Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah asante sana best.....kuna muda sitaki kukumbuka hayo maisha kabisa kuna jamaa waliowah niona kipindi cha ufalme wangu wanajua bado nipo vizuri ni ngumu kumuelezea mtu pesa iliisha yote na manyanyaso juuduuh pole mkuu
Pole sana mkuu kama nikweli ila afadhali umezibujua ukifurahia kipindi hicho ila kuna zile zinakata tuuu na hujazifaidi kabisa inauma sanaMiaka 3 iliyopita nililima eka 40 za mpunga na 30 za mahindi nilipokuja kuuza mazao niliingiza faida ya mil 55 ukitoa na pesa ya mtaji.
Leo tar 1 nina laki moja tu..wanawake sio viumbe vya mchezo na kazi nimefukuzwa..niliowasaidia wamenitupa.
Nimejifunza mistake zote nilizofanya ila nikikumbuka naumia mno..kwa vile nina nguvu sina ulemavu naendelea kupambana.
Nimerudi home kwa wazazi maana hali ni tete ninaweza kuwa tahaira
Acha tu kila umuonae anakua adui mwisho unajifungia ndani tuuu dahBora utajiri wa kuwekeza kuliko utajiri wa pesa,maana zikianza kupukutika utasema umerogwa
Mkuy pambana,hela iliyopotea hata ukiifikiria hairudi.Mi ningekuwa na roho nyepesi ningeshawehuka kitambo.tena bora wale waliofilisika kwa kuzitumbua atleast watasema walikula bata.mie hasara zote nimezipata kwenye biashara,lakini kukata tamaa kwangu ni mwiko.alimradi unapumua,hutakiwi kukata tamaa wala kusononeka.Umenipa courage, sifikirii tena mpunga niliopoteza,kila cha moto nakiona
Namaanisha mwanamke akipata hela amepata..hayo ya tundu yakoAs long as lile tundu lipo
ohoooKama nakufahamu hiv ,,si ulikuwa ukikuta malaya wa concord kwa anayekujua unamgawia elfu 10-20 ..ulikuwa unajiita jina flan hiv la dawa hedex kama sijakosea? Bora zilikuwa zako mana nilisikia ulifungwa kwa kuiba hela za ofis kumbe zilikuwa n zako na pikpik yako ilikuwa boxer nyeusi ,, mrefu ,mweusi mwembamba kiasi ,mkimya sana ! Tuanzie hapa nikukumbushe vingine
Wanakosa story na we mtaongea nn ssHivi ni nini ambacho huwa kinafanya mtu akishuka kimaisha watu wamkimbie? Hata uliowasaidia watakuteta hadi ukome.... tena wanakusimanga na kukutangaza jinsi gani we ni fala na hata mambo mengine mengi utasingiziwa
Ni kupukutika mpaka senti ya mwisho[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Pole sana mkuu! kufilisika kama kuku ndio inakuaje?
Mkuu si kuibia wahindi tu, kwa ujumla mali ya wizi haidumu, ni kama nguo ya kuazima itabaki kuwa sio yako hata ikikupendeza namna gani.Kuna jamaa yangu mmoja alikuwaga anafanya kazi sheli fulani kitengo cha stoo ye ndo anajua yameingia mafuta kias gani na yametoka kiasi gani jamaa alipoizoea kazi akaanza kupiga cha juu yeye na jamaaa zake wawili Sababu Ile sheli ilikuwa inahumia magari ya serikali na viwanda vikubwa akawa anakula njama na madereva wanapiga cha juu enzi za jakaya.
Maisha yakaendelea jamaa na wale wenzake maisha yakawa bomba wakajenga majumba mjini sehemu t ofauti ila nyumba walizokuwa wanakaa wakajenga sehemu moja majumba ya ukweli kwa mtu asiyefahamu kazi Yao ungedhani wanapiga kazi migodini au wafanyabiashara wakubwa au watu wenye nyadhifa kubwa serikalini wakafungua biashara mbali mbali kweli wakawa H abari ya mjini kutokana na jinsi walivyodesign zile nyumba zao na wakajenga sehemu moja .
Kilichowaroga wakanunua magari ya kifahari wakawa wanaibuka nayo kazi mmoja Lexus ,mmoja x3,mwingine prado tx wakawa wanaenda nayo kazini kwenye shell ya muhind hicho ndo kiliibua maswal mfanyakazi anayelipwa 120000 kwa mwez anawezaje kumiliki magari ya kifahari namna hiyo within two years ndo uchunguzi ukafanyika wa kimya kimya wakagundua njama zao ndo wakafukuzwa kazi walifunguliwa mashtaka ya wizi wakawa wameshinda mahakamani maana washitaki walikosa vielelezo vya ushahidi wa waliiba Wapi basi kesi ikaisha muhindi aliwaambia kitu kimoja akawabembeleza Mara kwa Mara kwamba wauze zile Mali wamrudishie ela yake hata nusu lasivyo watahangaika mpaka mwisho wa maisha Yao jamaa wakaona muhindi anatania.
Maisha yakaendelea miezi ikasonga walianzaga kufilisika biashara haziendi vitu vya kule nje majumba wakaanza kuuza hadi magari life likawa gumu wote wakabaki na Yale majumba.
Alianza mmoja akauza akakimbilia visiwani na familia yake mwingine naye akafata akamuuzia mnunuzi aliyenunua Ile ya awali ilikuwa kampuni ya wazungu akabaki jamaa yangu uyo akawa mgumu kuuza nyumba make angehangaika plan yake ilikuwa abaki na nyumba aje aiombee mkopo au akipata mtu mwenye ela nzuri ndo auze ajenge nyumba ya kawaida kama m30 hivi apo ashapigika watoto alikuwa amewapeleka medium school kawahamishia kwa gvt Kula anagongea kwa ndugu na jamaa .
Wakati anawaza hivyo ndo tetemeko la ardhi likapitia nyumba yake ikaharibika vibaya sana haikuwepo namna z aidi ya kubomoa akajenga upya ndo jamaa akawa ameishia apo alikimbia mji sijui yuko Wapi.
Wito:wizi sio mzuri hasa kiwaibia hawa wahindi
Saguda Umenichekesha sana hiki ulichokisema kimenikuta Mwezi wa 10 hapo Kahama nilifikisha Duara nilikuwa nakula si chini ya Laki nne na kuendelea kila siku...ninavyoongea hapa nimelala mchana huu naangalia Tv mambo yamegeuka...hahahaaa!! zungushaaaa, wape bia haoooo!!! wanywe mpaka waombe poa!! kampuni kubwa hiiiiiiii!!!, bill inakuja 70,000/= mfukoni una 50,000/= unachukua pikipiki fasta huku wadau unawaacha wanakula mvinyo, unaenda kuvuta 200,000/= ili imalize kila kitu[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] mnahama viwanja huku group linakufuata nyuma kila MTU na bebi wake unawanywesha wewe!!!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Hela za urithi hazina hasara.
Nilizitumbuaaaa.
KATIKA MAISHA HAKUNA KITU KIZURI KAMA KWENDA KU WITHDRAW ATM.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] pole comrade, haya ndo maisha buannna!!! VP lakini huko kahama mambo yakoje?Saguda Umenichekesha sana hiki ulichokisema kimenikuta Mwezi wa 10 hapo Kahama nilifikisha Duara nilikuwa nakula si chini ya Laki nne na kuendelea kila siku...ninavyoongea hapa nimelala mchana huu naangalia Tv mambo yamegeuka...