwa mbele kuna gari inaingia upande wa kulia yaani basi tukaigonga ile gari kishindo ndo kikanishtua usingizini nikaona gari imepaa mara miti inazunguka huku kurudi naona mawingu juu angani na sikuwa nimefunga belt.nikawa naskia kelele watu wanasema itakuwa wamekufa hawa,nilivyoskia hvyo nikasema embu niinuke nijue km nimekufa nikajiona mzima nikamvuta mshkaji miguu hadi nje akaamka tukaondoka eneo la tukio tukaenda baa ya jirani tukaendelea kunywa hadi askari walivyotufata tukalala nondo.ila mungu mkubwa hatukupata hata skrechi na gari ilipinduka zaid ya x7 gari hakuna fundi amesema itafaa tena hata irudishwe japan ni skrepa tu
 
Tarehe 24.12.2014 Niko na shynrey yangu nafuata kuku wa kufuga sibwesa barabara ya kwenda Karema, nashuka kigongo napandisha, Mara kabinti kanaendesha baiskeli kako upande wa kulia kwangu, kwa mwendo 80 km/h nikataka kupita kushoto kwangu... Duuuuuuu nafika nakenyewe kakahama kuja left....... Paaaaaaaaa.... Ajali mbaya sana, suruali ikawa kaptula upande mmoja, binti anajaribu kuinuka anaanguka..... Watu wanaanza kujaaa... Nikajua wataniua... Nikajaribu kutoroka Kwa pkpk, tairi la mbele nimenasa kwenye shokapu.... Nasukuma pkpk had nyumba iliyokuwa jirani na barabara, upande wa kushoto jicho halioni Kwa uvimbe na tayari na la kulia linaanza kufunga... Napata lift had district hospital..... Nalazwa ck 3 na Baada ya uvimbe kuisha nagundua jicho la kushoto limekuwa dogo kutokana na mbonyeo wa fuvu left side.... Duuuuuuu kweli hujafa hujaumbika... Nilikuwa nikiuona muonekano wangu Mpya Nashindwa kuelewa how will I stand in front of my students.... Safari had Ikonda hospital Dr akanambia no way they can return my skull to normal.....Hadi Leo najiuliza kwa nn skufa.... God is love.....
Mungu ana mipango na maisha yako mshukuru amekupa kilema cha jicho ila kuna wengine walikatika mikono wamepata strock ila wanamshukuru Mungu kwa uhai
 
nilicheka sana siku moja deiwaka kapewa akalaze hiace mida ya saa 4 usiku.
kapiga kona kubwa kuingia kushoto kumbe bodaboda inakuja ikagonga upande wa kushoto pembeni dereva ile helmeti ikachomoka ikaingia ndani ya hiace kwa wenge dereva akajua kichwa cha bodaboda kimekatika na ile helmeti ilikuwa nyekundu afu usiku jamaa akapata mawenge kila akiangalia pembeni yake anajua kichwa anazidi kukanyaga mafuta hadi mafuta ya gari yakaisha akaona haitoshi akashuka akakimbiaa hahaha
 
Mwaka 2002 TANGA
Tulikua tuna cheza mpira mtaani. Mpira ukapigwa nje ya uwanja kwa kuwa mm nilikua golikipa ili ilinibidi niufate huo mpira. Eneo tulilokuwa tunacheza lilikuwa na katani.. Kutokana na haraka haraka ya kutaka kurudisha mpira ili tuendelee na mtanange nililose umakini hvyo nikishitukia mwiba wa katani umeingia jichoni wakati nainama kuokota mpira. Nafikiri kwa watu walioishi Tanga na morogoro wanaelewa miiba ya katani ilivyo.. Nilipata maumiv ambayo sikuwah kuyapata na siwez ata kuyasimulia...Wenzangu walinipeleka Hospital na mechi ikaishia hapo hapo
 
mkuu sintosahau siku nilipo kuja dar kwa mara ya kwanza barabara ya mandela road nilipogogwa na gari nikapoteza mguu wangu mmoja daaah kwa kweli sintosahau .
Mkuu ulivyotoka mkoani kuja Dar hukuwa na mwejeji?
 
Mimi leo nipo hai ni Mungu tu amependa niwepo hai, nimenusurika katika ajali mara mbili ndani ya mwaka mmoja. Ajali ya kwanza ya pkpk ya pili gari yangu aina ya Noah mpka leo gari iko juu ya mawe but mimi natembea nikiwa mzima na viungo vyangu vyote, isipokua nina makovu mawili matatu. Hakika ninamrudishia Mungu shukurani za moyo wangu na ninampa sifa na utukufu kwa ajii ya uzima wangu. NARUDIA TENA NI MUNGU BABA KATIKA JINA LA YESU KRISTO AMEPENDA MIMI NIENDELEE KUWA HAI....I glorify you The Most High God in the name of Jesus Christ!!!
 
Back
Top Bottom