Tuliowahi kuvamiwa, kuibiwa au kutekwa na majambazi tujikumbushe

Tuliowahi kuvamiwa, kuibiwa au kutekwa na majambazi tujikumbushe

Way back miaka ya 2006 tulikua nyumba ya kupanga miaka hio kulkua na wale vibaka wahuni sura ngumu alafu wababe wanaiba hadi mchana kulikua na chuma kimoja kinaitwa Godzilla uyo alikua akipita mchana mjue usiku hakulaliki...
Akipita watoto wote ndani (ila vibaka wa zaman walikua wana sura ngumu aiseee)
Sasa siku moja tumelala usiku nyumba nzima imebaki na wamaza na sisi madogo (hakukua na mama mwenye kijana mkubwa) tunasikia mlango wa ukumbini unagongwa kinoma..
Wapangaji wote wakafolenishwa ukumbini wahuni wanapiga mibanzi wamaza kama sokweee
Wanawaambia leteni helaaa mamaza hatuna hela jaman
Sisi watoto wa kujikojolea washajikojolea mimi nmejificha chin ya mtungi wa ukumbini..
Baada ya kukosa hela wakauliza mmepika nini
Wapangaji walopika ugali wakala mibanzi tena kama ya sokwe
Mama dula alikua kapika wali mate mbele ndo akaokoa jahazi wahun wakala wali na ukoko wote tupo tunawaangalia wakamaliza wakachukua kopo la mafuta (mamujee) wakaingiza madole yao wakakomba mafuta wakasepa
bange sio chai🤣🤣🤣🤣
 
actually walikua sio majambaz Bali ni vibaka.Nakumbuka 2013 Arusha mitaa ya unga limited mida km saa sita usiku nimetoka zangu kuangalia mechi za Uefa champions ligi, natembea zangu barabani then nikafika mahali nikachepuka nikaingia kauchochoro flani ili niingie home. Sijatembea kitambo sana mara ghafa nimekabwa shingo. Wengine wamekaba shingo nyuma wengine kama wawili wamekuja kwa mbele wameshika visu virefu wamevilengeshea tumbon kwangu then wakasema ,"we charii toa kila kitu ulichonacho vinginevyo tunakutoboa toboa hili tumbo"......... Aisee watoto wakiarusha huwa hawaongei mara mbili. Nikawaambia chukueni chochote mtakachokikuta mfukon.... Wakachukua elfu kumi iliyokuwepo pamoja na simu.

Vile visu vilikua virefu sana kiasi kwamba wakitoboa tumbo lazima vitokee mgongoni
 
Nakumbuka ilikuwa 2013, bana wee sitaka nisahau maishani mwangu.

Nakumbuka nilipiga kazi kwenye biashara yangu, nikajikusanyia pesa nzuri tu sio chini ya million 2, ghetto nilipapendezesha vizuri sana.

Chumba changu kilikuwa pembezoni na mto Arusha eneo nililopewa na wazazi wangu pamezungukwa na miti na migomba mingi sana, kuna msitu mmoja mzuri sana kama ulaya vile.

Sasa kipindi hicho nilikuwa nimenunua bonge la speaker, daily nilikuwa nakula reggae na nyimbo za hiphop za chuga, nilikuwa na computer ya dell desktop, kipindi hicho ukiwa na computer mtaa mzima unakuheshimu.

Ilikuwa majira ya saa 9 usiku, nikiwa nimelala gheto, ghafla nikasikia mlango umepigwa jiwe fatuma kwa watu wanaojua jiwe fatuma ni nini watakuambia, walikuwa kama 7 hivi wameshika marungu na mapanga wengine wananimulika na torch machoni yani kama movie vile..

Jamaa wakaniambia toa ulichonacho, nikawaambia sina chochote zaidi ya hivi vitu vya gheto, hakuna!! toa pesa ulizonazo mara mabapa ya mgongo kwa sana, nikawaambia sina pesa, kuna jamaa akawaambia huyu mpaka akatwe ndo atoe pesa, daah jamaa akanikata na panga mgongoni, nikaona niwape hela zao waondoke.

Jamaa wakanipa kichapo cha maana, wakabeba computer, nguo, viatu vyote, speaker na pesa zote nilizosave wakaondoka zao.

Nilichojifunza, simuonei mwizi huruma nikishajua ameiba kweli, yani atakula vitofali mpaka ajute kwanini kaiba..

Hayo ni yangu yalionikuta enzi hizo je nyie kiliwakuta kipi, nakaribisha mchango wenu kwenye huu uzi.

ONE TIME,
ONE FOR THE ROAD..
APPROXIMATELY ONCE AGAIN..
,
Simuonei mwizi huruma[emoji23][emoji23]
 
Mimi nakumbuka miaka ya nyuma nimemaliza kidato cha sita, nimetoka kwenye mishe zangu usiku saa tisa, halafu napita eneo la makaburini. Ghafla kwa mbali nikawa nasikia harufu ya moshi wa sigara mchanganyiko na bangi, kucheki naona kundi la watu wanapuliza wamekaa juu ya makaburi. Kipindi hicho watu walikuwa wanapigwa sana na nondo, na wiki kadhaa nyuma kuna jirani yetu aliuawawa. Kurudi nilikotoka njia ni ndefu mno, na kwenda mbele lazima yale manjemba yangenifanya kitu mbaya.

Ile akili sijui hata ilitoka wapi, sijui ni mihadarati. Nilichofanya ni kuvua nguo zote na kuzishika kwa nyuma halafu nikaanza kuelekea usawa wao, niko uchi wa mnyama. Uzuri kulikuwa na mbalamwezi. Jamaa walivyoniona wakaanza kuuliza kwa mbali, wee nani. Mimi kimya nasonga mbele tu, ile kunisogelea na marungu yao na kuniona vizuri kuwa niko uchi, jamaa walipigwa na ganzi. Kilichofuata ni kutukana na kuanza kukimbia vibaya mno kila mtu njia yake.

Kila nikikumbuka huwa najionea sana huruma na kuwaza endapo kama yale manjemba yasingekimbia.
Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.......
Walikuona jini au?
 
Nikiwa nimeachowa nyumba na wadogo zangu wazee walikuwa wameenda msiban. niIiwasikia mapema wakiwa huko nje nikaenda kujibanza nyuma ya mlango nikafungua komeo taratiibu. Ile wanahesabu 1, 2,3 nikafungua mlango paap jiwe likapitiliza. Aisee walikimbia balaa.
Kwa hiyo wezi wakaibiwa Fatuma lao
 
actually walikua sio majambaz Bali ni vibaka.Nakumbuka 2013 Arusha mitaa ya unga limited mida km saa sita usiku nimetoka zangu kuangalia mechi za Uefa champions ligi, natembea zangu barabani then nikafika mahali nikachepuka nikaingia kauchochoro flani ili niingie home. Sijatembea kitambo sana mara ghafa nimekabwa shingo. Wengine wamekaba shingo nyuma wengine kama wawili wamekuja kwa mbele wameshika visu virefu wamevilengeshea tumbon kwangu then wakasema ,"we charii toa kila kitu ulichonacho vinginevyo tunakutoboa toboa hili tumbo"......... Aisee watoto wakiarusha huwa hawaongei mara mbili. Nikawaambia chukueni chochote mtakachokikuta mfukon.... Wakachukua elfu kumi iliyokuwepo pamoja na simu.

Vile visu vilikua virefu sana kiasi kwamba wakitoboa tumbo lazima vitokee mgongoni
Wahuni wakikuwahi inabidi uwe mpole tu [emoji28]
 
actually walikua sio majambaz Bali ni vibaka.Nakumbuka 2013 Arusha mitaa ya unga limited mida km saa sita usiku nimetoka zangu kuangalia mechi za Uefa champions ligi, natembea zangu barabani then nikafika mahali nikachepuka nikaingia kauchochoro flani ili niingie home. Sijatembea kitambo sana mara ghafa nimekabwa shingo. Wengine wamekaba shingo nyuma wengine kama wawili wamekuja kwa mbele wameshika visu virefu wamevilengeshea tumbon kwangu then wakasema ,"we charii toa kila kitu ulichonacho vinginevyo tunakutoboa toboa hili tumbo"......... Aisee watoto wakiarusha huwa hawaongei mara mbili. Nikawaambia chukueni chochote mtakachokikuta mfukon.... Wakachukua elfu kumi iliyokuwepo pamoja na simu.

Vile visu vilikua virefu sana kiasi kwamba wakitoboa tumbo lazima vitokee mgongoni
Pole sana .Mimi mitaa hiyo ya ungalimited miaka ya 2010 siku ya jumapili nikaamua kwenda kusali kanisa Moja huko unga limited .Wakati huo naishi sinoni karibu na faya na ni mgeni Arusha Nina miezi kadhaa Wala sijui mitaa ya unga limited ni nuksi.Sasa nikaondoka na jirani yangu mida kama saa tatu hivi tuende taratinu kwa miguu ,kipindi hicho simu aina ya blackberry ilikiwa hot sana nikaibeba jirani akaniambia iache nikamsikiliza, nikachukia kisimu changu Cha tochi nikahamishia line yangu tukaenda tukafila kanisani salama.Muda wa kurudi kumbuka mm nilikuwa bachelor nikanunua nyama robo nikabakiwa na chenji kama 3000 tukawa tunarudi na kihand bag changu nimetia kile kisimu Cha tochi na vile vichange.Sasa tunaongoza njia tukafika kwenye kidaraja kama Cha machuma hivi unga limited na Kuna migomba mingi mingi pembezoni tukaona vijana wakubwa tu wanaogelea mtoni yaani wako watupu kama nyani ikabidi tushangae .Mida hiyo ni kama saa saba mchana na jua linawaka .Ghafla tukamwona kijana mmoja yupo smart kiaina anakija mbele yetu huku anatabasamu,basi mm Nikajua anamjua yule nilikuwa naye kumbe na yeye anajuwa yule kijana ananijuwa mm tukawa tunazidi kukaribiana nae .Alitufikia akasalimia vizuri tu tukaitikia akaniambia sisteri naomba handbag Yako nikamjibu kimzaha kaka kirahisi hivyo?Akasema unataka mpaka udhurike ndo utoe ?Nikabaki nashangaa.Yule mwenzangu kumbe ashastukia tumevamiwa akaniambia mpe haraka huku amepaniki hatari basi Nikabaki sielewi nn kinaendelea.Ghafla yule kijana akatoa sime,sijui panga refu hatari kwenye mfuko wa suruali Sasa hapo ndo sijui suruali ilikiwa imechanwa mifukoni au lilikaaje mfukoni ,Sasa na lile jua la mchana lile panga lilikuwa linametameta kwa namna lilivyonolewa.Hapo akili fasta ikanijia nikamwambia kaka ulisema unataka handbag hii hapa nikampa mwenyewe fasta,akapokea Wala hakukimbia akufungua akaniuliza sista na kupendeza kote ndo una simu kama hii? Nikamjibu maisha kaka basi akachukua simu akanirudishia line akachukua zile hela akanirudishia funguo zangu huyo akashukia kule mtoni taratibu.Tuliondoka kimya kimya mpaka tunafika hakuna anayeuliza mwingine nn kimetokea.Yaan ungalimited sitak hata kupasikia.
 
dah huu uzi umenikumbusha tukio gumu saana maishani mwangu , ni 2016, tarehe saba 7/8/2016, nimetoka zangu bank ilikuwa nmb mwanjelwa nimechukua zangu kama milion moja narudi zangu njombe, by that time nina smartphone nokia , nimependa zangu daladala nitoke nje ya hapo nitafte mahali pa kulala., likaja wazo nikalale sai nikashuka ilipo mfikemo hotel kwa sasa , ili nivuke barabara wakaja jamaa wawili wakaniambia kwa upole usivuke tupe hizo pesa, ukipiga kelele tunakua , dah wakaniambia twende huku ukibisha tunakuua wanaonyesha pisto wakanitaka nifuate uchochoro aisee sikumbuki walinipiga na nini nilopoteza fahamu hadi 8, nipo rufaaa wananiambia umepigwa na nondo na umeletwa na wasamaria wema , mzee sina hata mia wala simu ,namshukuru sana dada moja nurse alinisaidia sana na she my sister hadi leo, ila wale jamaa nimewasahe kwa sababu siwafahamu so hata nikiwachukia hainisaidii kitu,wale watu wema walionipeleka hosptal MUNGU wangu awaongezee uhai mrefu huko waliko ,lile tukio limeniacha na tatizo hadi leo pua zangu hazinusi kabisa labda harufu ya bangi ndio naipatta nikipita kw wala ganja huwa najua nje ya hapo dah sinusi, niliambiwa kuna matibabu ya tatizo la pua nafuatilia nijaribu kutibiwa ,
 
Pole sana .Mimi mitaa hiyo ya ungalimited miaka ya 2010 siku ya jumapili nikaamua kwenda kusali kanisa Moja huko unga limited .Wakati huo naishi sinoni karibu na faya na ni mgeni Arusha Nina miezi kadhaa Wala sijui mitaa ya unga limited ni nuksi.Sasa nikaondoka na jirani yangu mida kama saa tatu hivi tuende taratinu kwa miguu ,kipindi hicho simu aina ya blackberry ilikiwa hot sana nikaibeba jirani akaniambia iache nikamsikiliza, nikachukia kisimu changu Cha tochi nikahamishia line yangu tukaenda tukafila kanisani salama.Muda wa kurudi kumbuka mm nilikuwa bachelor nikanunua nyama robo nikabakiwa na chenji kama 3000 tukawa tunarudi na kihand bag changu nimetia kile kisimu Cha tochi na vile vichange.Sasa tunaongoza njia tukafika kwenye kidaraja kama Cha machuma hivi unga limited na Kuna migomba mingi mingi pembezoni tukaona vijana wakubwa tu wanaogelea mtoni yaani wako watupu kama nyani ikabidi tushangae .Mida hiyo ni kama saa saba mchana na jua linawaka .Ghafla tukamwona kijana mmoja yupo smart kiaina anakija mbele yetu huku anatabasamu,basi mm Nikajua anamjua yule nilikuwa naye kumbe na yeye anajuwa yule kijana ananijuwa mm tukawa tunazidi kukaribiana nae .Alitufikia akasalimia vizuri tu tukaitikia akaniambia sisteri naomba handbag Yako nikamjibu kimzaha kaka kirahisi hivyo?Akasema unataka mpaka udhurike ndo utoe ?Nikabaki nashangaa.Yule mwenzangu kumbe ashastukia tumevamiwa akaniambia mpe haraka huku amepaniki hatari basi Nikabaki sielewi nn kinaendelea.Ghafla yule kijana akatoa sime,sijui panga refu hatari kwenye mfuko wa suruali Sasa hapo ndo sijui suruali ilikiwa imechanwa mifukoni au lilikaaje mfukoni ,Sasa na lile jua la mchana lile panga lilikuwa linametameta kwa namna lilivyonolewa.Hapo akili fasta ikanijia nikamwambia kaka ulisema unataka handbag hii hapa nikampa mwenyewe fasta,akapokea Wala hakukimbia akufungua akaniuliza sista na kupendeza kote ndo una simu kama hii? Nikamjibu maisha kaka basi akachukua simu akanirudishia line akachukua zile hela akanirudishia funguo zangu huyo akashukia kule mtoni taratibu.Tuliondoka kimya kimya mpaka tunafika hakuna anayeuliza mwingine nn kimetokea.Yaan ungalimited sitak hata kupasikia.
Dah,siku yangu imekuwa fupi ghafla 🤣🤣🤣
 
actually walikua sio majambaz Bali ni vibaka.Nakumbuka 2013 Arusha mitaa ya unga limited mida km saa sita usiku nimetoka zangu kuangalia mechi za Uefa champions ligi, natembea zangu barabani then nikafika mahali nikachepuka nikaingia kauchochoro flani ili niingie home. Sijatembea kitambo sana mara ghafa nimekabwa shingo. Wengine wamekaba shingo nyuma wengine kama wawili wamekuja kwa mbele wameshika visu virefu wamevilengeshea tumbon kwangu then wakasema ,"we charii toa kila kitu ulichonacho vinginevyo tunakutoboa toboa hili tumbo"......... Aisee watoto wakiarusha huwa hawaongei mara mbili. Nikawaambia chukueni chochote mtakachokikuta mfukon.... Wakachukua elfu kumi iliyokuwepo pamoja na simu.

Vile visu vilikua virefu sana kiasi kwamba wakitoboa tumbo lazima vitokee mgongoni
Waende huko Mara walete upuuzi watachezea wajute
 
dah huu uzi umenikumbusha tukio gumu saana maishani mwangu , ni 2016, tarehe saba 7/8/2016, nimetoka zangu bank ilikuwa nmb mwanjelwa nimechukua zangu kama milion moja narudi zangu njombe, by that time nina smartphone nokia , nimependa zangu daladala nitoke nje ya hapo nitafte mahali pa kulala., likaja wazo nikalale sai nikashuka ilipo mfikemo hotel kwa sasa , ili nivuke barabara wakaja jamaa wawili wakaniambia kwa upole usivuke tupe hizo pesa, ukipiga kelele tunakua , dah wakaniambia twende huku ukibisha tunakuua wanaonyesha pisto wakanitaka nifuate uchochoro aisee sikumbuki walinipiga na nini nilopoteza fahamu hadi 8, nipo rufaaa wananiambia umepigwa na nondo na umeletwa na wasamaria wema , mzee sina hata mia wala simu ,namshukuru sana dada moja nurse alinisaidia sana na she my sister hadi leo, ila wale jamaa,lile tukio limeniacha na tatizo hadi leo pua zangu hazinusi kabisa labda harufu ya bangi ndio naipatta nikipita kw wala ganja huwa najua nje ya hapo dah sinusi, niliambiwa kuna matibabu ya tatizo la pua nafuatilia nijaribu kutibiwa
Eeeeh pole aiseh
 
dah huu uzi umenikumbusha tukio gumu saana maishani mwangu , ni 2016, tarehe saba 7/8/2016, nimetoka zangu bank ilikuwa nmb mwanjelwa nimechukua zangu kama milion moja narudi zangu njombe, by that time nina smartphone nokia , nimependa zangu daladala nitoke nje ya hapo nitafte mahali pa kulala., likaja wazo nikalale sai nikashuka ilipo mfikemo hotel kwa sasa , ili nivuke barabara wakaja jamaa wawili wakaniambia kwa upole usivuke tupe hizo pesa, ukipiga kelele tunakua , dah wakaniambia twende huku ukibisha tunakuua wanaonyesha pisto wakanitaka nifuate uchochoro aisee sikumbuki walinipiga na nini nilopoteza fahamu hadi 8, nipo rufaaa wananiambia umepigwa na nondo na umeletwa na wasamaria wema , mzee sina hata mia wala simu ,namshukuru sana dada moja nurse alinisaidia sana na she my sister hadi leo, ila wale jamaa,lile tukio limeniacha na tatizo hadi leo pua zangu hazinusi kabisa labda harufu ya bangi ndio naipatta nikipita kw wala ganja huwa najua nje ya hapo dah sinusi, niliambiwa kuna matibabu ya tatizo la pua nafuatilia nijaribu kutibiwa
Maskini pole Sana Sai ndo mitaa ya home hiyo so walikukuta Sae?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Yan vibaka ni watu wa ajabu saana. Anakutana na mdada anahangaika kutumia nguvu kubwa kumuibia, ya nini yote, toa amri tu leta simu,leta pochi imeisha hiyo. Mimi kipind cha nyuma kuna siku nimetoka kazin mida tu ya SAA moja na nusu usiku

Yan akichokifanya yule mwehu alinipiga roba Na bonge mtama looh Mimi chini nikavunja miwan yangu ya macho ya gharama, kilichofata pale kwa uoga nikatoa tu kila kitu,
 
Back
Top Bottom