Tumsaidie Steven Mdoe aka Dj Steve B anaumwa sana

Tumsaidie Steven Mdoe aka Dj Steve B anaumwa sana

Nimesikiliza interview yake Global tv ikanisikitisha sana. Mahojiano yale yanafikirisha sana na ili kutoleta sintofahamu au kutokuelewana bora kuyaacha ili wadau wamsaidie apate matibabu.

Ila tujifunze kuwa siku yatakapokuja kukupata ya kukupata, ni familia yako ndio itayoangaika na wewe. Uzima na nafasi yako ndio kitu kinachofanya uheshimiwe na vikitoweka wote wanaojifanya kukupenda hutowaona.

Fikiria DJ Steve B akiwa active pale Clouds alikuwa anafuatwa na wangapi awasaidie? Alikuwa na marafiki including wasanii wakubwa wangapi? Simu ngapi zilikuwa zikiita kila dakika? Imagine yule ni icon wa XXL kipindi kikubwa mno cha vijana Tanzania, Kuna wakati ndio alikuwa DJ tegemeo na kichwa pekee pale Clouds baada ya Boniluv kuacha lakini sasa yupo peke yake akihangaika na ndugu zake!

Tuwe karibu na familia zetu na hasa muumba wetu. Sometimes tunaishi kama tutaishi milele, mtu hata hukumbuki hata lini mara ya mwisho kukanyaga Kanisani/msikitini! Hata ule utii na nia ya kushirikiana na Kanisa au waamini wenzako huna time zaidi ya kukimbizana na dunia!

Kama Mungu anakuhitaji na wewe mkaidi anaweza kutumia hata njia ngumu sana kukurudisha kwake kama alivyomfanyia Yona. Una siku saba za wiki tenga siku moja ya kuhudhuria ibada, kila siku omba/mshukuru Mungu hata kwa dakika chache, itakujenga na kukuokoa na mengi.

Tujitahidi kumsaidia ndugu yetu Steve B kwa kila hali ili arejee afya yake. Nimeona huruma sana. Kristo kupitia mateso na madonda yake pale msalabani amponye ndugu yetu.
Ubarikiwe kaka
 
Gharama za matibabu ya figo NHIF hawawezi kutoa,sababu ni kubwa, gharama za kusafisha figo ni zaidi ya laki tano kwa wiki.
Kila wiki unatakiwa usafishe mpaka hali itapotengemaa.
Jiepushe kuongea mambo usiyoyajua vizuri kwenye mitandao kiongozi...
NHIF hiyo huduma ipo
 
Jiepushe kuongea mambo usiyoyajua vizuri kwenye mitandao kiongozi...
NHIF hiyo huduma ipo
Miaka mitatu nilisikia intv ITV wagonjwa wa Figo wakihojiwa hii huduma haikuwepo,labda hivi sasa na hata ikiwepo labda kwa mchangiaji na si mtegemeaji.Wewe mtegemeaji hata miwani hapewi anaishiwa kupimwa basi miwani utanunua mwenyewe.
 
Nataka kutuma Tsh. 3,000,000/= kwa namba hiyo
 
Madj wenzake na clouds waandae tamasha moja linatosha kumsaidia muda upo ila naona iko shida cmg....clouds huwa wanabeba kitu na kukifanya kwa haraka ila kwenye hili sioni

Sent from my SM-G7102 using JamiiForums mobile app
Utajua kwann walimlilia ruge kwa sauti sana. Jamaa ndio ilikuwa engine ya maarifa leo clouds unaiona ipo ipo tu hakuna ubunifu wowote unaofanyika, ukiona mtu anakufa kwa mshtuko wa kifo cha mwingine jua the true mastermind is gone.
 
Nimesikiliza interview yake Global tv ikanisikitisha sana. Mahojiano yale yanafikirisha sana na ili kutoleta sintofahamu au kutokuelewana bora kuyaacha ili wadau wamsaidie apate matibabu.

Ila tujifunze kuwa siku yatakapokuja kukupata ya kukupata, ni familia yako ndio itayoangaika na wewe. Uzima na nafasi yako ndio kitu kinachofanya uheshimiwe na vikitoweka wote wanaojifanya kukupenda hutowaona.

Fikiria DJ Steve B akiwa active pale Clouds alikuwa anafuatwa na wangapi awasaidie? Alikuwa na marafiki including wasanii wakubwa wangapi? Simu ngapi zilikuwa zikiita kila dakika? Imagine yule ni icon wa XXL kipindi kikubwa mno cha vijana Tanzania, Kuna wakati ndio alikuwa DJ tegemeo na kichwa pekee pale Clouds baada ya Boniluv kuacha lakini sasa yupo peke yake akihangaika na ndugu zake!

Tuwe karibu na familia zetu na hasa muumba wetu. Sometimes tunaishi kama tutaishi milele, mtu hata hukumbuki hata lini mara ya mwisho kukanyaga Kanisani/msikitini! Hata ule utii na nia ya kushirikiana na Kanisa au waamini wenzako huna time zaidi ya kukimbizana na dunia!

Kama Mungu anakuhitaji na wewe mkaidi anaweza kutumia hata njia ngumu sana kukurudisha kwake kama alivyomfanyia Yona. Una siku saba za wiki tenga siku moja ya kuhudhuria ibada, kila siku omba/mshukuru Mungu hata kwa dakika chache, itakujenga na kukuokoa na mengi.

Tujitahidi kumsaidia ndugu yetu Steve B kwa kila hali ili arejee afya yake. Nimeona huruma sana. Kristo kupitia mateso na madonda yake pale msalabani amponye ndugu yetu.
Umeongea vizuri sana mkuu,kiburi cha uzima kinaponza wengi sana...
 
"Sitivuu biii, ni wewe nasababisha muji kutishingika kinoooma nooma tupa sisi rubudaniii...asaaanduuu" hahaha ilikuwa ni jingle jmosi bongoflava clouds fm kuanzia ngoma nne hivi...
 
Mkuu Mimi Nina utapeli gani? Namba ya simu ambayo nimeiweka ni ya DJ Steve b mwenyewe nimeiweka baada ya yeye mwenyewe kuitaja kwenye interview, pitia interview yake you tube aliyofanya na global publishers. Usiwe mwepesi wa kuhukumu, pengine we we ndo tapeli mkuu.
Weka link ya hiyo video wengine hatujaiona bro.
 
Huyu bwana kuna kipindi fulani cha nyuma tulikuwa majirani hapo dsm, wakati huo anafanya kazi CMG, naweza kusema alikuwa ni mtu muungwana sana mnyenyekevu mno, kutoa ni moyo wadau tumsaidie kadiri tunavyoweza.
 
Back
Top Bottom