Tunajikumbusha kidogo tu ili kuweka kumbukumbu sawa


👉🏾Ukiacha ile Yanga ya kampa kampa tena Yanga (2016) kuna ile Yanga ya 2014 yanga ya kina Cannavaro Didi, Yondani, Ngassa, Msuva, Okwi, Chuji, kiiza, Domayo , Twite Joshua, Bahanuzi kavumbagu na wengine.

👉🏾Ambayo kwenye vikosi bora Ambavyo klabu ya Yanga imewahi kuwa navyo pale jangwani basi kikosi hicho cha 2014 kilikuwepo.

👉🏾1march 2014 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza (first round leg) ya ligi ya mabingwa barani Afrika Yanga alicheza na Al Ahly katika uwanja wa Benjamin mkapa (Zamani taifa) na Yanga ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao moja kwa sifuri bao la dakika ya 83 lilofungwa na beki Nadir Haroub "Cannavaro " akimalizia kazi nzuri ya mpira wa kona wa Simon Msava.

👉🏾Mchezo wa pili ukapigwa Misiri tarehe 9March 2014 ambapo yanga walikuwa na kiwango Bora sana Al Ahly wakisubiri mpaka dakika ya 71 kipindi cha pili ndio wakarudi mchezoni kwa bao Sayed Moawad na mchezo kumalizika kwa sare ya jumla ya kufungana bao moja kwa moja kwenye (aggregate ).

👉🏾Kwenye Changamoto ya mikwaju ya penalti Al Ahly akashinda kwa mikwaju ya penalti 4 kwa 3 . japo haikuwa rahisi kwenye mikwaju ya penalti Dida aliokoa penalti (2) penalti ya 4 na 5 ya Al Ahly zote aliokoa. huku kwa Yanga Oscar Joshua na Said Bahanuzi wakikosa penalti ya 4 na 5 . Kisha katika penalti moja moja Mbuyu Twite akakosa penalti yake . na Yanga kutolewa.

👉🏾Hapo Al Ahly ndio alikuwa bingwa mtetezi wa michuano hiyo alichukua (2013) Hivyo Yanga aliondolewa katika mashindano hayo na Bingwa mtetezi. japo ilikuwa katika hatua ya awali ya michuano hiyo lakini watu walisema "Yanga amekufa kiume"

👉🏾kwenye moja ya michezo ya kimataifa ambayo ipo katika kumbukumbu za mashabiki wa Yanga basi ni mchezo huo kwa sababu ya wengi kuamini yanga walikuwa bora sana . na wengine waliamini kama sio uzembe wa wapiga penalti Basi Yanga wangesoma mbele.

👉🏾 Nafikiri hii ni kama ilitokea jana kwa Simba tofauti yake Yanga ilikuwa katika hatua ya awali ya ligi ya mabingwa Simba katika hatua ya Robo fainali ya ligi ya mabingwa.
 
Mwamba Bujibuji Simba Nyamaume nakukubali.
Ila suala la BANDARI yetu bado liko palepale
Kama kumbukumbu zangu zipo vizuri hawa DPW ni kampuni ya waarabu walewale au wenye nasaba na wale waliohusika na kwenye kashfa ya Loliondo Gate,ambayo inanikumbusha marehemu Stan Katabalo rip mwandishi nguli miaka hiyo.
Hawa jamaa walikuwa wakivuna wanyama wetu kwa silaha za kivita badala ya zile za kuwindia.Jinsi wanavyoweza kuwaweka viongozi wetu mifukoni mwao. Na hakuna hatua yoyote iliwahi chukuliwa dhidi ya hao jamaa juu ya uhalifu wote waliokuwa wakiufanya.(Maana hayo ndiyo yaliyokuwa yakiletwa kwetu wananchi na magazeti yetu ya zama hizo).

Jamaa hawa walisafirisha wanyama wetu hai kwenda kwao huko Imarati ambako waliaanzisha mbuga ya wanyama kwa kutumia hao wanyama wetu.Kitu ambacho kina athari hasi tena ya kudumu kwenye uchumi wetu.

Sasa kama wananchi wameyaona na kuyasikia hayo , na wengine wakiuishi ukweli mchungu wa uwepo wa hao jamaa nchini mwetu huko umasaini. Kwanini mtake tu kulazimisha watu wa kutoka nchi hiyohiyo tena ikiaminika wanatoka familia ileile kuja nchini kwa namna inavyofanywa na kukabidhiwa bandari zetu kwa jina la “Serikali haifanyi biashara”?

Nina mengi ya kuandika kuhusu hii nchi yetu na uongozi wake. Ni aibu kubwa kutumia madaraka na nguvu kubaka watu, kubaka utashi wao, kuwalazimisha na kuwatumbukiza kwenye vitu vya hovyohovyo eti tu kwasababu hakuna anayeweza kuwafanya chochote (nga kwa sasa). Inaweza kuja siku huko mbele ya safari maamuzi ya kitemi(mimi nayaita ya kiduanzi na ushamba tu) yakasababisha kilio na kusaga meno hapahapa chini ya jua.Ipo siku inakuja.

Watu wenye weledi wakihoji na kutoa taarifa za namna mambo yanatakiwa kuwa, inatumika nguvu kubwa kuwanyamazisha na mara nyingine hadi kuwadhuru. Yaani wahuni fulani wachache wanatuingiza mkenge na hatupaswi kuhoji , lakini madhara na hasara ni zetu wote. Hii ni kali.

Wengine tuna kumbukumbu ya mambo mengi yaliyowahi kufanyika huko miaka ya nyuma, narratives wanazotembelea ni hizihizi , za kujifanya wameona kitu kinachoweza tufaidisha kama nchi ilhali ni matumizi mabaya ya madaraka kuingiza upigaji ambao ukiuangalia vizuri kwa undani unakuta wana maslahi nao upigaji huo ya moja kwa moja . This isn’t fair at all na ni dhambi mbele za Mungu na mbele ya wananchi wenye mali yao.

#herimimisijasema
 
Kumbukumbu na Picha.

Pichani ni Jamshid bin Abdullah Al Said, GCMG, Sultani wa mwisho wa Zanzibar, akiwa uhamishoni na mkewe Sheikha Anisa binti Salim Al Said na watoto wao katika Hoteli ya St James, Jijini London, Uingereza. Hii ni mnamo Januari 21, 1964

Sultani Jamshid bin Abdullah alalizimika kuikimbia Zanzibar usiku wa kuamkia Januari 12, 1964 mara baada ya vijana wa Chama cha Umma Party wakishirikiana na vijana Chama cha ASP na wakaazi wengine wa Unguja kuanzisha taharuki na vurugu ambazo baadae zilipelekea Mapinduzi yaliyoingusha serikali ya Waziri Mkuu Muhammad Shamte Hamadi.

Jamshid bin Abdullah alizaliwa mnamo Septemba 16, 1929 katika visiwa vya Unguja, Zanzibar na alitwaa madaraka kama Sultani na baadae Mkuu wa nchi ya Zanzibar mnamo Julai 1, 1963 baada ya kifo cha baba yake Sultani Abdullah bin Khalifa Al-Said, KBE, CMG.

Sultani Jamshid aliitawala Zanzibar wakati bado ikiwa koloni la Uingereza na hata baada ya Uingereza kuipatia Zanzibar uhuru wake mnamo Desemba 10, 1963 aliendelea kuitawala kupitia serikali ya Waziri Mkuu Muhammad Shamte hadi Januari 12, 1964 alipolazimika kuikimbia Zanzibar kutokana na taharuki, vurugu na baadae Mapinduzi ya serikali na dola.

Zanzibar ina historia tamu, chungu na nzito sana. Kwa hakika kuisema inaitaji ujasiri kidogo, Inshallah hivi karibuni tutaanza kuingazia historia hii yenye pingili pingili nyingi za sumu na vidonda vyenye damu.

 
KUMBUKUMBU Oktoba 21,1980 alizaliwa mwanamuziki ambaye ni mmoja wa waasisi wa bongo fleva, Juma Kasim 'Nature'.
Mtakie heri hapa chini alafu tuambie unaburudika na ngoma gani kutoka kwake.
 
Kumbe simba walianza kufungwa tangu zamani masikini....
 
Hawa tukiwakamata tuwapeleke kwa Mparange
 
Sijafika kitambo huku,hapo Pana mwendokasi kumbe
 
Tukuyu tawi la simba
 
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan wakati huo kwenye Jubilee ya miaka hamsini Ihungo high school, inaelezwa hapa alimuwakilisha Waziri wa Elimu mwaka 1997, kushoto Kwa Rais Samia ni Mzee Rutanjuka (RIP) alikuwa ndiye Mkuu wa Shule, nyuma (Mwenye suti nyeusi) ni Mkuu wa Mkoa Kiwelu ( wakati huo.)

Ihungo High School ipo Bukoba Mjini, kama una kumbukumbu iliharibiwa na Tetemeko, wakati wa Rais Magufuli ilikarabatiwa na Sasa Ina majengo ya kisasa . Ilianzishwa mwaka 1947 zamani ikijulikana kama St. Thomas Collage.

NB: Suti za Hawa waheshimiwa zinachekesha sana, kiasi akiiona @idrissultan anaweza kucheka Kwa nguvu, akajikuta Sentro! Unakumbuka Ile kesi ya Idris , aliye mcheka Mheshimiwa Magufuli akakamatwa Kwa kucheka suti?!. Don't try this at home, school or anywhere. 😂😂😂
 
THE UNTOLD STORY OF HOW AND WHY FELA KUTI MARRIED 27 WOMEN ON THE SAME DAY IN 1978 (A must read)

In 1978, the pioneer of Afrobeats, Fela Anikulapo Kuti, married 27 women in one day. This should not be strange to those who know the life and style of the Nigerian music legend nicknamed Abami Eda (strange creature).

Many of Fela’s band members became homeless after the devastating soldier attack on Fela’s commune (Kalakuta Republic) in 1977. In order to keep them together, Fela decided to do the unusual.

He gave a piece of paper to his female band members requesting the names of those that would like to marry him; the entire twenty-seven female band members put down their names.

After getting their consent, Fela Kuti married the 27 women on the 20th of February, 1978, at the Parisona Hotel in Anthony, Lagos, with the blessings of twelve Ifa priests. It was alleged that some parents of the ladies objected the marriage.

Fela married the women to protect and keep them together. The marriage ceremony was attended by Fela’s families, friends and other band members.

During the marriage ceremony, Fela rendered a short speech, pressed naira notes on his new wives’ foreheads and gave them marriage certificates. Fela embraced a rotation system of 12 wives at a time. After the marriage, Fela took his 27 wives to Ghana for honeymoon.

However, in 1986, shortly after his release from prison, Fela Kuti divorced his 27 wives on the claim that marriage brings jealousy. It should be noted that they were not forced to leave his house after the divorce; some lived with him till his death in 1997.

Source: NIGERIA STORIES
 
Your browser is not able to display this video.

Gwajima kanunua train kwa cash, tangu mwaka 2016 liko njiani linakuja mdogo mdogo
 
Your browser is not able to display this video.

Chris Turker playing as Smokey on the movie Friday
 
Your browser is not able to display this video.

Pamba ya Mwanza ilikuwa tishio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…