Tumshauri kijana huyu cha kufanya, muda bado upo

Tumshauri kijana huyu cha kufanya, muda bado upo

Ajaribu kazi za vibarua viwandani na Katika miradi ya ujenzi, huko ndiko mimi kulikonilea. Ingawa asione aibu kupokea 2500 mpk 7000 kwa siku na akikuta anatumwa na watu wa standard 7 na pia wanakula mshahara mnono kuliko yeye. Mi nilichekwa sana ati msomi unafanya kazi moja na asiyesoma, nilivumilia ila mwishowe nilizoea na wakaanza niita professor
😄😄 Walikubali wenyewe.
 
Asante Mungu mwaka wa tano bila ajira,watoto wawili na mke. Watakula nini,watavaa nini,shule wataendaje?

Maswali hayo na mengine mengi kuhusu wao sijawahi kujiuliza kwasababu wakati nafanya uamzi wa kuwa na familia sikuwahi kujiuliza hayo yote lakini kuamini katika kujituma kwenye kazi yoyote halali ndyo chanzo cha wazo la kuanzisha familia.
 
Asante Mungu mwaka wa tano bila ajira,watoto wawili na mke. Watakula nini,watavaa nini,shule wataendaje?

Maswali hayo na mengine mengi kuhusu wao sijawahi kujiuliza kwasababu wakati nafanya uamzi wa kuwa na familia sikuwahi kujiuliza hayo yote lakini kuamini katika kujituma kwenye kazi yoyote halali ndyo chanzo cha wazo la kuanzisha familia.
Big up soja.
Unashauri tuwe na familia bila kujipanga?
 
Nyeto mkuu Tlaatlaah asiache.... Although Kuna gepu moja kubwa sana watu wamlisahau. Gepu hili lipo kwenye innovation! Nguvu ya kuzitumia kusaka ajira zitumie kubuni miradi au njia mpya...


Vipindi vinavyoruhswa dstv, clouds nk ni ubunifu. Hivyohivyo vifurushi kama jipimie... Nk ni watu wanabuni, wanaacha impact na wanasogea!. That's all!
huwa nina mawazo ya kusaidia jamii ya kutengeneza mfumo/ sytem bt uwa nakosa nianzie wapi
 
Tokea 2015 mpaka sasa kwavile hajafa njaa, maana yake hela anaingiza. Je, anafanya mishe gani kwa sasa?

Anaishi wapi?
Mkuu Analyse,
siyo mtu moja ama wawili katika hili,
Ni kundi kubwa kidogo, miongoni mwao binafsi ninawafahamu. Wengine ni ndugu zangu, jamaa na marafiki zangu. Wengine tulisoma shule pamoja na hata michezo ya utotoni tuliicheza pamoja. Yawezekana pia unao.

Sasa ni watu wazima kiasi, social life forces marika zimewatupa mkono kidogo, si unajua zile lazima uvae pamba kali, raba kali, uchukue demu mkali wiki hii, wiki ijayao mwingine, club kila alhamisi na Jmos. Japo hizo forces bado zipozipo lakini umate umate unapiga breki kama zote.....

Na sasa hivi umri umekimbia kidogo. Real Life forces ndio hivyo tena zimeanza na zinahitaji kijana awajibike na hana namna.
Lakini kabachelor degree kako mfukoni.......

Mfukoni kijana hana jambo,
akilini kwa kijana, moja haikai mbili haikai....

kijana huyu hivi sasa bado yupo mjini anaishi kwa uncle, unt, shemeji, bamkubwa, bamdogo na washkaji kitaani tangu alipokuja mjini kusoma chuo na tangu amalize chuo miaka hiyo hajapata ajira mpaka sasa....

Katika ujumla huo ndipo, nikaomba nasaha na ushauri humu jukwaani kwajili ya kijana huyu, ili aondokane na huo mkwamao....
 
Nikipita maeneo ya vyuo vikuu i.e UDSM,TIA,SAUT etc nikaona wanafunzi wanaenda madarasi kusoma hua nasikitika Sana.

Yajayo hayatawafurahisha.
Hpn wacha watoto wapate elimu bhan kwanin uogope mungu ndio anapanga na kutoa risiki Ni vyema wakasoma kuliko kuto kusoma kbsaa
 
huenda wamo humu, na bila shaka watakucheki wakiwiwa kufanya hivyo
Hyo Hali ya huyo kijan ilishanipitia na kwa Sasa maisha yanaenda ingwa kwa Kweli yake limezid mnk ,,mm wakt nawaza hayo Nina kiwanja Cha dhamani ya milion 15 HV japo nilikuwa Sina maisha kabsaa


Tumatafutie kibarua kisha atarecover tu mungu ni mwema mno
 
Almanusura niseme ni ww[emoji848]lkn nikakumbuka siyo ww bn we ni mleta mada tu!

Kwa mtu aliemaliza chuo 2015 saiv atakua na miaka 30+ sio umri mbaya sana ukituliza akili, kwa miaka 8 uliyokua mtaani Kuna jambo utakua umeligundua na unaweza lifanya either mjini au kijijini kafanye kwa moyo wote.

Epuka kujiweka karibu na siasa na wanasiasa, achana na mawazo ya kujiweka karibu na makada wa chama flan ukiamini kwenye uteuzi, kua low key fanya yako siasa ina wenyewe

Epuka mahusiano kama hujaoa usihangaike piga kazi zako chora ramani vzr kila unachokifanya fikiria namna inaweza kukupa Hela sio kupoteza Hela.

Baki kwenye Imani yako acha kuwaza miujiza, acha kuwaza laana/baraka, acha kuwaza unachopitia ni majaribu, sali kwa Imani yako ishi vzr na watu Linda amani ya moyo wako.

KWA SAIVI NIISHIE HAPA
Mm baada ya kuhahah San baadae nikatulia akili ndipo nikapata njia sahih na vitu vya kufanya na kuningiziaa pesa aambovyo nilipata experience mtaani
 
Naomba Sana mshauri kijan huyo aanze Mara moja ufundi wa simu itamsadia saan kuokotaa okota
 
Mkuu Analyse,
siyo mtu moja ama wawili katika hili,
Ni kundi kubwa kidogo, miongoni mwao binafsi ninawafahamu. Wengine ni ndugu zangu, jamaa na marafiki zangu. Wengine tulisoma shule pamoja na hata michezo ya utotoni tuliicheza pamoja. Yawezekana pia unao.
Nilidhani upo specific na mtu mmoja, kumbe unaongelea collectively?

Watu wa hivyo wapo wengi, na huwezi toa ushauri au solution collectively, it won't work.
 
mpe njia kijana kwa uwazi na upendo kabisa...

usimfiche,
hapo aepuke kua karibu sana na makada wa chama Fulani, muelekeze akiambatana na chama kipi sasa atapata ahueni ya mahangaiko yake na kamwe asithubutu kuambatana nao🤓, na kwakweli utakua umemsaidia sana kiasi kama ni msaada..

Na miaka 8 aendelee kujifariji, kung'ang'ana na kukomaa apoapo alipo kusaka kuajiriwa? Au akacheki na maeneo mengine mbali kidogo lakin ajitose kujiajiri pia?

Umenikonga sana kumshauri kijana ajiepushe na mahusiano ambayo for sure ni kupteza pesa tu hali ya kua hana ajira. Badala yake apige kazi kwa bidii na kujijengea uchumi wake mwenyewe utakae muwezesha sasa kutafuta mchumba na hata mke amtakae kwa ujasiri mkubwa. Maana uchumi ni nguvu na uchumi ni ujasiri.

Human being are political Animals.
Siasa haiepukiki.
If you don't want to take part in political administration don't blame to be ruled by a fools.

Kila kitu kwa kasi, kiasi na viwango tajika na hakika tutafika...
Word....👊👊👊
 
Back
Top Bottom