Tumalize Ubishi: Tundu Lissu nitajie IGA au BIT inayoeleza kutakuwa na HGA alafu bado inayoenesha kiwango cha uwekezaji na mgawanyo wa mapato?

Dunia haiendi kwa uelewa wa nchi moja inakwenda kwa uelewa wa jumla. Kanuni zinatungwa na sheria za kimataifa ambazo zinasomewa huko vyuoni, unaposikia mwanasheria wa kimataifa mbobezi tambua kuwa alisoma hizo kanuni huko vyuoni na akazifanyia mitihani na akafaulu, masuala ya mikataba ya kimataifa sio sawa na biashara za mapeasi au maembe yanafuata miiko na maadili yake.

Watu 350 wanaitwa wabunge na ndio wanaokuwakilisha wewe na mimi baada ya kupigiwa kura, na ndio hawa wenye kuongoza nchi kupitia bunge lililopo kisheria.

Huwezi kuishi kwa kufuata taratibu zako mwenyewe ni lazima uheshimu zile zilizopo na zinazoheshimiwa na dunia nzima, hakuna nchi inayoweza kuwepo kama kisiwa cha baharini.

Hizi kelele hazitusaidii kwa ujumla wetu.
 
Bibi kiukweli hii IGA sio rafiki kwa Tanzania na hicho ndo hatukitaki na unajua HILO
 
Usichoelewa contract ni Makubaliano; Na hakuna sheria inayosema makubaliano lazima yawe SIRI; ila mnaoingia Mkataba ndio maamuzi yenu muweke nini siri na nini muweke wazi (UAMUZI NI WENU) sasa linapokuja suala la mali ya nchi na sio mtu (kuwaamulia wananchi mambo gani yawe SIRI na wewe kuona ni sawa, nachelea kusema watu kama wewe ndio walitufikisha hapa)

Unaongelea kwamba wabunge ndio wawakilishi; Niambie ni Mikataba mingapi huwa inakwenda kujadiliwa Bungeni au huwa ni watu wanamalizana huko huko (tena wengine wanamalizana huko ughaibuni afadhali hata wangekuwa wanakuja kusaini mikataba huku huenda tungeambulia pesa ya juice na vitafunwa na malazi ambayo wangelala)
 
Naona unaendelea kuleta longolongo
 
Mkataba wa bomba la mafuta Uganda mpaka Tanga umepita bungeni.

Mikataba ya manunuzi ya ndege yote imepita bungeni.

Mkataba wa bandari umepita bungeni na umekwenda mbali zaidi unajadiliwa kwa zaidi ya mwezi mmoja na jamii nzima.

Wewe ndiye huelewi unayedhani mkataba unapaswa uwekwe wazi, kumbuka kuna mengi yanayoandikwa kwenye mikataba ambayo kampuni moja haipendi yajulikane kwa washindani wao wa kibiashara.
 
Hivi unajua unachoandika kweli hapa au unachosema baada ya kuandika unasahau hapo hapo..., Umesema Bungeni zinakwenda Summary haziwezi kwenda Mkataba ? Je Mikataba ya Gesi ilipita Bungeni; Na yale so called Madudu aliyoshangaa JPM ambayo kikweke alituingiza Bagamoyo ilipita wapi ? Au mpaka leo nani anajua nini ni nini ?

Mimi naongelea Transparency ili hata yale So called Madudu aliyopitisha JK; JPM akashangaa; Au Samia Akipitsha leo atakayekuja Kesho akashangaa ; Au yeye mwenyewe alivyoshangaa vipengele vimebadilishwa..., Haya yote yataendelea kutokea kama Hakuna UWAZI kwenye mali za UMMA; Na hawa wajanja wanajua kucheza na watu kama nyie ndio maana wanajibanza kwenye Non Disclosure Agreements...
 
Unataka kushindana na Gwiji la sheria TUNDU ANTIPAS MUGWAI LISSU J.

Ngoja vijana wake tukupe shule.
Lisu ambae alibwagwa mahakamani na Albert Msando? Hii nchi kwakweli Acha tu masisiemu yatawale milele ikiwa hawa Walokole wanaojiita mbadala ndio wako katika tope hili la upumbavu, inasikitisha sana huenda ukawa ni graduate wa chuo kikuu na bado akili yako ikawa imedumaa kiwango hicho, kuna mwenzio mwingine hata kinachoendelea mahakamani hafuatilii
 
Kuwepo kwa uwazi kwenye mikataba inategemea na makampuni tunayofanya nayo biashara iwapo yanaridhika nao au hapana.

Bomba la gesi alilosaini mkataba hayati JPM, umeshawahi kuuona mkataba wake hadharani?.

Biashara ya manunuzi ya ndege ya cash, umeshawahi kuiona mikataba yake hadharani?

Na kila kitu kinapita huko huko bungeni. JPM aliyeyaona madudu ya JK, na yeye Samia anayashangaa madudu aliyoyacha, mfano ni watu wengi kufungwa bila ya makosa yenye kueleweka na kuishia kutesa familia zisizo na makosa yoyote.

JPM alikuwa anapenda kuonyesha yeye ni bora kuliko JK na hata kuliko Mkapa, alikuwa anapenda sana kuidharau awamu ya Kikwete na alipoingia akataka kubadilisha kila kitu kilichoanzishwa na mtangulizi wake na akayafanya maisha yakawa magumu zaidi.
 
Mpaka sasa 192 - 0

Hakuna hata mmoja aliyeweza Kui-challenge hoja.


Kweli hii ni funga kazi.
 
Hacha kutuandikia ujinga...ili swala sio la lissu ni la viongozi wako wa ccm na Wanasheria wenu Mavi wanaoshindwa ata kujibu maswali huko ughaibuni,wanaishia kusema yes ,No. i was not there that day...wakati sahihi kwenye makaratasi ni yake.
 
Haha
 
Hacha kutuandikia ujinga...ili swala sio la lissu ni la viongozi wako wa ccm na Wanasheria wenu Mavi wanaoshindwa ata kujibu maswali huko ughaibuni,wanaishia kusema yes ,No. i was not there that day...wakati sahihi kwenye makaratasi ni yake.
Umeelewa hoja na swali?
 
Kama unaona Lissu amepotosha umma, panda jukwaani ukaelimishe inavyojua wewe ili watanzania wengi wajue na siyo kumkosoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…