Tume ya Haki Jinai kuanza kuzichunguza TAKUKURU, DCEA, Polisi, Magereza na Mahakama kesho

Tume ya Haki Jinai kuanza kuzichunguza TAKUKURU, DCEA, Polisi, Magereza na Mahakama kesho

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Akizungumza leo Jumanne Januari 31, 2023 Ikulu Chamwino, Dodoma wakati akizindua tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki jinai nchini, Rais Samia ameitaka tume hiyo kuichunguza ofisi hiyo juu ya utendaji kazi na uendeshaji ili kubaini kasoro zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuiboresha iweze kutoa haki kwa wananchi.

Amesema mbali na ofisi hiyo ya mashtaka tume hiyo itakayoanza kazi Jumatano Februari 1, hadi Mei 30, 2023 itazifanyia tathmini taasisi za utoaji haki jinai nchini ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na kuibua manung’uniko kwa wananchi, ikiwamo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Jeshi la Polisi, Magereza na Mahakama.

“Kutokana na ukubwa wa kazi tunawapa miezi minne kuanzia kesho hadi Mei 30 nendeni mkaangalie Ofisi ya Mashtaka kwenyewe kukoje na kuna kasoro zipi.

“Zamani ofisi hii kulikuwa na ngoma nzito inachezwa mpaka kukusanya fedha za plea bargaining nyingine zimeonekana na nyingine hazijaonekana ukifuatilia utaambiwa mara kuna akaunti China.

“Tutazame kuna nini haswa kilichoharibu hii taasisi, pia tuiangalie Takukuru kwa sababu kubadilisha tu mkuu wa taasisi haisaidii watamdanganya tu wafanye wanavyotaka.

“Jeshi la Magereza na kwenyewe tukalitazame, magereza zetu zikoje na zinatakiwa ziweje, mwendelezo wake na kama linafanya kazi ya msingi? Mamlaka ya Kuzuia Dawa za Kulevya nako kuna changamoto nyingi za kutegea watu dawa,” amesema Rais Samia.

Naye, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amempongeza Rais kwa kuanzisha tume hiyo ili Watanzania waweze kupata haki kwani kumekuwa na manung’uniko mengi ya wananchi juu ya mfumo wa utoaji haki jinai nchini.

MWANANCHI
 
Itapendeza kwa kweli khaa.
Hongera mama Kwa hatua hii. Katika hiyo miezi 3 ya tume kufanya kazi naomba miezi 2 itumike kuchunguza mapolisi maana huko ndio kumeoza na rushwa na kesi za kubambikiziana ili wapate pesa.

Kama kuna taassi hawatosheki na mishahara yao basi ni mapolisi.

Hawa jamaa wana njaa Sana ase
 
Wajumbe wa timu ni nani, wasijekuwa wajomba wa wakurugenzi wa hizo taasisi
Mapolisi, Jaji mkuu, Katibu mkuu, Mkurugenzi mkuu wa Takukuru na nani sijui shasahau, lakini wote hao walikuwa ni viongozi waandamizi wa taasisi hizo, kwa sasa ni wastaafu.

Utaratibu huu tayari ulikwishakukosolewa mapema kwamba, hao wote hawawezi kutenda ya maana kwa sababu mfumo huu wa hovyo wa haki jinai ndiyo walioukuta na ukawanufaisha.

Na hakuna hata mmoja wao katika historia ya maisha yake ambaye alikwishapata misukosuko ya kisheria na kutiwa ndani na akaonja joto ya jiwe kwa uharamia wa haki jinai.

Hivyo sasa, haidhaniwi kuwa tume hiyo wataweza kuleta mapendekezo ya maana na yenye tija.

Wadau walishauri kuwa ingelichaguliwa tume yenye mchanganyiko ulio sawa, pamoja na hao waliochaguliwa sasa, wangelikuwemo pia na watu kama Mbowe ama Wakili Madeleka na wafungwa waliofungwa hadi kumaliza vifungo kwa kesi za kubambikiziwa.

Hapo wangeweza kufukua vizuri makaburi bila kuacha mabaki ya mifupa.

Sasa ngoja tusubiri tuone tume hiyo kama itakidhi matakwa ya aliye wateua pamoja na wananchi kwa ujumla.

Ninaona dhamira njema ya kutoka moyoni ya Rais wetu Samia, lakini sina imani sana na viongozi wengi waliobebwa na mfumo huu mbovu wa ukandamizaji na uonevu wa haki jinai kwa watu.
 
Soma comment #10 ama uangalie You tube leo Ikulu Chamwino.
Wamepewa room ya kuongeza Watu kulingana na vile wao watahitaji au watakavyo ona itafaa.

Ila ishu ni pale pale... Wataweza kuchimbua na kupukutisha magugu yote? Au ndio recycling of endless cycles
 
Kuna abuse kubwa ya ofisi katika baadhi ya kazi zilizofanyika katika kushitaki au kukusanya kodi kwa wafanyabiashara.

Nilihisi ipo siku, wale waliojitia wako kimbelembele kufanya dhuluma zile, rungu litawaporomokea. Kuna mambo hayakuwa ya haki, wala hayakuwa ya kujenga na kuendeleza Taifa.
 
Wamepewa room ya kuongeza Watu kulingana na vile wao watahitaji au watakavyo ona itafaa.

Ila ishu ni pale pale... Wataweza kuchimbua na kupukutisha magugu yote? Au ndio recycling of endless cycles
Nimemsikia Rais akiwaasa wenye mamlaka kule tume itakakopita, watoe "room" kwa ushirikiano mkubwa!

Mimi ninataka kuona mabadiliko ya kisheria ya kweli kuhusu hizi taasisi za kihaki jinai yanafanyiwa kazi.

Maana kumbu kumbu bado zipo za tume nyingi sana zilikwisha kuundwa huko nyuma, lakini hakuna popote matokeo yake yalikaa yakatangazwa na kufanyiwa kazi.

Na mabadiliko yakija kufanywa kwa kubaraza ili hali hii iendelee, basi yatubidi sasa citizen wote tuungane na kushinikiza mabadiliko ya kweli yafanyike ndani ya katiba mpya na siyo vinginevyo.
 
Naye, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amempongeza Rais kwa kuanzisha tume hiyo ili Watanzania waweze kupata haki kwani kumekuwa na manung’uniko mengi ya wananchi juu ya mfumo wa utoaji haki jinai nchini.
Sijui kwanini huyu Mtu simwini hata angesema nini
 
Nimemsikia Rais akiwaasa wenye mamlaka kule tume itakakopita, watoe "room" kwa ushirikiano mkubwa!

Mimi ninataka kuona mabadiliko ya kisheria ya kweli kuhusu hizi taasisi za kihaki jinai yanafanyiwa kazi.

Maana kumbu kumbu bado zipo za tume nyingi sana zilikwisha kuundwa huko nyuma, lakini hakuna popote matokeo yake yalikaa yakatangazwa na kufanyiwa kazi.

Na mabadiliko yakija kufanywa kwa kubaraza ili hali hii iendelee, basi yatubidi sasa citizen wote tuungane na kushinikiza mabadiliko ya kweli yafanyike ndani ya katiba mpya na siyo vinginevyo.
Uko sahihi
 
Kuna abuse kubwa ya ofisi katika baadhi ya kazi zilizofanyika katika kushitaki au kukusanya kodi kwa wafanyabiashara.

Nilihisi ipo siku, wale waliojitia wako kimbelembele kufanya dhuluma zile, rungu litawaporomokea. Kuna mambo hayakuwa ya haki, wala hayakuwa ya kujenga na kuendeleza Taifa.
Yaani hata hivyo kwa Rais Samia kutambua kuwa hakuna haki huko ni nia njema.
 
Akizungumza leo Jumanne Januari 31, 2023 Ikulu Chamwino, Dodoma wakati akizindua tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki jinai nchini, Rais Samia ameitaka tume hiyo kuichunguza ofisi hiyo juu ya utendaji kazi na uendeshaji ili kubaini kasoro zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuiboresha iweze kutoa haki kwa wananchi.

Amesema mbali na ofisi hiyo ya mashtaka tume hiyo itakayoanza kazi Jumatano Februari 1, hadi Mei 30, 2023 itazifanyia tathmini taasisi za utoaji haki jinai nchini ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na kuibua manung’uniko kwa wananchi, ikiwamo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Jeshi la Polisi, Magereza na Mahakama.

“Kutokana na ukubwa wa kazi tunawapa miezi minne kuanzia kesho hadi Mei 30 nendeni mkaangalie Ofisi ya Mashtaka kwenyewe kukoje na kuna kasoro zipi.

“Zamani ofisi hii kulikuwa na ngoma nzito inachezwa mpaka kukusanya fedha za plea bargaining nyingine zimeonekana na nyingine hazijaonekana ukifuatilia utaambiwa mara kuna akaunti China.

“Tutazame kuna nini haswa kilichoharibu hii taasisi, pia tuiangalie Takukuru kwa sababu kubadilisha tu mkuu wa taasisi haisaidii watamdanganya tu wafanye wanavyotaka.

“Jeshi la Magereza na kwenyewe tukalitazame, magereza zetu zikoje na zinatakiwa ziweje, mwendelezo wake na kama linafanya kazi ya msingi? Mamlaka ya Kuzuia Dawa za Kulevya nako kuna changamoto nyingi za kutegea watu dawa,” amesema Rais Samia.

Naye, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amempongeza Rais kwa kuanzisha tume hiyo ili Watanzania waweze kupata haki kwani kumekuwa na manung’uniko mengi ya wananchi juu ya mfumo wa utoaji haki jinai nchini.

MWANANCHI
Uishi mileleeee mama
 
Back
Top Bottom