Tunamhitaji Mbowe, Zitto, Lipumba na wapinzani wengine wote kusimama imara kwa umoja kuna mambo hayaendi sawa nchi hii

Tunamhitaji Mbowe, Zitto, Lipumba na wapinzani wengine wote kusimama imara kwa umoja kuna mambo hayaendi sawa nchi hii

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Sisi ndio tutakaoteseka kama mambo yataendelea kama yanavyoendelea sasa hapa nchini. Kwa kweli tumerudi nyuma mno kwenye masuala ya uongozi na usimamizi wa utendaji wa watumishi wa serikali na rasilimali zetu.

Huu ndio wakati muafaka sana kwa viongozi wa upinzani kuungana na kuwa sauti moja kusaidia kuwaunganisha watanzania kuinusuru nchi yao.

Kama mambo yataendelea hivi tutaishia pabaya muda si muda. Viongozi wasifurahie kuona wanachi wamekaa kimya tu, hakuna kitu kibaya kama mtu akaaye kimya baada ya kudhulumiwa.

Watanzania tunahitaji kufanya kitu hata kama ni kuonesha kutoridhishwa kwetu kwa kuandika ama kwa jinsi yoyote kwani sisi ndio tutakaoteseka na hali hii inayozidi kuwa mbaya.

Mungu inusuru nchi yetu na watawala wasiojali hali za wananchi na kuangalia maslahi yao tu.
 
Upinzani uliosimama ulikuwa ulikuwa wa Dr. Slaa Tu.

Wengine matumbo yao festi
 
Simameni wenyewe, kwani lazima mwasubirie wakina Lissu, Mbowe, Lipumba na Zitto.
 
Simameni wenyewe hata Mbowe, Zitto na Lipumba wana familia zao zinawategemea na kuwapenda. Wakiwaita kwenye mahandamano ya amani unatia mikia matakoni.
 
Upinzani uliosimama ulikuwa ulikuwa wa Dr. Slaa Tu.

Wengine matumbo yao festi
Haya yanayoendelea bora yaendelee tu watu wote waungane kudai uhuru wa pili kutoka kwa mkoloni mweusi. Huwezi kufanya upinzani bila support ya wananchi. We don't support the opposition basi ngoja tuvune matunda ya upuuzi wetu.
 
Chadema mlitutenga enzi zile, leo yamewakalia kooni ndio mnatuita, hatutaki
 
Sisi ndio tutakaoteseka kama mambo yataendelea kama yanavyoendelea sasa hapa nchini. Kwa kweli tumerudi nyuma mno kwenye masuala ya uongozi na usimamizi wa utendaji wa watumishi wa serikali na rasilimali zetu.

Huu ndio wakati muafaka sana kwa viongozi wa upinzani kuungana na kuwa sauti moja kusaidia kuwaunganisha watanzania kuinusuru nchi yao.

Kama mambo yataendelea hivi tutaishia pabaya muda si muda. Viongozi wasifurahie kuona wanachi wamekaa kimya tu, hakuna kitu kibaya kama mtu akaaye kimya baada ya kudhulumiwa.

Watanzania tunahitaji kufanya kitu hata kama ni kuonesha kutoridhishwa kwetu kwa kuandika ama kwa jinsi yoyote kwani sisi ndio tutakaoteseka na hali hii inayozidi kuwa mbaya.

Mungu inusuru nchi yetu na watawala wasiojali hali za wananchi na kuangalia maslahi yao tu.
Hao wote ulio wataja kwa sasa hawaaminiki hata chembe wapo hivi sasa kifaida zaidi Lika tutigite.
 
Back
Top Bottom