Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yabandika majina ya walioteuliwa kuwania Urais na Makamu wa Rais

Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yabandika majina ya walioteuliwa kuwania Urais na Makamu wa Rais

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
NEC leo inatarajiwa kutangaza waombaji walioteuliwa kugombea urais wakati wa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Wagombea hao walitakiwa kupata wadhamini 200 kila mkoa kutoka mikoa 10 na kati ya hiyo miwili ya Zanzibar

Tanzania ina vyama 19 vya siasa vyenye usajili, viwili TLP na UDP havikufanya mchakato wa kupata wagombea urais kwa kuwa vimeamua kumuunga mkono mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli

Wagombea kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), UPDP, DP na NCCR-Mageuzi jana walifika katika ofisi za makao makuu ya NEC kuhakiki taarifa na ujazaji wa fomu kama ziko sahihi.

Kwa mujibu wa ratiba ya NEC baada ya wagombea kurejesha fomu, itachambua, itapitisha majina na kutangaza wale walioteuliwa ifikapo leo saa 10 jioni.

Majina hayo yatakaa kwenye ubao wa matangazo hadi kesho saa 10 jioni ikiwa ni fursa iliyotolewa na NEC kwa wale wanaotaka kuwawekea pingamizi wateule. wagombea kuanza kampeni.

Uteuzi huo utafanyika katika ofisi za makao makuu ya NEC, Njedengwa jijini Dodoma. Mwanzoni mwa mwezi huu, NEC ilikutana na vyama vya siasa na pamoja na mambo mengine, ilitangaza kuwa fomu za uteuzi wagombea urais zingeanza kutolewa Agosti 5 hadi 25 mwaka huu, Dodoma.

Wagombea 17 wamechukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea urais akiwemo Seif Maalim Seif (AAFP), Philip Fimbo ( DP), Leopard Mahona (NRA), John Magufuli (CCM), Qeen Sendiga (ADC) , Mutamwega Mgaiwa (SAU) naYeremia Maganja (NCCR Mageuzi).

Wengine waliochukua fomu za kuomba kuteuliwa ni Twalib Ibrahim Kadege (UPDP), Bernard Membe (ACT Wazalendo), Cecilia Mwanga (Demokrasia Makini), na Tundu Lissu (Chadema).

Wagombea wengine ni Hashim Rungwe (Chauma), Khalfan Mohamed Mazurui (UMD), Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), David Mwaijojele (CCK), John Shibuda (ADA-TADEA, na Maisha Muchunguzi (NLD).

Wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 waombaji 11 walichukua fomu NEC, wawili hawakuzirudisha, na mmoja alirejesha nje ya muda uliokuwa umepangwa hivyo kulikuwa na wagombea wanane.

Katika uchaguzi wa mwaka huu, kati ya wagombea 17 waliochukua fomu za uteuzi NEC, wanawake ni wawili Cecilia Augustino Mwanga, Qeen Sendiga na kuna wagombea wenza watano wanawake.

Mwenyekiti wa NEC Jaji mstaafu Semistocles Kaijage amesema fomu kwa ajili ya ubunge na udiwani zingetolewa makao makuu ya halmashauri za wilaya yalipo majimbo na za udiwani zingetolewa kwenye kata husika kuanzia Agosti 12 hadi leo.

Kukamilika kwa kazi hiyo kutatoa fursa kwa vyama kuanza kampeni kwa wagombea urais, ubunge na udiwani. Kampeni kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu zinatarajiwa kuanza kesho Agosti 26 hadi Oktoba 27 mwaka huu.

Oktoba 28 Watanzania waliojiandikisha kupiga kura watatumia haki yao hiyo kuchagua viongozi wao. Kwa mujibu wa NEC daftari la wapigakura kwa sasa lina jumla ya wapiga kura milioni 29,188,347, vituo vyakupigia kura 80,155 na kila kituo kitakuwa na wapiga kura wasiozidi 500.

NEC pia imetangaza kuwa kama ilivyokuwa wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 mwaka huu kutakuwa na majimbo ya uchaguzi 264 yakiwemo 214 ya Tanzania Bara na 50 ya Zanzibar.

UPDATES

NEC YAANZA KUBANDIKA MAJINA YA WAGOMBEA KUTOA NAFASI YA PINGAMIZI

Zoezi la kubandika majina ya walioteuliwa kugombea kiti cha Rais na Makamu wa Rais linaendelea nje ya Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) eneo la Njedengwa Jijini Dodoma.

Hatua hii inatoa fursa kwa watu walioruhusiwa kisheria kuweka pingamizi dhidi ya wagombea hao kuweka pingamizi zao. Mwisho wa kuweka pingamizi ni kesho tarehe 26 Agosti 2020, saa 10 jioni.

Wanaoruhusiwa kuweka pingamizi ni Mgombea mwingine wa nafasi hiyo, Msimamizi wa Uchaguzi, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
 
Haki itendeke. Ubatili; Uporaji na Utekaji. Hii ni nchi iliyostaarabika mbele ya mataifa mengine? Hii ya utekaji na uporaji wa fomu inafanyika Uganda, Kenya, Zambia, Malawi?
 
Polisi wanajidhalilisha mbele ya jamii na mbele ya mataifa jirani.

NEC wanatumika wasi wasi, NEC hawakemei matendo ya Wakurugenzi wa Wilaya (wasimamizi)
 
Agosti 25, 2020
M/Kiti wa NEC, Jaji Mstaafu Semistolces Kaijage kwa mamlaka aliyopewa amemteua Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mama Samia Suluhu kuwa mgombea wa kiti cha Makamu wa Rais kupitia CCM.
 
Ratiba inaonekana inaenda kwa Alphabetical ila cha ajabu sana kuna C moja iko juu ya A then sasa ndo mtiririko unaendelea, kwa nini CCM imekaa juu wakati ilipaswa kuwa katikati huko?

NEC kwenye kurejesha fomu nako kuna watu au vyama viko treated tofauti?
FB_IMG_1598343822499.jpeg
 
Ndugu fanya hivi kila kitu wa 500 x 5dakika kupiga kura kila mtu , hizo ni dakika 2500 gawa kwa 60dak hayo ni masaaa 60. je kura zinapigw asiku ngapi?

twende sasa na figa zao za 29,000,000 gagwa kwa vituo 80,000 sawa 360 wapiga kura kila kituo.

haya watu 360 x 5 dakika ni 1,800 dakika, haya gawa kwa 60dakika hayo ni masaa 30.
je hawa NEC wapo makini kweli?

je tukisema kuna mpango w akuiba kura utabisha vipi?

kw aidadi iliopo ya wapiga kura hata wakitokea nusu ya 29,000,000 tutaitaji 15Hrs kupiga kura.
Kifupi kuna wapiga kura hewa wengi sanaa sanaaaaa! zaidi ya nusu hapo ni wapiga kura feki.
 
Nimesoma mitandaoni kuwa siku ya kurudisha form za kuwania ubunge na udiwani ni moja nchi nzima.

Kama ni kweli sababu ni nini?

Hawaoni wanawapa wapinzani sababu za hata wakati mwingine kujiteka au kuuza mechi kwa kusingizia muda,au wagombea kujitengezea au kutengezewa mizengwe?

Kiukweli naona mwaka huu wapinzani wakigaragazwa bila huruma awe Lissu au member na wabunge wao wote.

Time kama ni kweli fanyeni mambo kisomi ili kama mtu ananyukwa hadi mtoto Mdogo ajue msimu huu kuna mtu kapigwa ndani ya box mapema asubuhi.

Kama sivyo ni uzushi mods mfute huu Uzi baada ya kuelimishwa
 
Ratiba inaonekana inaenda kwa Alphabetical ila cha ajabu sana kuna C moja iko juu ya A then sasa ndo mtiririko unaendelea, kwa nini CCM imekaa juu wakati ilipaswa kuwa katikati huko?

NEC kwenye kurejesha fomu nako kuna watu au vyama viko treated tofauti? View attachment 1547433
Kitabu cha Animal Farm kina majibu khs hilo.
 
Habarini wanajukwa.

Nimefuatilia huu mchakato wa kurudisha fomu na kuteuliwa, ila sijaona wakihakiki taarifa zilizo kwenye fomu hizo.

Swali, je uhakiki wa taarifa za fomu umefanyika? Umefanyika wapi na lini?

Kuna mgombea yeye fomu zake zimetolewa kwenye bahasha zilizokuwa zimefungwa, mpaka ikabidi bahasha hizo zichanwe.
 
NEC hatakiw kulaumiwa hata kama wata mkata Tundulisu kwa sababu Nec Ina mamlaka ya kuchagua watu wanao enda kushindana na sio kuchagua washind

Wote mnakumbuka kua Tundulisu amesha ongea wazi wazi kua endapo hato pita kwenye uchaguz apo October hato kibali lazima Ataingiza watu barabaran kauli ambayo inaonesha kabisa kua kichwan kwa Tundulisu Kuna jibu moja tu baada ya Matokeo kua yeye ni mshind na ikienda Tofaut basi hatokubali

Kwa hili Mimi nawapongeza Nec kwani wameangalia Taifa kwanza sababu Tundulisu na Genge lake wamejipanga kufanya vurugu kwenye uchaguzi.

Pia Tundulisu kuwekewa waiting Room ni somo kwake ili akitoka ndan baadae ajue kua ili upate kitu lazima ueshim Watu
 
Wakuu, kuna kazi hapa Dodoma imeanza rasmi saa 12 kamili jioni hii. Majina yanabandikwa kama mnavyoona.

Nimepitia majina na mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema ndugu Tundu Antipasi Lissu Limo
20200825_180838.jpg
 
Back
Top Bottom