Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

umefutwa, ni baada ya Maalim Seifu kujitangazia ushindi, bila kufuata utaratibu

Hio si sababu sababu ni kushindwa kwa ccm nothing else, na walikusudia wamtangaze sheni kwa nguvu ila kusingekalika, ccm ni madhalimu wakubwa walaaniwe popote walipo
 
Katika hali ya kushtua Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar(ZEC) imetangaza kuyafuta Matokeo ya urais wa Zanzibar.

Yadaiwa Uchaguzi uligubikwa na kasoro nyingi.

Imeahidi kutangaza tarehe rasmi ya kurudiwa uchaguzi.

Chanzo: ZBC TV

kwani ZEC ni mahakama? je, ni nani aliyelalamika kwamba uchaguzi umegubikwa na dosari? inawezekana DOSARI ni UWEZO MDOGO WA ZEC KUSHINDWA KUCHAKACHUA MATOKEO. ngoja NEC wamalize kuchakachua huku bara halafu waende kuchakachua kule zanzibar. naona ZEC wanataka kutuletea machafuko yasiyokuwa ya lazima. haiwezekani matokeo ya urais yakataliwe wakati matokeo ya ubunge, uwakilishi, udiwani na usheha yakubaliwe.
 
Zanzibar Electoral Commission (ZEC), hivi punde, imeyafuta matokeo yote ya Urais ya Visiwani Zanzibar katika kile kilichosemwa kuwa yalikuwa na kasoro nyingi. ZEC imeahidi kutangaza tarehe nyingine ya kufanyika upya kwa uchaguzi huo wa Rais wa Zanzibar.

Hata huku Tanzania Bara, katika Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuna manung'uniko mengi juu ya matokeo yanayoendelea kutangazwa na National Electoral Commission (NEC). Vipi napo hatua kama ya Zanzibar ikachukuliwa kumaliza fukuto lililopo?

ZEC imeonesha njia. NEC mko wapi nanyi mfanye jambo? Tanzania inapaswa kuwa moja: ya amani, utulivu na mshikamano. Mambo ya uchaguzi, kuyarudia, si mambo mageni. Ni mambo yetu na kwa mustakabali wetu kama Taifa la Tanzania. NEC, chukueni hatua!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Vipi kuhusu BAra?
Nasisi tutasubiri au tutarudia?
Naomba kuelimiswa hapa.
 
Sheria za Uchaguzi/ Maadili ya Uchaguzi yanasemaje kuhusu adhabu ya mgombea anayejikasimu madaraka ya Tume? Wangemfutia matokeo take tu!
 
Hatimaye ZEC wamefitilia mbali uchaguzi wa Zanzibar.

Kwa mujibu wa tangazo la ZEC wameainisha mambo mawili ambayo yamepelekea kufutwa kwa uchaguzi huo ambayo ni mgombea mmoja kujitangaza mshindi kinyume cha taratibu na jambo lingine wamedai kuwa uchaguzi huo haukuwa wa huru na haki.

Wajiuzulu basi kama wameshindwa kuufanya uchaguzi uwe huru na haki
 
Kama uchaguzi haukuwa wa huru na haki, bado watataka wasimamie ukirudiwa tena? Iwapo taarifa hii ni ya kweli Tume pia ifutiliwe mbali na Tume mpya ibuniwe yenye uwakilishi(representatives) wa vyama vyote pamoja na wadau wengine.

Kwa maana hiyo majumuisho ya kura ya Urais nayo yatasimama mpaka uchaguzi urudiwe???? Je Rais wa JMT hatapatikana mpaka uchaguzi wa Zanzibar urudiwe?
 
katika hali ya kushtua tume ya uchaguzi ya zanzibar(zec) imetangaza kuyafuta matokeo ya urais wa zanzibar.

Yadaiwa uchaguzi uligubikwa na kasoro nyingi.

Imeahidi kutangaza tarehe rasmi ya kurudiwa uchaguzi.

chanzo: zbc tv

..........jesus ....!!
 
Bara kuna mtu alisema tuna muapisha magufuli tarehe 29/10 kabla hata rais hajajulikana, Je hiyo haikuwa kujitangazia ushindi?

Sio kuna mtu ...Januari Makamba alitangaza kwamba Magufuli kashinda na atatangazwa kama raisi mteule tarehe 29 October!
Halafu ati anajitetea kwamba na ukawa walisema watachukua nchi asubuhi...anadhani sisi ni malofa saaana hatujui tofauti ya sheria kwa kuongea kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi
 
Mungu atafanya kila njia, pamoja na hii iliyotokea sasa, ili haki ipatikane. Its very important to respect the will of people in the Ballot Boxes.

Naomba Mungu tubaki wamoja, tamaa za madaraka za upande wowote ule zisituingize kubaya, Mungu wetu na aingilie. Amina.
 
Back
Top Bottom