Tuliozaa nje ya ndoa tukutane hapa, tujadili changamoto tunazokutana nazo

Sasa huyo bikra kwanini hujamwoa mkuu! mi nikikutana na bikra, naoa.
 
kuna mmoja alikuwa na binti yangu .. baada ya mtoto kufikisha miaka 9 ndo ikawa mwisho kumuona...ila hapa na pale matumizi + ada nikawa natuma.. kumbe yule mama ameshamlisha matango pori mtoto kuwa baba yako ameshafariki na korona.. . mtoto akaumia sana... juzi matokeo ya form foru yametoka binti kapiga 1.7.... sasa mama yake na mashost zake wakamchukua binti kwenda kumpongeza ..wakiwa huko gafla bint akaanza kulia akasema baba yangu angekuwa hai angefurah sana.. shost mmoja akauliza kwa Edson ameshafariki? . mama mtu akajiuma uma..... baadae sijui ni katika mazingira gani mtoto akasikia akimwambia yule shost yake kuwa nilimdanganya maana sitak baba yake ahusike kwa lolote...mtoto akaidaka hiyo....halooo palichimbika.. juzi jumamosi imebid mwenyewe (mama mtoto) anipigie na amsafirishe binti.. niko nae hapa.....huyu ndo nilijua nimepoteza.. kawa wa kwanza kufika hapa home.. w..mke wa ndoa wawili... nje ninao watano...
 
Hivi kuna familia kabisaaaa iko baba mmoja mama mmoja na watoto wao tuu?? Yaani hakuna mambo ya nazi na nyanya kukutanishwa gengeni??

Duh!!!
Ndiyo ipo.Ya kwangu ni mfano .Nina watoto watatu tu kwa mke mmoja wa ndoa.Hatuna mpango wa kuongeza na haiwezekani kwakuwa mke alishafunga kizazi.Mimi mwenyewe nishafanya maamuzi ya kutoza nje.
 
Watafutie pori walime na kufuga; maisha ni haya haya
 
Umechangia kuiharibu dunia chief. Hao wote baada ya kuwazalisha umewafanya wazinzi ni vigumu kuolewa.
Kwa takwimu zilizopo, wanawake ni wengi kuliko wanaume, na wanaume wanazidi kupungua siku hadi siku kutokana na kukimbilia michezo ya wanawake; mwisho wa siku dada zetu wanakosa watu wa kuwapa ujauzito.
 
Nilichojionea kutoka kwa Baba yangu juu ya watoto wakimatabaka litabaki kuwa darasa kwangu juu ya athari zilizopo kwenye mfumo wa maisha ya namna hii.

Kama watoto hawataishi kwa kupendana na kushirikiana jua kwamba umetengeneza bomu litakalo kuathiri siku zote za uzee wako.
 
Somesha hao watoto had I chuo kikuu ikibidi na huo utakuwa uridhi wao.Kisha andika usia ukimkabidhi ma mkubwa uridhi mliochuma pamoja
Bi mkubwa atabaki na vile vyote tulivyovipata tukiwa kwenye ndoa; huku nje ni kuwasapoti mahitaji ya shule na tiba kama itahitajika.
 
Siku zote mtoto akishakuwa mkubwa atapenda kujua wazazi wake wawili walipo.
 
Kwa sasa hapana mkuu, nipo makini. Hata micheps nimeacha kabisa🤣
Ni vizuri kutulia, umri ukishaenda wanaume tunakuwa hatuna nguvu za kimamlaka; tunakuwa kama simba dume, tukisubiri jike awinde alete chakula.
 
Ndiyo ipo.Ya kwangu ni mfano .Nina watoto watatu tu kwa mke mmoja wa ndoa.Hatuna mpango wa kuongeza na haiwezekani kwakuwa mke alishafunga kizazi.Mimi mwenyewe nishafanya maamuzi ya kutoza nje.
Wapime hao watoto wako dna, isijekuwa wakulungwa walishaingia huko ndani.
 
Ukianza kuwaweka pamoja sasa hivi, uchague ndoa yako ivunjike au ukaribishe migogoro isiyokuwa ya lazima.
 
hongera bro! unawakilisha. namimi nina ndoto kama hiyo ya kuwa na watoto wasiopungua 12 kama wale wanafunzi wa Yesu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…