justus emily ndyanabo
Member
- Dec 30, 2015
- 32
- 25
Ghana oyeeeee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera kwa uchambuzi mahiri, uzalendo , kupenda Nchi na kufikiri nje ya boksi! JPM anatosha kiongozi bora Afrika 2020. Nana Kaiba kura Juzi tu Disemba 2020 watu wamepigana Bungeni.RAIS MAGUFULI NI BORA KULIKO RAIS NANA AKUFO-ADDO WA GHANA; TUZO TUIREJESHE KWETU
Na: Suphian Juma
Jarida la African Leadership ambalo husaidia kuinena vema Afrika duniani, linaendesha zoezi la upigaji kura. Katika kipengele cha Kiongozi Bora wa Kisiasa Afrika yaani AFRICAN POLITICAL LEADER OF THE YEAR; Rais wetu Magufuli yumo akiwaacha mbali MaRais wa Senegal, Afrika Kusini, huku akipitwa kura kiduchu na Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo katika upigaji kura unaoendelea mtandaoni.
Naona baadhi yetu Watanzania wanampigia chapuo Nana, nadhani hii ni kwa sababu aidha hawajawahi kuishi Ghana ya Nana, hawajazisoma vema siasa za Ghana ama basi tu ni chuki zao binafsi kwa Rais wetu Magufuli.
Wasiojua Nana ndiye Rais wa kwanza wa Ghana kukopa fedha nyingi zaidi kuliko Rais yeyote tangu Ghana ipate Uhuru. Shirika la Fedha duniani (IMF) limetamka kwamba deni la Ghana linakadiriwa kufika 74.7% kufikia mwaka huu wa 2021. Huyu Rais wa madeni ambaye anawaumiza wananchi wake maskini kulipa madeni hayo atafaaje kuwa bora kuliko Rais wetu Magufuli?
Nana anakadiriwa ndiye Rais ambaye hadi sasa ndiye mwenye mawaziri wengi zaidi kuliko Rais yeyote duniani. Yaani Baraza la mawaziri lake lina jumla ya mawaziri 125 achilia mbali Manaibu waziri wake. Fikiria mishahara yao na marupurupu yao katika nchi ndogo kama Ghana yenye jumla ya watu milioni 30. Sisi Tanzania tupo milioni karibia 60 yaani mara mbili ya Ghana ila Rais Magufuli hata mawaziri robo ya mawaziri wake Nana hatujawahi kuwafikisha. Maana hadi sasa Rais Magufuli ana mawaziri 23 tu.
Kingine cha kutia huzuni Ghana ya Nana ni AJIRA. Unaambiwa Ghana kijana kupata kazi Serikalini au hata kwa Taasisi binafsi ni kizungumkuti. Mwandishi wa DW wa Ghana Manasseh Azure Awuni katika uhariri wake uliochapishwa Desemba 10, 2020 anasema
ni rahisi kijana kubebeshwa mfuko wa saruji shingoni mwake na akapita bahari ya Atlantiki ila si kijana huyo kupata kazi Ghana katika utawala wa Nana Akudo-Addo. Sasa tujiulize Nana Serikali yake kukopa kote huko kwanini pasisaidie kutatua janga la ajira? Nana ni msanii.
Huku kwetu tangu Rais Magufuli aingie madarakani tukiweka unafiki pembeni, hakika viongozi wamekuwa na adabu kwa wananchi. Hali haiko hivo kwa Nana. Wachambuzi wa Siasa walioko Ghana wanasema Mghana wa kawaida hana mamlaka ya kummwajibisha Kiongozi isipokuwa tu hadi ifike muda wa uchaguzi kupitia kura yake sandukuni. Ila huku kwa Mzee Magu, mwananchi wa Buza kwa Mpalange alitukanwa tu na M/kiti wake wa Mtaa, mwenyekiti huyo kazi hana.
Mfano wa hili la kukosekana 'accountability' kwa Viongozi huko Ghana; mwaka 2019 Mwandishi wa Habari za Uchaguzi wa Ghana Ahmed Hussein-Suale alipigwa risasi na kufa Accra. Kabla ya kuuawa Ahmed alitishiwa kifo na Mbunge wa Chama cha Nana, na hadi sasa si Polisi wa Nana wala vyombo vyake vya Ulinzi na Usalama ambavyo vimewahi kutoa matokeo ya uchunguzi wala kumwajibisha huyo Mbunge ambaye alimtishia kifo Ahmed.
Nana si muumini wa Utawala bora wala wa Uhuru wa vyombo vya habari; Imagine Julai mwaka jana Rais Nana aliamuru kuachishwa kazi Mhariri Mkuu wa Chombo cha habari nchini humo aitwaye Daniel Domelevo licha ya kukatazwa na Asasi za Kiraia kisa tu Mhariri huyo aliruhusu habari irushwe iliyohusu ukaguzi wa Mali za kifisadi za Waziri wake aliyemtegemea kwenye Baraza aitwaye Yaw Osafo-Maafo.
Kiufupi Rais Nana Akufo-Addo ana udhaifu mkubwa mno katika maeneo ya utawala bora na katika vita dhidi ya ufisaidi ukimlinganisha na jembe letu Magufuli. Demokrasia ya kweli lazima iambatane na Utawala bora, uwajibishwaji wa Viongozi na Serikali huku matatizo makubwa kama ajira na maisha bora kwa wananchi yakitekelezwa kikamilifu ila haya kwa Nana bado ni mtihani Mkubwa.
Na isitoshe kusema: uchaguzi wa Ghana ambao ulipita mwaka jana bila kumwaga damu, nyumba na mali za watu kuchomwa si kigezo pekee cha kupima ubora wa Kiongozi. Ghana wana vyama viwili ambavyo ni pacha tofauti ni majina tu NPP ya Nana na NDC ambavyo huachiana madaraka kila uchaguzi; kimoja kikiwa upinzani kinaonekana bora kwa kukisema kilichopo madarakani lakini maisha ya raia wa kawaida ni magumu mno. Huku si kukomaa kwa demokrasia bali kudumaa kwa demokrasia tofauti na tunavyoaminishwa na wanaharakati mtandaoni.
Hivyo nawaombeni kura zote tumpigie Rais wetu Magufuli ambaye ni mchapakazi wa kweli, msimamizi makini wa kodi zetu na mwendelezaji wa miradi mikubwa ya wananchi wake, na kinara wa Utawala bora unaompa mwananchi wa kawaida fursa ya kummwajibisha Kiongozi wake muda wowote kuliko kusubiri wakati wa uchaguzi kama huko kwa Nana Akufo-Addo wa Ghana.
Bofya: https://t.co/xhDotKvYzI?amp=1
Mwisho wa kupiga kura ni Januari 8, 2021. Wahi sasa tuing'arishe Tanzania yetu duniani.
Suphian Juma Nkuwi,
Mtanzania Halisi,
Januari 06, 2020
Phone: 0717027973
Email: yessuphian@gmail.comView attachment 1669966View attachment 1669967
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Una hasira sana dogo,! Una fikiri kushinda uchaguzi ni sawa na kushinda umonitor wa darasa la nne?
Si umeona kwa bwana zenu usa mlikofikiri mtapata msaada wamekufa watu 4 kisa uchaguzi?
Usifikiri kwamba mlivyoparaganyika hapo ufipa basi ni tz nzima.
Kawadanganye Lumumba, sjyo kweli. Hata hivyo mtu wenu keshashindwa na Rais wa Ghana. Angalia kuraWaghana jana wameandamana na kuvamia Bunge Nana amewaibia kura wewe unamuona kiongozi bora ,wonders will never end!
Sema anaongoza siyo kashinda, sina haja ya kumdanganya mtu yeyote! Nini kimetokea uchaguzi wa Ghana 2020 , na jana Bungeni?! Chuki binafsi na kukosa uzalendo zisitawale maisha yako mkuu.Kawadanganye Lumumba, sjyo kweli. Hata hivyo mtu wenu keshashindwa na Rais wa Ghana. Angalia kura
Uzalendo tafisiri ya Lumumba hainihusu. Chuki mmepandikiza nyinyi sasa ni majira ya mavuno.Sema anaongoza siyo kashinda, sina haja ya kumdanganya mtu yeyote! Nini kimetokea uchaguzi wa Ghana 2020 , na jana Bungeni?! Chuki binafsi na kukosa uzalendo zisitawale maisha yako mkuu.
Kuliko masaubwileKupiga kura ni mara moja tu. Labda uwe na simu nyingi kama kocha wa JKT Ruvu
Huyuhuyu ambae jeshi limevamia bunge kutuliza vurugu?Najua saa hii uko hapo kibarazani ikulu unachangia hapa jf. Nimecheka kwa nguvu. Nana Akufo ndio rais bora Afrika.
Huyo huyo.Huyuhuyu ambae jeshi limevamia bunge kutuliza vurugu?
Watanzania wakiibiwa kura wanaweza kuamdamna?Waghana jana wameandamana na kuvamia Bunge Nana amewaibia kura wewe unamuona kiongozi bora ,wonders will never end!
The point is Magufuli si mstawisha demokrasia bali mwaribifu wa demokrasiaUmeandika ujinga!
Ndio maana huwa nasema mtaendelea kugongwa na ccm sababu hamjitambui!
Kwanza raia wapi wanamoshabikia rais wa nje? Hao wajinga wachache wa twiter kina kigogo, hilda newton, fatuma, sarungi na wapuuzi wa aina yao?
Hao si hata kwenye uchaguzi mkuu walisema bora wampigie mbwa kuliko ccm?
Endeleeni na ujinga, ila 2025 jueni kipondo kipo palepale.
Ghana bado wanao uhuru wa kuandamana hata wale wanaotofautiana na serekali yao.Mumekariri tu, embu nenda forum ya internation huko uone kinachoendelea Ghana leo hii..! Jeshi na police wameingia bungeni huko
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwingine alikodi kabisa wanajeshiHuyuhuyu ambae jeshi limevamia bunge kutuliza vurugu?
sasa si bora huyo anayevamia bunge kutuliza tu vurugu, huyu amekwenda mbali zaidi (usiniulize anawafanyaje labda ukiweza muulize Tundu Lisu!!!!).Huyuhuyu ambae jeshi limevamia bunge kutuliza vurugu?
Safari hii atajua kuwa hajui. Uzuri mwizi mkishamjua haisumbui maana hata kumsogelea hamumsogelei asije kukuchomolea.Huyu ataiba kura hata za online atashinda tu hakuna haja kumpigia.
The president elect in Ghana Nana Akufo Addo is too weakl in leadership can't manage to contain the enemies of the country and he sits on a burning chair that his pretence he respects peoples freedom of speech will tear apart the nation diffuclt to integrate it.
Hamna kitu hapo.VOTE COUNTS AS FOR TODAY AT 21:00
View attachment 1672044
Kesho tarehe 8/1/2021 saa 23:59pm ndiyo mwisho wa kupiga kura..
Wote ambao mnaamini JOHN P. MAGUFULI hajawahi kushinda uchaguzi kuanzia ubunge hadi Urais fairly and squarely tupige kura kwa wingi katika saa hizi takribani 24 zilizosalia tumkatae na dunia ijue hivyo kuwa wananchi wake mwenyewe wamemkataa...