Sio wote wenye mpango wa kuzaa nje ya ndoa wengine inatokea tu. Kuna jamaa Alikuwa mpole na muadilifu Sana ukatokea rafiki yake kufukuza mke aliyeishi naye muda mrefu bila ya kuzaa jamaa akawa mshauri wao kwa kipindi kirefu sana.
Shida ikaja ikaonekana kwa mke kitabibu kabisa sasa mume huyu akasema waitatue kienyeji yaani waende kwa waganga mke akagoma Kata Kata jamaa akafukuza mke. Baada ya miezi kama Sita jamaa akamuomba rafikiye (mshauri) amsaidie warudiane tena jamaa akasuruhisha mwanamke kwa shingo upande akarudi maisha yakaendelea.
Miezi kadhaa wakazinguana tena jamaa anataka mtoto mwanamke hayuko tayari kuenda kwa waganga. Jamaa (mshauri) akaongea na rafikiye kuwa atumie njia ya kitabibu na yuko tayari hata kuchangia gharama za matibabu jamaa akagoma akamtimua tena. Tendo hili la kutimuana lilidumu kwa muda mrefu mshauri akawatema akapiga beat wasimshirikishe Mambo Yao.
Siku moja mke wa jamaa akaja kumuaga ( mshauri) kuwa amefukuzwa na hatorudi tena kwa jamaa hivyo maisha yake amemuachia Mungu tu. Haikupita miezi Sita jamaa akaanza kuishi na mke mwingine. Mke asiyezaa akaleta taarifa kwa mshauri kuwa jamaa kaoa mshauri akamuuliza analichukuliaje jambo hilo?. Ye ye akasema poa tu hakuna shida. Ikapita ka miaka miwili kamili. Mshauri akaingia kwenye mgogoro wa kindoa kwa mke kukosa uaminifu na dharau.
Mshauri akawa na mawasiliano na na Yule mke aliyeachwa na rafikiye haikupita kipindi kirefu mahusiano yakaanza. Huyu mshauri akijua huyu mwanamke ana shida ya uzazi kabisaa akajiachia, aisee haikupita miezi Sita kitu kikaitika, mwanamke mimba, anaulizwa naye anashangaa hajui ikabidi wote wacheke tu imekuawaje Kuwaje. Mwanamke analea mimba sasa. Ni mimi na mshauri tu ndio tunajua. Sasa nikamuuliza jamaa ( mshauri) isijekuta mimba si yake siku wamekutana kimwili iliKuwaje?. Akanisimulia K ilikuwa tight isivyo kawaida, demu Alikuwa anakema Sana kwa uchungu pia alipofanikiwa na demu kuzoea game demu Alikuwa anafika kileleni mapema Sana inaonekana demu Alikuwa ametulia kweli. Nikamwambia basi huna jinsi msitiri tu kama ni hivyo.
Hivyo sio kila anayezaa nje huwa ni makusudi. kuna wengine inatokea pasipokukusudia.
kikubwa mimba ni kiumbe hakina hatia hivyo kinahitaji kutunzwa na kuhudumiwa ipasavyo ili nacho kifikie hatima yake duniani.