#COVID19 Tumsikilize mchungaji Gwajima, tusimbeze. Chanjo zote zina bechi tofauti na kuna nchi hukataa baadhi ya bechi na nyingine ni zile zilizobakia

Richard, I hope that's your name, wewe ni mtu wa siku nyingi humu, ongea kama veteran wa JF. Simply put ulichoandika hapa juu does not make any sense. Unavyojibu nakuwa na wasi wasi na uwezo wako kwani huna tofauti na viwavi vilivyosukumizwa humu na status quo kutetea kila tendo la watawala wetu.
 
elimu yako kwanza mkuu ,tuijue,maana tunaweza tukawa tunabishana humu kumbe hata fani ya medicine huijui,kumbe wewe ni makenika.
 
1. Ukipata chanjo unaweza kupata corona? = Ndiyo

2. Ukipata chanjo unaweza pia kufa kwa corona? = Ndiyo

SWALI:
Kwanini upate chanjo?
Na Kama yote hayo jibu ni ndiyo,Sasa hiyo inayosisitizwa watu wachanje ni NINI!? NA NI KWA NINI!???

Hii kitu inachanganya na kuacha maswali mengi kwa watu,serikali pia haina majibu ,wazungu pia hawana majibu.sijui nini kinaendelea kwenye hii dunia!!!!
 
Hata kama wanao muona.. Radio mbovu lkn wajue anasema kweli..
Your browser is not able to display this video.
 
Wazifahamu gharama za kurusha Drone na kuiweka angani?
 
Seriously Gwajima?? Kwanini usitumie paper ya kitaaluma?? Yaani Gwajima ndio mchambuzi wa kitaaluma mpaka mseme hoja yake ipo hapo? Anajua nini kuhusu DNA au mRNA
Msikilizeni.

Kuna mambo yamo ndani ya yale anayoyaongea.
 
Wanajua lugha ya kibeberu tusaidieni hii forum inasema?

View attachment 1872412
Hiyo ni fomu ya ruhusa/hiari kwa mchomwaji sindano mtarajiwa na mhudumu wa afya na mchomaji sindano.

Wakubali kuchomwa sindano ya chanjo lakini serikali haitahusika/ haitawajibika kwa lolote litakalokutokea baada ya kuchomwa sindano hiyo.
 
Pasco hapo nadhani ni swala la kofia.Amepinga chanjo kwenye madhabahu ya kanisa katika nafasi ya uaskofu wake na sio kama Mbunge.....
sidhani kama kuna ukinzani wa kauli zake kanisani kama askofu dhidi ya Mwenyekiti wake wa chama....
laiti angechalenge kwenye ulingo wa kisiasa hapo pangekuwa na shida/usaliti
 
Madactari wa tanzania bwana ukiwauliza wamefanya utafiti gani ili kupata dawa ya corona hata miti shamba hangaikeni huko wasomi ninyi
 
Kaka, I'm humbled.

Naona naanza kujikita kuandika maana ninapata nguvu.

Mchungaji Gwajima anatoa maoni tumsikilize.

Cha msingi ni kwamba amesema na amefafanua kuwa raisi Samia ametanabaisha kuwa hizi chanjo ni hiyari na hajashurutisha watanzania wende kudungwa.

Tumsikilize pia kesho.

Umefika wakati sasa hata CCM wenyewe wakubali tu kuwa wapo watanzania ambao wapo tayari kusema ukweli na tuachane na haya masuala ya vitisho na hata kuwakolimba hawa watu.

Hizi ni zama zingine kabisa tuwe tayari na tuweke mazingiza ya utayari kwa watu wa aina ya mchungaji Gwajima.

Wapo wengi ila kwa sasa wameingiwa woga.

Mchungaji anawapa ari mpya na nguvu mpya.

Kwa kiingereza twasema,"It about power of reasoning"

Ni maoni yangu tu.
 
Umesema vyema mtaalamu, ni matumaini yangu hufungamani na chama chochote cha siasa, kinyume na hivyo, usingeweza kufikiria hata moja ya hoja ulizoainisha hapo.
Huyo atakuwa MATAGA, anajaribu kulinda legacy kwa angle ya taaluma
 
Sijamtetea mtu yoyote nimeshauri tu kuwa Mchungaji asikilizwe.

Mbona inakuwa taabu sana kuelewa hii?
 

Unaposema amesema "watu wote wasichanjwe" maana yake ametoa amri...

Lakini ukweli ni kuwa, amesema "watu watumie hiari ya kuchagua kwa kuchagua kutochanjwa"

Yeye anatumia ushawishi wake kuwashawishi watu kuchagua salama (kwa kadiri anavyoona yeye) badala ya hatari...

Kama ni kuhukumiwa, muhukumuni Rev. Bishop Josephat Gwajima kwa kushawishi watu kukataa chanjo...

Na kwa upande wa serikali (kama inaamini iko sahihi),kama njia ya kuwadhibiti watu aina ya Gwajima, basi igeuze hiari hii iwe AMRI YA LAZIMA kama inaweza...
 
Umeandika sana but hayo yote ni mawazo ya Kichawi.

Kwanza siyo bech ni Batch.

Hakuna mechanism ya ujinga kihivyo.

Ulaya wameoa na kuolewa Africa.
Huwezi kufikiri kwamba batch fulani watachomwa nani na nani hawatachomwa.

Mzalishaji yeyote atafuata taratibu zote zinazostahili.

Hujawahi kujua kwamba Tanzania tuna Mabigwa wa Virology mahiri kwa kiasi gani.

Gwajima is the Jack of all trades..

Hajui medicines na hatakaa ajue kwa sababu hataki kujifunza.

Tanzania ina wasomi wazuri wacha kabisa.

Tuna Machine za kisasa we acha kabisa.

Conspiracy ya Medicine ipo na zitaendelea kuwepo lakini siyo kwenye hali ya taharuki kama sasa.

Ziko Njia milioni kidogo.

Pandemic inatishia Usalama wa kila kiumbe hapa Duniani, plan ni kupambana nayo iondoke.
 
Wacha upumbavu.

Bechi ni kiswahili sanifu na Batch ni kiingereza.

Bechi - kundi

Batch -group, flock, category, gang, batch

Kisha jikite kwenye mada.
 
1. Ukipata chanjo unaweza kupata corona? = Ndiyo

2. Ukipata chanjo unaweza pia kufa kwa corona? = Ndiyo

SWALI:
Kwanini upate chanjo?

Maswali ya kitoto! Mtu mzima haishii kuangalia hayo tu!! Kwa makusudi hujasema ambaye hajachanjwa anaweza kupata corona na anaweza pia kufa!!

Twende mbali zaidi - je ni wangapi kati ya wangapi waliochanjwa wanapata covid na hta kufikia tu kuumwa, achilia mbali kufa!

Kwa taarifa yako - hata ulipochanjwa polio. Walikusudia ikikupata isikuathiri - sio isikupate kabisa!!!
 
Mbona kwenye chanjo ya surua au polio mbona hizo side effects hazikutokea mpaka sasa; kwani chanjo ya corona?
 

Richard, soma kidogo changamoto zilizoandama juhudi za kupambana na gonjwa lililowafyeka binadamu zaidi ya 300,000,000 miaka zaidi ya100 iliyopita. Gonjwa hilo lilijulikana kama small pox.

Katika juhudi za kulitokomeza, soma changamoto ambazo juhudi hizo zilipitia hadi dawa ya kwanza kabisa ya chanjo kupatikana na ilipatikanaje. Soma upinzani mkali ulioandama matumizi ya chanjo hiyo.

Soma jinsi mtu moja alivyofungua kesi hadi makama kuu nchini Marekani (Supreme Court) kupinga chanjo hiyo na soma maamuzi ya mahakama hiyo na hatua zilizochukuliwa kuhakikisha chanjo inatolewa.

Soma wahubiri na manabii uongo walivyohusisha chanjo hiyo na mafundisho ya dini kama anavyofanya Gwajima hadi nguvu kutumika kwa kupita nyumba hadi nyumba kutoa chanjo hiyo kwa nguvu.

Watu wenye uelewa mdogo na wasiojua historia wanafikiri hii ni chanjo ya kwanza kupata upinzani mkali wa chanjo na wanatumia ujinga wao kupinga hii chanjo kwa sababu kama hizo hizo za karne zilizopita.

Hebu pitia hapa kidogo... Upinzani dhi ya chanjo ya small pox vaccine supreme-court-smallpox-covid/
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…