Pre GE2025 Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yamkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka Paul Makonda

Pre GE2025 Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yamkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka Paul Makonda

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa kuwaweka ndani watu bila kuwapeleka mahakamani masaa 96? Angewekwa dada yako au mama yako ndani ungesema hivyo?
Kwani makonda ana kituo cha polisi kipi hicho cha magomeni au kibirizi😂😂
 
Na kukaidi kuitikia wito wa Time, kuna toa taswira gani kwa wake anaowangoza.
Makonda Kenya nchi zinazo heshimu haki za binadamu, hawezi kuwa hata mwenyekiti wa kitongoji
Hivi kupeleka Mahakamani anahusika Makonda au? Yeye aliweka ndani taratibu zingine zinabaki juu ya polisi!
Vilaza hao bila shaka wanatumika lakini watafail big time!

Nasimama na MAKONDA
Kwa vile ndugu zako au wewe hujawai kuwa muhanga wa kadhia za kunyimwa haki ya kuishi.
Subiri yakukute utajuta kuzaliwa.
 
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imemkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka, Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Paul Makonda aliyeagiza mwananchi mmoja kukamatwa na kuwenda rumande saa 96 bila kufunguliwa mashtaka...
Way forward ya hiyo tume ni nini

Maana binafsi nilitegemea tume wangetoa na mwelekeo kwamba baada ya kumkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka huyo aliye shitakiwa nini kinafata
 
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imemkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka, Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Paul Makonda aliyeagiza mwananchi mmoja kukamatwa na kuwenda rumande saa 96 bila kufunguliwa mashtaka.

Pia imesema, Makonda alipoitwa mbele ya tume kuwasilisha utetezi wake alikaidi.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Julai 19, 2024 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji mstaafu Mathew Mwaimu wakati akitoa taarifa ya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora kwa mwaka 2022/23.

Amesema tume ilipokea malalamiko dhidi ya Makonda katika uchunguzi wa kutoa amri ya kukamatwa na kuwekwa ndani ya mahabusu ya polisi mkazi mmoja wa Arusha (hakutajwa jina).

Amesema Tume baada ya uchunguzi imebaini amri iliyotolewa na mkuu wa mkoa haikuwa halali na haikuzingatia aina ya makosa na taratibu ulioainishwa kisheria wa utekelezaji wa mamlaka hayo na kwamba mwananchi huyo hakuwa muhusika wa madai ya msingi, ambayo Makonda aliyatumia kushughulikia suala lililokuwa mbele yake.

“Ilibainika pia kuwa mkuu wa mkoa huyo alivuka mipaka ya majukumu yake kwa kushughulikia na kutoa maamuzi katika suala ambalo lilipaswa kufuata mkondo wa kisheria wa kimahakama kwa kuwa madai hayo yangeshughulikiwa kama shauri la daawa,” amesema Jaji Mwaimu.

“Aidha, hata kama kulikuwa na viashiria vya makosa ya kijinai, njia sahihi ingekuwa ni kulielekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.”

Amewataka viongozi wa umma kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi wakati wote wanapotekeleza majukumu yao na si kujichukulia sheria mkononi.

Jaji Mwaimu amesema tume pia imebaini kutozingatiwa kwa haki za mtuhumiwa kwa kuwekwa mahabusu kwa saa 96 (sawa na siku nne) bila ya kufunguliwa mashtaka.

“Pamoja na kuitwa kutoa maelezo mbele ya tume ili kuwasilisha utetezi wake, mkuu huyo wa mkoa (Makonda) alikaidi kufika mbele ya Tume,” amesema Jaji Mwaimu.

Amesema lakini hilo halikuweza kuzuia tume kutekeleza majuku yake kwa sababu ni taratibu tume inapowaita wahusika katika kutoa ile haki ya kusikilizwa, kwamba mtu ametoa, kwa hiyo tume ni lazima itoe fursa ya wewe kusikilizwa pia unasemaje kuhusu tuhuma zinazokukabili.

“Kwa hiyo, ukikataa kufika mbele ya tume na kutoa maelezo, haituzuii tume kuendelea kufanya shughuli zetu na kukamilisha uchunguzi,” amesema Jaji Mwaimu

Jitihada za Mwananchi kumpata Makonda kwa simu yake ya mkononi hakupatikana kujua kwa nini hakwenda na kuhusu tukio hilo tanjwa
Jaji Mwaimu amesema katika kipindi cha mwaka 2022/23 tume imepokea malalamiko 1,524 ambapo ilihitimisha jumla ya malalamiko 789 na kufanya malalamiko yaliyoendelea kuanzia Julai 1, 2023 kuwa ni 885.

Katika hatua nyingine, Jaji Maimu amesema uchunguzi dhidi ya madai ya Mbunge wa Babati (CCM), Pauline Gekul na wenzake kudaiwa kuwafanyia vitendo vya ukatili na udhalilishaji vijana wawili waliokuwa wafanyakazi wake, hayakuweza kuthibitishwa.

Amesema tume hiyo ilifanya uchunguzi wa tuhuma hizo zinazodaiwa kufanywa na Gekul aliyedaiwa kutenda kosa hilo Desemba 2023 kwa Hashim Philemon na Michael Marishamu kwa kuwaingizia chupa sehemu ya haja kubwa ili waseme ukweli, kuhusu kumwekea sumu kwenye chakula na kuweka vitu vya uchawi kwenye hoteli yake ya Paleii Lake View.

Mwenyekiti huyo amesema baada ya uchunguzi, tume kwa kuzingatia maelezo ya watu mbalimbali waliohojiwa na vielelezo ambavyo tume imevipitia haikubaini suala hilo kufanyika.

“Hata hivyo tume ilibaini walalamikaji walizuiliwa kwa muda mrefu wakati wakihojiwa na mlalamikiwa kuhusu tuhuma za kutaka kumwekea sumu (Pauline Gekul) pamoja na kupeleka madawa ya kishirikina katika hoteli yake na hivyo kusababisha walalamikaji kukosa haki yao ya kuwa huru,” amesema Jaji Mwaimu.

Chanzo: Mwananchi
Hivi hizo tume za Nini?naona kama tunapoteza fedha za umma Bure
 
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imemkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka, Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Paul Makonda aliyeagiza mwananchi mmoja kukamatwa na kuwenda rumande saa 96 bila kufunguliwa mashtaka.

Pia imesema, Makonda alipoitwa mbele ya tume kuwasilisha utetezi wake alikaidi.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Julai 19, 2024 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji mstaafu Mathew Mwaimu wakati akitoa taarifa ya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora kwa mwaka 2022/23.

Amesema tume ilipokea malalamiko dhidi ya Makonda katika uchunguzi wa kutoa amri ya kukamatwa na kuwekwa ndani ya mahabusu ya polisi mkazi mmoja wa Arusha (hakutajwa jina).

Amesema Tume baada ya uchunguzi imebaini amri iliyotolewa na mkuu wa mkoa haikuwa halali na haikuzingatia aina ya makosa na taratibu ulioainishwa kisheria wa utekelezaji wa mamlaka hayo na kwamba mwananchi huyo hakuwa muhusika wa madai ya msingi, ambayo Makonda aliyatumia kushughulikia suala lililokuwa mbele yake.

“Ilibainika pia kuwa mkuu wa mkoa huyo alivuka mipaka ya majukumu yake kwa kushughulikia na kutoa maamuzi katika suala ambalo lilipaswa kufuata mkondo wa kisheria wa kimahakama kwa kuwa madai hayo yangeshughulikiwa kama shauri la daawa,” amesema Jaji Mwaimu.

“Aidha, hata kama kulikuwa na viashiria vya makosa ya kijinai, njia sahihi ingekuwa ni kulielekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.”

Amewataka viongozi wa umma kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi wakati wote wanapotekeleza majukumu yao na si kujichukulia sheria mkononi.

Jaji Mwaimu amesema tume pia imebaini kutozingatiwa kwa haki za mtuhumiwa kwa kuwekwa mahabusu kwa saa 96 (sawa na siku nne) bila ya kufunguliwa mashtaka.

“Pamoja na kuitwa kutoa maelezo mbele ya tume ili kuwasilisha utetezi wake, mkuu huyo wa mkoa (Makonda) alikaidi kufika mbele ya Tume,” amesema Jaji Mwaimu.

Amesema lakini hilo halikuweza kuzuia tume kutekeleza majuku yake kwa sababu ni taratibu tume inapowaita wahusika katika kutoa ile haki ya kusikilizwa, kwamba mtu ametoa, kwa hiyo tume ni lazima itoe fursa ya wewe kusikilizwa pia unasemaje kuhusu tuhuma zinazokukabili.

“Kwa hiyo, ukikataa kufika mbele ya tume na kutoa maelezo, haituzuii tume kuendelea kufanya shughuli zetu na kukamilisha uchunguzi,” amesema Jaji Mwaimu

Jitihada za Mwananchi kumpata Makonda kwa simu yake ya mkononi hakupatikana kujua kwa nini hakwenda na kuhusu tukio hilo tanjwa
Jaji Mwaimu amesema katika kipindi cha mwaka 2022/23 tume imepokea malalamiko 1,524 ambapo ilihitimisha jumla ya malalamiko 789 na kufanya malalamiko yaliyoendelea kuanzia Julai 1, 2023 kuwa ni 885.

Katika hatua nyingine, Jaji Maimu amesema uchunguzi dhidi ya madai ya Mbunge wa Babati (CCM), Pauline Gekul na wenzake kudaiwa kuwafanyia vitendo vya ukatili na udhalilishaji vijana wawili waliokuwa wafanyakazi wake, hayakuweza kuthibitishwa.

Amesema tume hiyo ilifanya uchunguzi wa tuhuma hizo zinazodaiwa kufanywa na Gekul aliyedaiwa kutenda kosa hilo Desemba 2023 kwa Hashim Philemon na Michael Marishamu kwa kuwaingizia chupa sehemu ya haja kubwa ili waseme ukweli, kuhusu kumwekea sumu kwenye chakula na kuweka vitu vya uchawi kwenye hoteli yake ya Paleii Lake View.

Mwenyekiti huyo amesema baada ya uchunguzi, tume kwa kuzingatia maelezo ya watu mbalimbali waliohojiwa na vielelezo ambavyo tume imevipitia haikubaini suala hilo kufanyika.

“Hata hivyo tume ilibaini walalamikaji walizuiliwa kwa muda mrefu wakati wakihojiwa na mlalamikiwa kuhusu tuhuma za kutaka kumwekea sumu (Pauline Gekul) pamoja na kupeleka madawa ya kishirikina katika hoteli yake na hivyo kusababisha walalamikaji kukosa haki yao ya kuwa huru,” amesema Jaji Mwaimu.

Chanzo: Mwananchi
Hivi hizo tume za Nini?naona kama tunapoteza fedha za umma Bure
 
Hayo mambo mbona tunayaona kwa viongozi karibu wote ktk serikali ya Samia kwann iwe Makonda tu? Nahisi Kuna watu wanamuwinda Makonda kwa udi na ubani.
 
Hii rume haianaga meno bali ina recommendations tu ..ni moja ya taasisi zinazo kula pesa zetu tu bure
 
Wawe wanapima mabaya na mazuri then wanafanya uamuzi, yawezekana issue ilikuwa framed kumchafua Makonda lakini kwanini akatae wito...?
Kuna umuhimu wa Viongozi vijana kuwa na unyenyekevu,lakini pia wenye kufanya tathmini wasijudge kabla ya kusikiliza upande wa pili hata kama upande huo umekataa kutoa ushirikiano,mbinu zipo nyingi kabla ya kutoa report.
 
Ndugu zake wasukuma wakikusikia watakuja mbio mbio kama kumtetea ndugu yao.
Hakuna habari ya usukuma au ukabila hapa. Andika habari ya Makonda kama mtanzania.
Watanzania tulivuka mipaka ya ukabila miongo mingi iliyopita, tusirudi nyuma. Ukienda usukumani wanakuona kama ndugu yao (walioishi mikoa mingi ya Tanzania wanalijua hili).
 
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imemkuta na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka, Mkuu wa Mkoa wa Arusha (RC), Paul Makonda aliyeagiza mwananchi mmoja kukamatwa na kuwenda rumande saa 96 bila kufunguliwa mashtaka...
Hii tume ingebadili jina tu maana haisadifu.

Kujiita Tume ya Haki za binadamu na utawala bora sio sahihi.
 
Siasa haiamini kama binadamu hatujakamilika...
 
Nauliza tu ndugu zangu kwa mfano Makonda katoa Amri fulani akamatwe je wakamataji hawaangalii sheria inasemaje?!

Niliwahi kuuliza swali hili mahali fulani wakati DC wa Kinondoni by then Salum Happi alipoagiza Polisi wamuweke rumande mbunge wa Kawe mh Halima Mdee kwa saa 48

Mlale Unono 😀
 
Amesema Tume baada ya uchunguzi imebaini amri iliyotolewa na mkuu wa mkoa haikuwa halali na haikuzingatia aina ya makosa na taratibu ulioainishwa kisheria wa utekelezaji wa mamlaka hayo na kwamba mwananchi huyo hakuwa muhusika wa madai ya msingi, ambayo Makonda aliyatumia kushughulikia suala lililokuwa mbele yake.
Tume ndiyo inafanya uchunguzi, inasikiliza kesi na ndiyo inayotoa hukumu? Mbona hapa ni kama hapajakaa sawa au wanasheria mnasemaje? Yaani mtu huyo huyo afanye uchunguzi, aendeshe mashitaka na awe hakimu wa kutoa hukumu? Mbona hii tume ni kama imekaa kisiasa zaidi badala ya ki profession.
 
Kwanza nimpongeze tume kwa kutekekeleza majukumu yake bila woga, ila niipe pole kwa kukanganyikiwa na kesi za viongozi.

Kwa uelewa wangu mdogo ninaoweza kusema kwa upande mmoja wa Sheria makonda hayupo sawa maana ameikandamiza hakika ya mshtakiwa, lakini kwa upande mwingine ni sahihi kwa alichokifanya.

Kuna muda inabidi kuchukua maamuzi makali kwa wakosaji ili kuwakumbusha wajibu wa haki kwa wote, mathalani na hapo maamuzi ya makonda yalilenga kutetea haki na sio kuipoteza.

Tukumbuke na yeye ni mwanadamu mwenye moyo wa damu na nyama
 
Chadema mmepata ajenda 🐼
Simpaka iwe😮🐼🔥

CHADEMA toka imeshikiliwa na Dikteta Mbowe, ajenda yao ni moja tu-kutengeneza mazingira ya kudhoofisha Jeshi la Polisi-na hivyo kuonekana hakuna usalama wa raia. Yaani kwa kifupi,wanataka kuidhoofisha serikali na hatimaye nchi.

Hatahivyo
==========
Kuh: Makonda
Swali la msingi: Amevunja sheria gani?
 
Back
Top Bottom