Poleni sana Dada zetu. Na pole kwa vikwazo mnavyovipata kutoka kwa Wanaume. Tunawapenda ndo maana tunawasema pale mnapokosea. Mimi rafiki yangu namshauri kile ninachoona kinafaa akikataa naachane naye. Akinisikiliza namheshimu sana na kumthamini. Mawigi na vipodozi hamnogi ila pia si vizuri kiafya, twende wote Taratibu mtaelewa.
Achaneni na Mawazo eti tunakataa kwa kuogopa gharama za kugharamia Mavijimekapu vyenu, sio kweli. Ukweli ni tunawaonea huruma mnavyojiharibu na kuondoa muonekano wenu mzuri. Lakini pia pamoja na madhara ni Uharibifu wa fedha.
Nakuhakikishieni kwamba, Wanaume wanaokukataza Vipodozi anakupenda na anakuonea huruma. Siku zote hata mzazi anapenda kuwakataza Watoto wao tabia mbaya. Nakuhakikishieni, Mwanaume au mwanamke ambaye hana muda na wewe au ambaye hakuthamini, hawezi kukukataza mabaya. Mwanaume anayekushauri mema Usimchukie japo ukweli unauma. Mpende, si wote wenye moyo wa kukukosoa pale unapokosea, wanasema ngoja likome..na akikuona anakusifia.
Mfano kucha bandia zinaharibu kucha zako hadi zinaanza kung'oka. Zzinaleta magonjwa.
Kuhusu Vipodozi, Vingi vimekatazwa na vina madhara, halafu vinaondoa muonekano wa mwanamke. Wengi wanatumia vipodozi kuficha ubaya wao wa sura na wengine wanapaka kwa kuiga wafanane na fulani.
Tatizo kubwa la vipodozi vingi leo kwa afya ya wasichana linakuja pale msichana atakapotumia vipodozi vyenye viambato vyenye sumu na dawa vinavyochubua ngozi na kuharibu rangi ya asili ya ngozi, kucha na nywele. Na hali hii husababisha madhara ya kiafya mapema sana au baadaye sana. Vipodozi vingi vya leo wanavyotumia wasichana vimechanganywa na sumu ya ‘hydroquinone’ pamoja na viambato vya dawa za ngozi na rangi zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.
Wanawake hampendi, sisi tunaopenda ndo tunajua nini tunataka kutoka kwa mwanamke. Nyinyi mnafanya yote hayo ili Mpendwe, mnakuwa mnajaribu labda nikifanya hivi ntapendwa. Kwanza unaonekana limbukeni. Sisi wanaume hatutumi vipodozi lakini tunajua ni vibaya. nyie hamuwezi jua sababu mwapenda na kipendacho roho hula nyama mbichi. Tunawapenda sana na sisi ndo kichwa cha nyumba hivyo tusikilizeni sisi. na kama mna swali uliza. REF:
Wadhamini kidogo
Ukweli ni kwamba hamjui umuhimu wenu. Mfano mimi napenda kulambalamba mwili mzima. Nikilamba hivyo vidude mnavyojipaka si ntatapika?
Vipodozi vingi huathiri ubora wa afya ya ngozi na kusababisha ngozi kuwa na mabakamabaka, ngozi kukunjamana na kupoteza hali yake ya kuvutia. Ngozi pia huwa nyembamba sana na kulainika kuliko kawaida. Hali hii husababisha ngozi kuchanika kwa urahisi na kushoneka kwa shida pale mtumiaji anapopata jeraha kubwa linalohitaji matibabu ya kushona. Ngozi iliyolainishwa sana kwa kemikali huzeeka haraka na kukunjamana baada ya miaka michache ya kutumia vipodozi vyenye kemikali hizo.
Vipodozi vingi pia huleta weupe bandia wa mwili kwa kuondosha dawa ya melanin inayofanya ngozi ya mwafrika kuwa nyeusi ambayo kimsingi humsaidia kukabiliana na mionzi ya jua. Ngozi isiyokuwa na melanin ya kutosha huathiriwa na mionzi ya jua kwa urahisi na kuongeza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani (kansa) ya ngozi kwa urahisi.
Matumizi ya vipodozi hivi hatari pia yanaweza kusababisha kansa ya damu, kansa ya mapafu, kansa ya ini, kansa ya ubongo na uvimbe ndani ya pua (nasal polyps). Madhara mengine ya vipodozi visivyofaa ni pamoja na kupata chunusi kubwa, kupata ugonjwa wa mzio wa ngozi (allergy) na mwili kuwasha mara kwa mara. Vipodozi vyenye harufu kali pia vinaweza kusababisha ugonjwa wa pumu na kikohozi kwa mtumiaji au kwa watoto wadogo hasa wale wanaonyonya.
Pafyumu nyingi zina viambato vya manukato bandia yatokanayo na kemikali zinazodhuru afya ya neva, na wakati mwingine husababisha matatizo katika mfumo wa damu, na kuharibu utaratibu mzuri wa msukumo wa damu pamoja na kusababisha maumivu ya kichwa na kizunguzungu.
Vipodozi vyenye viambato vya dawa vikitumiwa kwa muda mrefu zaidi ya majuma mawili vinaweza kusababisha hali ya kukosekana kwa ulinganifu na usawaziko wa vichocheo vya ujinsia katika mwili wa msichana. Hali hii husababisha baadhi ya wasichana kuwa na misitari au milia ya ngozi katika baadhi ya sehemu za mwili pamoja na dalili au tabia za kiume kama vile kuota ndevu, kunenepa kwa kisanduku cha sauti (Adam’s apple) na kuwa na sauti nene yenye mikwaruzo au besi.
Mabadiliko mengine huusisha kunenepa kwa kinembe (clitoromegaly) na mabadiliko katika upataji wa damu ya hedhi. Msichana anaweza kupata damu ya hedhi kidogo, anaweza asiione kabisa au damu inaweza kutoka bila mpangilio maalumu, jambo hili linaweza kusababisha mahangaiko ya kihisia kwa msichana, na wasichana wengi huenda kuonana na madaktari mara kwa mara kutokana na athari hizi za vipodozi.
Mamlaka ya chakula na dawa Tanzania [TFDA], wenye dhamana ya kisheria ya kulinda afya ya watumiaji wa dawa, vipodozi na vyakula katika taifa la Tanzania, wamepiga marufuku matumizi ya cream, jeli, mafuta ya kujipaka, sabuni na lotion zenye kiambato cha Hydroquinone. Pia sabuni na cream zenye zebaki na homoni ya steroid zimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu nchiniTanzania, [kwa taarifa zaidi tembelea katika tovuti ya TFDA,
www.tfda.or.tz].
Viambato vingine ndani ya vipodozi vinavyodhuru afya ni pamoja na Petrolatum (mineral oil), Phthalates (DMP). 1, 4 dioxane /Polyethylene Glycol(PEG), Triethanolamine (TEA) na Parabens.Viambato hivi vinaweza kusababisha athari katika mfumo wa uzazi na kupunguza uwezo wa kutunga mimba, ugonjwa wa ini na figo na kupungua kwa uwezo wa kufikiri pamoja na ubunifu.
Athari za vipodozi hivi pia ni pamoja na kupunguza uwezo wa akili katika kujifunza mambo. Tatizo jingine ni urahibu na tamaa ya kutaka kuendelea kutumia na kupoteza uwezo wa kujidhibiti dhidi ya vipodozi hatari. Akili ya mtumiaji wa vipodozi hasa vile vinavyochubua ngozi na kuleta weupe bandia huzoea hali ya kudanganywa kuwa weupe ndio uzuri na urembo kiasi kwamba haikubaliani kwa urahisi tena na muonekano wa asili.
Kukosa au kuacha matumizi ya vipodozi hivi, husababisha msongo wa mawazo na msichana hupata hisia kuwa ngozi nyeusi siyo ya kuvutia hasa kwa wanaume au wavulana. Kwa wasichana hawa ngozi nyeusi ya asili husababisha huzuni na ngozi yenye weupe wa bandia ndiyo inayoleta furaha maishani mwao bila kujali hatari za kiafya.
Ngozi nyeusi kwao humaanisha kukosa mafanikio maishani, na hili huwafanya kuwa wabaguzi wa rangi na kuaibishwa na asili yao kama watu weusi. Huu ni mwendelezo wa dhana ya ubaguzi wa rangi uliokomaa katika mfumo wa kisayansi.
Msichana mmoja mwenye asili ya Afrika anayeishi Uingereza, aliwahi kusema kuwa anachukia kuwa mtu mweusi, anatamani kama angeweza kuondoa damu yote mwilini mwake na kuimwaga pamoja na kuchuna ngozi yake nyeusi yote ili awe mweupe. (
I hate being a black girl; I wish I could drain all the black blood out and rip the black skin off me | imirasire.com).
Huu ni ushahidi tosha kuwa wasichana wanaojichubua kwa vipodozi hatari ni waathirika kiasikolojia. Lakini hii pia inaweza kutafasiriwa kama athari ya biashara ya utumwa na utawala wa kikoloni.
Mimi Mke wangu, Mpenzi wangu atajipodoa tena sana tu, ila ahakikishe haondoi muonekano wake. Mfano mimi sipendi kucha ndefu kwani nachukulia kama uchafu. Ukiwa una kucha ndefu ukatoka chooni zinarudi na kuchafu au bakteria. Napenda kucha fupi au ndefu ziwe zake na zisizidi sana. Ukiwa na kucha ndefu wewe sio wangu na hiyo ni sababu tosha ya kuleta mgogogoro. Uzuri Mungu ananisaidia nimpendaye anaelewa nataka nini hivyo sichoki kumuangalia.
Ndo maana wanaume wengi wanachelewa kurudi Majumbani sababu anaogopa kumuona mke wake alivyojiharibu.
Kwanini uhatarishe mahusiano yako kisa una hela ya kufanya Utakacho? Ukibadilishwa na hela jua una wazimu
Wahenga walisema "PATA FEDHA TUJUE TABIA ZAKO"
Nachukia, sipendi na sitaki kusikia hayo madude yenu sijui Miwigi na mikucha kama mwewe, Unapaka mirangi mdomoni utafikiri umetoka kula nyama ya mtu. Hadi kinyaa. Alaaniwe aliyeleta hayo madude. Kwanza Mawigi yananuka kama gari la taka.. na usiombe anyeshewe na mvua. Wanawake wanaovaa mawigi ukitaka ujue wanavyojua kutimua mbio, yaje manyunyu ya mvua. Unaweza kuwa na hela lakini lazima avae mfuko wa shangazi. Tabu za nini? Manyunyu tu makeup yote kwisha. Nami kabla ya kusalimiana Kitandani kaoge kwanza.
Ngoja niishie hapa nisisimangwe bure na nikanunuwa wiki nzima hata like za jukwa la picha nisipate.
Mkinisoma Vizuri ntakuwa nimewaongezea kitu, Dah.. Anyway..ya Kaisali mwachie kaisali. MIA