Kwenye vutana vutana inayoendelea nchini kuhusiana na chanjo ya UVIKO-19, nimepata nafasi ya kuwafahamu viongozi wetu wanaotuongoza na maneno yao wanayosema kila siku.
Hayati JPM alijua siri ya Corona na akatwambia ukweli mtupu kwa nia njema kabisa. Kipindi chote alichokuwepo hakuwahi kamwe kupindisha maneno yake katika kile alichokijua na kukielewa, alitahadharisha watanzania kuhusu vitu vinavyotoka nje. Msimamo wake ndio uliolivusha taifa na kuonekana la tofauti na kipekee ulimwenguni, na kuchochea maendeleo mpaka taifa likaingia uchumi wa kati. Hapa nchini, shughuli ziliendelea kama kawaida utadhani korona haikuwepo kabisa.
Rais Samia ameonesha kutokuwa na msimamo katika maneno yake. Alipokuwa makamu wa rais, msaidizi wa kwanza wa rais JPM, alionesha kuwa na uelewa kwenye jambo linaloendelea duniani na alisisitiza watu kumtegemea Mungu. JPM hayupo, amepiga kona ya nyuzi 180; amemwacha Mungu na ameamua kuwategemea wazungu, mabeberu ambao awali alisema walikuwa wameanza kumtegemea Mungu kama sisi. Watu tuliokuwa tunaishi vizuri ameturudisha kwenye mijadala ya Corona na chanjo.
Unaweza kumwamini kiongozi kama huyu anayebadilika? Kiongozi wa hivi si anaweza kuuza nchi na watu wake kabisa? Kama kweli ni rais wa nchi, aliyeapa kuilinda nchi na watu wake, kwa maslahi gani hasa anayafanya haya? Huyu kweli ni mzalendo kwa taifa lake? Tafakari.
SAMIA AMETUKOSEA SANA WATANZANIA
Waziri wa Afya ni kigeugeu na mtu hatari sana kwa taifa letu. Wizara inaongozwa na mtu ambaye kipaumbele chake ni ajira yake. Amenukuliwa mara nyingi akilalamika kwamba watu wanaojaribu kumchallange wanahatarisha ugali wake. Huyu ni mchumia tumbo tu huyu. Anajua jinsi chanjo zilivyo hatari lakini amepiga U-turn na kuzikumbatia kwasababu tu anataka kumfurahisha rais ili alinde kibarua chake hata kama watanzania wataangamia. DR DOROTH BORA UBWAGE MANYANGA WEWE NI MNAFIKI
Mtu pekee nchini ambaye tangu ameanza kuongea hajawahi kabisa kupindisha maneno yake ni ASKOFU GWAJIMA. Binafsi sikuwa nimemfuatilia sana enzi za nyuma kabla ya kuwa mbunge. Lakini nimegundua msimamo wake juu ya korona na chanjo ni ule ule kabla ya kuwa mbunge na baada ya kuwa mbunge. Maneno ya Askofu Gwajima sio ya kuandikiwa na mtu, sio ya kusoma kwenye karatasi, sio ya kumfurahisha mtu. Maneno yake yanaonesha anajua kitu fulani ambacho muda wote yuko tayari kuhatarisha hata maisha yake ili kuokoa kundi kubwa lililo hatarini ambalo halijui undani wa korona na chanjo. Amedhihirisha kuwa mtu thabiti asiyeyumba.
Ukifuatilia kwa karibu, utagundua Askofu Gwajima ameanza kuongea mambo yanayotokea hivi sasa tangu mwaka juzi. Na aliyoyaongea, taratibu yanaanza kutokea, ingawa watu wengine waliyapuuzia na kuyabeza. Anayatoa wapi mambo haya? Mtu wa namna hii ni vizuri kumsikiliza na kuwa makini naye kwa sababu inaonekana vyanzo vyake vya taarifa ni vya uhakika.
Aliwahi kusema itafika mahali kama mtu hajachanjwa hataruhusiwa kuuuza au kununua vitu. Jana tu taarifa inazunguka inayoonyesha rais wa Ufaransa akisema mtu ambaye hatachanjwa hataruhusiwa kununua vitu. Tunaelekea wapi?
Askofu Gwajima mwanzoni kabisa wa korona alisema Tanzania itachukua msimamo wa tofauti, na huo msimamo tofauti utaipaisha juu kiuchumi. Haikupita mwaka, Tanzania iliingia Uchumi wa Kati na watalii walikuwa wanakuja kwa wingi kipindi ambapo nchi nyingi zilikuwa zimefunga mipaka yake.
KAMA ALIYOYASEMA ASKOFU GWAJIMA YAMETOKEA, MANGAPI ANAYAJUA AMBAYO HAJAYAWEKA WAZI BADO?
Watanzania wa leo sio wa jana; ukisoma maoni ya watanzania wengi, utagundua kuwa walisubiri mtu atakayejitoa muhanga kuwanasua kutoka kwenye mikono ya viongozi wao wanaotaka kuwachanja kitu kilichokataliwa na waliokileta.
Gwajima anajua kuwa hiari inayosemwa ni mtego, baadaye chanjo itakuwa lazima kama waliotayari kuchanja kwa hiari wataisha; dawa ni kila mtu kugoma kuchanja.
Lakini pia Gwajima ameshauri serikali ianze kufanyia utafiti wa kutengeneza chanjo hapa nchini, maana hata wale wanaosukumiza chanjo huku Afrika hawaamini chanjo za mataifa mengine.
KWA NINI SERIKALI ISIZINGATIE USHAURI WA KUTENGENEZA CHANJO HAPA HAPA NCHINI?
Serikali isipambane na Askofu Gwajima, nyuma yake kuna mamilioni ya watanzania ambao hawana mtetezi na wote wamekuja nyuma yake waliposikia anasema anapinga kinachoendelea. Badala yake isikilize ushauri anaotoa na kuufanyia kazi.
Kama serikali inasema wazi haitahusika na madhara yoyote yatokanayo na chanjo kwa mtu atakayechanjwa...je, ni nani atawajibika kwa madhara yatakayosababishwa na chanjo? Ni nani atamsaidia atakayepata madhara hayo.? Tafakari.
Kama serikali haitaki kubeba lawama, basi tuisaidie kwa kugoma kupokea chanjo. Kunipa chakula halafu ukasema kikinidhuru usiulizwe... maana yake lazima hicho chakula kitaleta madhara na hutaki kuwajibika kwa madhara hayo!!
Naomba watanzania kwa pamoja tusikubali kuwa sehemu ya majaribio. Hata mtu akiamua kuchanja mbele ya TV hiyo haitoshi kutuaminisha maana anaweza kuchanja kitu kingine chochote ambacho sio chanjo ya UVIKO-19 anayotaka wengine wachanjwe.
KATAA CHANJO NA KWA PAMOJA TUSIMAME NA ASKOFU GWAJIMA.
CHANJO NI HATARI!!!!!!