Kenya 2022 Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) inajitengenezea bomu kupitia kile wanadhani ni Uhuru wa Vyombo vya Habari

Kenya 2022 General Election
Kwanza umecopy hii habari twitter,pili kwa akili yako ilivyo ndogo bila kuichambua ukaileta huku uchukue point lakini umeandika utumbo.

Kenya ni mfano wa kuigwa katika hili hata kama kuna dosari ndogo ndogo zitatokea.
 
Wewe ilitakiwa kipindi magu anakufa na wewe uende naye...akili finyu kabisa hii..ulitaka wafiche kama NEC ili waibe?
 

Kwa hoja kama hizi ndio inaonyesha ni jinsi gani waTz tumepumbazwa kiakili na Serikali ya CCM

Wakenya wote wanajua Tume yao ndio itatoa matokeo halisi baada ya majumlisho yote
Lakini sisi makomdoo ya ccm tunaona bomu linatengenezwa....... hii nchi ya ajabu sana aisee
 

..ni utaratibu mzuri lakini unahitaji MABORESHO.

..VYOMBO vya habari vinatakiwa viboreshe huu utaratibu ili MATOKEO yakitoka ktk JIMBO fulani, basi vyombo vyote vinapata matokeo hayo kwa WAKATI mmoja.
 
Yaani wewe msukule wa ccm una akili kuliko time ya Uchaguzi wa Kenya. Hivi kwenye Uchaguzi kunahitajika usiri ili watu waibe kura. Kwa wenzetu wametuvua nguo kuona walikofika katika kiwango Cha democracy. Katika Uchaguzi huu.

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Sasa mtu akijumlisha 2+0+5+8+1 na mwingine akajumlisha 8+5+1+2+0 mwisho jibu si litakuwa Moja? Au shida ipo wapi? Huyu say kaanza kujumlisha Dodoma yule akaanza Kigoma mwisho wa siku aliyeanza Dodoma si atajumlisha na Kigoma na aliyeanza kigoma so atajumlisha Dodoma?
 
Pole sana ndugu The unpaid Seller .
Nimeona uchungu ulionao katikati ya maandishi yako.
Pole sana.
Asante mkuu, Mungu ni mwema kuna faraja kwake japo kuna mida kumbukumbu zikija mtu unahisi kutamani kufa nao wadhulumu yani kama mbwai iwe mbwai.

Mtu unawaza kama amekufa ndugu yako wewe unaishi ili iweje wangekuja wakaniua na mimi nisiteseke kwa kumbukumbu hizi.
 
Hongera kwa thread. Kwa mtazamo wako unadhani hawa jamaa wana mtazamo kama wako? Kwamba hawajaliona hilo?
 
Nadhani kuna jambo umeliacha! Na umezongwa na taswira ya chaguzi za Tanzania (mostly). Kinachofanywa Kenya hakitoharibu jambo lolote kwasababu kura hazibadiliki kinachotokea ni vituo vinatofautiana kutokana na speed ya ujumlishaji matokeo! Lakin mwisho vyote zitakua na matoke sawa!
 
Wanafiki tu hao wanajifanya wanademokrasia
 
Bora ukae kimya kuliko kujidhalilisha

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Kwanza umecopy hii habari twitter,pili kwa akili yako ilivyo ndogo bila kuichambua ukaileta huku uchukue point lakini umeandika utumbo.

Kenya ni mfano wa kuigwa katika hili hata kama kuna dosari ndogo ndogo zitatokea.
Mfano upi, kupigana na kuchinjana kila uchaguzi?, Sasa mbona vyombo vyote vimeacha kurusha matangazo baada ya kuonekana Kuna dalili za mparaganyiko?

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Hamna bomu mkuu..
Umezoea uchaguzi wa kwenu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…