Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi imevionya Vyombo vya Habari vinavyotangaza wagombea wamepita bila kupingwa Kinyume cha Sheria

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi imevionya Vyombo vya Habari vinavyotangaza wagombea wamepita bila kupingwa Kinyume cha Sheria

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
NEC imesema muda wa kutangaza wateule bado kwani kuna mapingamizi yanayoshughulikiwa na kwa mujibu wa ratiba mwisho wa kupokea mapingamizi ni leo 26 Agosti, saa 10.00 jioni. NEC imesema taarifa hizo zinaweza kupeleka uvunjifu wa amani



Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera amesema, hadi kufikia 6:32 mchana, tume hiyo ilikuwa haijapokea pingamizi lolote la nafasi ya urais. Mwisho wa kuweka pingamizi ni saa 10 jioni.

Agosti 25,2020 tume ilikamilisha uteuzi wagombea urais na makamu, ubunge na udiwani, hatujatoa taarifa yoyote juu ya zoezi hili, tayari vyombo vya habari kadhaa vinaaza kutoa matokeo ya uteuzi huu, hii ni kinyume na sheria” Dk.Wilson Mahera, Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC.

Mkurugenzi wa uchaguzi amesema haya... namnukuu

''Unapotangaza mtu amepita bila kupingwa hiyo inaweza pelekea uvunjifu wa amani pale mtu anapowekewa mapingamizi, isionekane ameshinda. Mimi mwenyewe mkurugenzi wa uchaguzi sijapata majina hayo rasmi''

''Kumekuwepo na dhana ambayo wanadhani watu wanakatwa, suala la uteuzi huwezi kukata mtu kwa matakwa yako, sababu tume inafanya kazi kwa kuzingatia kanuni, tumeweka masharti ya uteuzi kwa urais wa Tanzania, ubunge na udiwani''


Unapowekea mtu pingamizi au ukiona hakuteuliwa maana yake hajatekeleza masharti, mtu akitoa maneno nje ya masharti hatafanikiwa sababau huyu akitaka rufaa atashinda. Tume inafanya kazi kwa uwazi na uhuru .

EgWJM1bXsAAL0RW.jpg
 
Mkuu kuna shida mahali huko kwenye chama chenu.

Chonde chonde maelekezo mnawapa wakurugenzi yataleta shida kubwa sana kuanzia kwao wenyewe, familia zao, na taifa kwa ujumla.

Msifikiri polisi watawalinda kila mahali na kila saa, jitafakarini sana, haswa wakurugenzi.
 
Idadi ya vyama vyenye wagombea ambao wameripotiwa kufanya hivyo inafikirisha sana!
 
Mkuu kuna shida mahali huko kwenye chama chenu.
Chonde chonde maelekezo mnawapa wakurugenzi yataleta shida kubwa sana kuanzia kwao wenyewe, familia zao, na taifa kwa ujumla.
Msifikiri polisi watawalinda kila mahali na kila saa, jitafakarini sana, haswa wakurugenzi.
Tanzania ni nchi ya amani bwashee!
 
Tanzania ni nchi ya amani bwashee!
Hakuna amani mahali pasipo na haki wala uhuru mkuu.
Natoa tu angalizo, haya yanayoendelea hayatavumilika milele, itaanza vuguvugu ambalo ni passive, litafuata ambalo hata hao mnaowapa maelekezo watakimbia ama kuungana na ndugu zao kushinikiza haki na uhuru vichukue nafasi, hapo ndipo watu watahama nchi.
 
Ni vyema tume ikaongeza muda wa mapingamiza ikiwezekana ikawa siku tatu zaidi kulingana na hali halisi kwenye ground huku...taarifa zinazosikika zinahitaji hekima kidogo na busara ili kila mtu apate haki yake..
 
Ni vyema tume ikaongeza muda wa mapingamiza ikiwezekana ikawa siku tatu zaidi kulingana na hali halisi kwenye ground huku...taarifa zinazosikika zinahitaji hekima kidogo na busara ili kila mtu apate haki yake..
Umenikumbusha Morogoro mjini kasoro bahari!
 
Mimi na shangaa vya zaidi ya 14 wagombea wao hawajui kujaza fomu za ubunge na udiwani wanao weza ni CCM tuu
 
Kwahiyo ktk jimbo moja kuna wagombea wa vyama 15 kwahiyo wote wamekosea kujaza fomu au wamechelewa kupeleka fomu aliyewahi ni mmoja tuu
 
Wapeni salamu Job Ndugai, Kasim Majaliwa, Nape Nnauye, Abood
Waambieni wajiandae na kampeni na muda wa wahuni kama wao kupita KIJAMBAZI ulishapitwa na wakati.

Spika na Waziri mkuu wa nchi mnakuwa WAHUNI first class! Waambieni warudi majimboni wakaandae sera wapuuzi hao!
 
Wapeni salamu Job Ndugai, Kasim Majaliwa, Nape Nnauye, Abood
Waambieni wajiandae na kampeni na muda wa wahuni kama wao kupita KIJAMBAZI ulishapitwa na wakati.

Spika na Waziri mkuu wa nchi mnakuwa WAHUNI first class! Waambieni warudi majimboni wakaandae sera wapuuzi hao!
Bwashee usitukane mamba kabla hujavuka mto!
 
[SUP]NEC iwakemee na kuwaengua wakurugenzu wahuni walitoa baarua za 'kupita bila kupingwa' kwa wahuni wenzao wa CCM.[/SUP]
 
Back
Top Bottom