Tuna Imani na CHADEMA hii, wala si nyingine

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Tunahitaji kuwa na uhakika ili kuweza kujipanga kwa hatua zetu za baadaye, iwe ni kusuka au kunyoa nywele zetu. Tunayo imani na CHADEMA ambayo ina misimamo ifuatayo:

1. Kipaumbele chao ni kupatikana kwa Katiba mpya.
2. Hawatakuwepo uchaguzi mkuu wa mwaka 2024/25 bila Katiba mpya.

Baada ya sherehe na matukio muhimu ya uzinduzi wa mikutano ya kisiasa na mapokezi ya wenzetu waliokuwa uhamishoni, tunatarajia sasa kama chama, tunajiandaa kwa kazi rasmi.

Tunatambua kuwa safari yetu haitakuwa rahisi. Tutakutana na changamoto nyingi na uchungu, lakini tunaamini tutashinda.

Tunapenda kupata taarifa kuhusu mpango wa hatua za kupata Katiba mpya. Tungependa kujua wazo lililopo akilini mwa viongozi wetu ili tuweze kuchangia na kujiridhisha.

Pia, ingekuwa vyema sana kumtambulisha mkuu wa mikakati ya chama kuelekea Katiba mpya.

Tunamuomba Mungu abariki CHADEMA.
 
Yes, sure, Action plan!
 
Kwahiyo Dr Miguna Miguna ndiye atakayeleta Katiba Mpya?



Lema alisikia kutoka kwake jambo la msingi moja tu:

"Hatutaweza kubadilisha lolote kama wito wa kudai katiba mpya hautakuwa kipaumbele."

Alichokisikia Lema ndicho sisi tunachokijua kama msimamo wa CHADEMA tunayoijua sisi.

Zingatia hakuna katiba mpya hakuna uchaguzi mkuu.

Magereza hayatoshi. Kama vipi simamisheni mradi wa umeme mwalimu Nyerere mjikite sasa kwenye kujenga magereza.
 
Inabidi wapambane kweli, na waonekane wana nia hiyo, kwa sababu mazingira ya kisiasa wanayopitia yanaweza kuwafanya wajisahau, au kuzubaishwa na mtawala.
 
Hii ndio imani yangu. Kama tuli afford kukosa viongozi woote 2020 sijui kama tutashindwa sasa.
 
Inabidi wapambane kweli, na waonekane wana nia hiyo, kwa sababu mazingira ya kisiasa wanayopitia yanaweza kuwafanya wajisahau, au kuzubaishwa na mtawala.

Bila kuweka tashwishi niombe kufanya maboresho haya:

"Inabidi tupambane kweli, tuonekane tuna nia hiyo ....."
 
Wiki mbili alizoahidi Lissu kuwa amerudia hazijafuka tu?
 
Hii mbinu ya safari hii niliisubiri siku nyingi hatimaye imenikuta hai.
 
Cdm ya Mbowe imeshindwa kusimamia hayo kwa vitendo.
Imeamua kuungana na ccm ili kuvuna mapesa ya Abdul na ndio maana inakataliwa na wenye akili.
Lisu pekee atakiokoa hiki chama na kukirudisha kwenye agenda zake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…