Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Sasa mkuu si ungeturushia hapa jamvini wazalendo wanzako tuvisikie pia!!!
 
I don't think you can compare Sokoine to Slaa in anyway. Sokoine was more charismatic, more patriotic and more passionate. But this is my own opinion.
 
Thanks.

Kila aliyewahi kumfahamu au kusoma historia vizuri ataungana na wewe kuwa kile kilikuwa kichwa cha Tz na tungekuwa mbali sana angekuwepo. Lakini nakusihi kuwa huo ni mkakati tu wa wale wanaoutamani urais 2015 wameamua kutuwekea hayo ili kutayarisha njia kwa baadhi yao ambao ni kinyume na Sokoine
 
Leo ni kumbukumbu ya miaka 27,toka kifo cha Sokoine,aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tz. Kifo ambacho kilitokana na ajali yenye Utata. Hivi ni kwel yasemwayo kuwa Sokoine aliuliwa ktk ajali ile ya kupangwa ??
 
"Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na Wananchi peke yake.

Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu" - Edward Moringe Sokoine, 26 Machi 1983

Leo hii viongozi wa nchi yetu wanawakumbatia wala rushwa na kuwaita mashujaa.
 
Hizi ni baadhi ya quotes zake. Tutakukumbuka daima Mwennyezi Mungu akulaze mahali pema peponi.

"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asimuulize mwanae, 'mali hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983​

"Katika nchi inayojali haki na usawa, majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya walio wengi. Na kamwe hayaruhusiwi kuwa ni chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao na kusahau maslahi ya walio wengi" - Edward Moringe Sokoine, 1Februari 1977
 
Hi thread imenikumbusha "The Original JF"!

Sijui ni kitu gani kimewasibu hawa wachangiaji?

Anywayz RIP Comrade Edward Moringe Sokoine ...

Mkoa wa Kagera watakukumbuka sana jinsi ulivyoendesha zoezi la kukamata wahujumu uchumi! Kuna sentensi uliyoitoa kupitia redio Tanzania mpaka leo uwa naikumbuka...

".. Na wale mapadri waliokamatwa tutawapeleka kwa Baba Askofu wao..."
 
Heshima mbele kwa wazalendo wa Tz,

Nami kidogo nawiwa niweke hapa machache kuhusu shujaa wa Tz, hayati Edward M. Sokoine.

Ni mtu aliyekuwa amejitoa sana kulitumikia Taifa, kiasi kwamba hata ilikuwa ni vigumu kwake kupumzika au kujivinjari kama hawa vilaza. Hata msafara wake ulikuwa na kawaida ya kuwa na magari machache na hakuwa mpenda anasa.

Nawakumbuka vizuri watoto wake Lazaro, Namelow (mwingine anaitwa Abraham) kwa uchache, walipata elimu ya kawaida pale Arusha na badae Lazaro alikwenda ng'ambo. Pia waliishi maisha ya kawaida sana. Soloine likuwa mjamaa wa imani na vitendo. Mimi si mjamaa wala sipendi ujamaa lakini nina heshimu sana jinsi hayati Sokoine alivyoamini na kuishi falsafa hiyo (kuliko hata Mwl. Nyerere).

Kifo chake kilikuwa na utata, na nadhani mpaka leo ukitazama bado kuna wingu lipo. Ni siri ya wazi kuwa Sokoine kwa tabia, hulka na utendaji kazi wake alikuwa na maadui wengi hasa miongoni mwa viongozi wenzake na hivyo kuipa dhana ya mauaji/ajali ya kupanga kutokuwa ya kupuuza. Alipewa maonyo na waliompenda kuwa macho na mafisadi lakini kwa namna alikuwa charged aliona uhai wake uko katika dhamira yake ya ukombozi wa Tz na hali njema ya wananchi wake.

Ilisemwa miezi mingi kabla ya kifo chake kuwa kulikuwa na msuguano mkali katika kinyang'anyiro cha kumrithi Nyerere. Na marehemu Kawawa alikuwa mshukiwa mkuu wa kifo cha Sokoine. Nionavyo Mwl. Nyerere hakuwa mathubuti (strong and fair) katika kushughulikia mzozo huo ambao pengine ni moja ya chanzo cha u-mauti wa Sokoine. Msuya ni wazi alikuwa mpinzani lakini pia kuna akina Mwakawago na Chiduo nk hawakuwa wema kwake. Na kwa vile alikuwa tishio kwa maslahi ya badhi ya wakubwa wengine....elimination method ushered against him.

Tujiulize leo baada ya kifo chake kwanini Taifa la Tz halikubahatika tena kupata kiongozi wa aina yake katika ngazi ya uwaziri (sio lazima PM)? Sizungumzii kumuenzi maana haiwezekani kwa mazingira ya Tz. Kwa nini Sokoine aliendesha vita peke yake tena ikamgharimu uhai (?). Angekuwa hai Sokoine asingebaki CCM yenye ufisadi kwa muda wote huu ....kwake cheo/madaraka havikuwa muhimu bali dhamira ya alichokiamini. Ikumbukwe aliwahi kujiuzulu uwaziri mara 2, mara moja kwa ajili ya afya na mara nyingine kwenda kuongeza elimu Ujeremani. Mbona hao vilaza leo wagonjwa wa kutupa na vyeo wanavililia>

Mwisho, napinga kwa nguvu zote watu wowote wenye kutaka kutumia kwa namna yoyote jina na/au wasifu wa hayati Sokoine kwa faida za kisiasa. Tena nashangaa ni hivi karibuni tu ndio shujaa huyu ametokea kutajwa tena....najiuliza kwa nini sasa?
 
Sokoine, atakumbukwa Jumanne hii kwa ibada maalumu ya kumwombea kuadhimisha miaka 27 tangu kufariki kwake, Aprili 12, 1984.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, katika siku hii, kumeandaliwa ibada maalumu ya kumwombea Hayati Sokoine katika kanisa alilosali mara ya mwisho kabla ya kifo chake mjini Dodoma.

Lowassa ambaye ni Kiongozi Mkuu wa jamii ya kabila la Kimasai ‘Olaigwanani’ wa Tanzania na Kenya, alibainisha hilo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano wa kimila na viongozi wa jamii ya Kimasai wa Kanda ya Mashariki yenye mikoa ya Pwani, Tanga na Morogoro uliofanyika Kijiji cha Wami Sokoine wilayani Mvomero.

“Aprili 12, siku ya kifo chake kilichotokea kwa ajali ya gari eneo la Wami Ruhindo, Barabara Kuu ya Dodoma – Morogoro…sisi wana Jimbo la Monduli pamoja na Watanzania wenzetu, tumeandaa ibada maalumu mkoani Dodoma itakayofanyika kwenye kanisa alilosali siku ya mwisho kabla ya kupatwa na mauti yake,” alisema.

Alisema kwa vile siku hiyo vikao vya Bunge, vitakuwa vikiendelea, wamepanga ibada maalumu kwa ajili ya Watanzania kumwombea ifanyike katika kanisa ambalo alisali mara ya mwisho mkoani Dodoma.

Aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Mvomero kwa kuandaa mipango mizuri ya kupaendeleza mahali alipofia Sokoine kwa ajali ya gari, Kijiji cha Wami Ruhindo, wakati akitokea bungeni Dodoma kwenda Dar es Salaam.

Pamoja na kuusifu uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Mvomero, Lowassa amewataka wafugaji wa jamii ya Kimasai wanaoishi katika vijiji vya Wami Sokoine, Wami Dakawa na Wami Ruhindo kuanzisha vivutio kwa kujenga mgahawa wa kisasa eneo hilo.

Sokoine aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, alifariki dunia jioni ya Aprili 12, 1984 baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kugongwa na gari lililokuwa likiendeshwa na mkimbizi wa Afrika Kusini katika eneo hilo la Wami Ruhindo na kupoteza maisha papo hapo.
 
me unajua nimeshanga sana mwaka huuuuuuuu, yani naona majabu katika nchi hi ya kisiwa cha amani?am nit sure //???mana naona hataamani haipo sokoine angepata wasa akamka ange waua wote walioanzisha iyo kampeni. then hata familia yake idont know why wametoa maoni ni izalilishaji kataifa mana hata baba wa taifa hakumtambua why?
 
Sokoine, atakumbukwa Jumanne hii kwa ibada maalumu ya kumwombea kuadhimisha miaka 27 tangu kufariki kwake, Aprili 12, 1984.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, katika siku hii, kumeandaliwa ibada maalumu ya kumwombea Hayati Sokoine katika kanisa alilosali mara ya mwisho kabla ya kifo chake mjini Dodoma.

Lowassa ambaye ni Kiongozi Mkuu wa jamii ya kabila la Kimasai ‘Olaigwanani' wa Tanzania na Kenya, alibainisha hilo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano wa kimila na viongozi wa jamii ya Kimasai wa Kanda ya Mashariki yenye mikoa ya Pwani, Tanga na Morogoro uliofanyika Kijiji cha Wami Sokoine wilayani Mvomero.

"Aprili 12, siku ya kifo chake kilichotokea kwa ajali ya gari eneo la Wami Ruhindo, Barabara Kuu ya Dodoma – Morogoro…sisi wana Jimbo la Monduli pamoja na Watanzania wenzetu, tumeandaa ibada maalumu mkoani Dodoma itakayofanyika kwenye kanisa alilosali siku ya mwisho kabla ya kupatwa na mauti yake," alisema.

Alisema kwa vile siku hiyo vikao vya Bunge, vitakuwa vikiendelea, wamepanga ibada maalumu kwa ajili ya Watanzania kumwombea ifanyike katika kanisa ambalo alisali mara ya mwisho mkoani Dodoma.

Aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Mvomero kwa kuandaa mipango mizuri ya kupaendeleza mahali alipofia Sokoine kwa ajali ya gari, Kijiji cha Wami Ruhindo, wakati akitokea bungeni Dodoma kwenda Dar es Salaam.

Pamoja na kuusifu uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Mvomero, Lowassa amewataka wafugaji wa jamii ya Kimasai wanaoishi katika vijiji vya Wami Sokoine, Wami Dakawa na Wami Ruhindo kuanzisha vivutio kwa kujenga mgahawa wa kisasa eneo hilo.

Sokoine aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, alifariki dunia jioni ya Aprili 12, 1984 baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kugongwa na gari lililokuwa likiendeshwa na mkimbizi wa Afrika Kusini katika eneo hilo la Wami Ruhindo na kupoteza maisha papo hapo.


Hapo kwenye red ebuniambie Lowasa kakulipa shilingi ngapi ?.Lowasa Olaigwanani' unaishia Monduli juu akienda Simanjiro wamasai hawamtambui kwanza hakuna hicho cheo kwa kabila la wamasai Lowasa kajipachika kama mtaji wake wa kisiasa.
 
Kweli Sokoine alikuwa shujaa halisi, daima tutamkumbuka.
 
Ndugu Edward Moringe Sokoine (01/08/1938-12/04/1984) alikuwa Waziri Mkuu wa aina yake nchini Tanzania. Aliongoza katika kipindi ambacho nchi ilikuwa katika hali ngumu sana ya kiuchumi. Ni miaka 27 toka Taifa limpoteze shujaa huyu. Katika kuenzi fikra zake ambazo bado zinahitajika sana leo, Ninaomba niwaletee ndugu wana jf baadhi ya nukuu nilivyowahi kuzipata kutoka kwenye Kitabu cha Edward Moringe Sokoine: Kiongozi wa Watu Aliyejitolea kilichoandikwa na Luteni Kanali Albert N. Kigadye mnamo mwaka 1984:
"Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na Wananchi peke yake. Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu" - Edward Moringe Sokoine, 26 Machi 1983​
"Juu ya suala hili la mapato kutolingana na matumizi ni kwamba tungependa kupunguza uongezaji wa wataalam wasiohitajika katika Serikali na katika mashirika ya umma mpaka hapo hali yetu ya uchumi itakapokuwa katika hali nzuri" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1982​
"Serikali inasimamia bei, lakini Serikali yetu itakwenda mpaka itasimamia bei ya mhogo, dagaa na bei ya kila kitu? Haiwezekani, vitu vingine ni lazima vizalishwe kwa wingi ili bei yenyewe iweze kujirekebisha" - Edward Moringe Sokoine, 24 Septemba 1983​
"Wajibu wa kila Mtanzania, kila familia na kila anayekula ni kujilisha mwenyewe. Si wajibu wa Taifa kumlisha mtu. Unaweza ukasaidiwa unapopatikana na janga. Lakini kama hakuna janga ni wajibu wa kila mtu aweze kujitosheleza kwa chakula na atoe ziada kwa Taifa" - Edward Moringe Sokoine, 4 Oktoba 1983​
"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asumuulize mwanae, 'mali hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983​
"Katika nchi inayojali haki na usawa, majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya walio wengi. Na kamwe hayaruhusiwi kuwa ni chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao na kusahau maslahi ya walio wengi" - Edward Moringe Sokoine, 1Februari 1977​
Nionavyo mie ni kwamba tuna mengi zaidi tunahitaji kujifunza kutoka kwa viongozi wetu waliotutangulia mbele za haki ama kwa kupitia kwenye hotuba zao au kwa kupitia kwenye maandiko mbalimbali.Na kwa kuwa jamii forum ni mojawapo ya maktaba muhimu kwenye uhifadhi wa habari muhimu za ujenzi wa Taifa letu la TANGANYIKA basi ninaona ni heri wote tuisome na kuitafakari kwa pamoja.
 
Ndugu Edward Moringe Sokoine (01/08/1938-12/04/1984) alikuwa Waziri Mkuu wa aina yake nchini Tanzania. Aliongoza katika kipindi ambacho nchi ilikuwa katika hali ngumu sana ya kiuchumi. Ni miaka 27 toka Taifa limpoteze shujaa huyu. Katika kuenzi fikra zake ambazo bado zinahitajika sana leo, Ninaomba niwaletee ndugu wana jf baadhi ya nukuu nilivyowahi kuzipata kutoka kwenye Kitabu cha Edward Moringe Sokoine: Kiongozi wa Watu Aliyejitolea kilichoandikwa na Luteni Kanali Albert N. Kigadye mnamo mwaka 1984:
"Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na Wananchi peke yake. Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu" - Edward Moringe Sokoine, 26 Machi 1983​
"Juu ya suala hili la mapato kutolingana na matumizi ni kwamba tungependa kupunguza uongezaji wa wataalam wasiohitajika katika Serikali na katika mashirika ya umma mpaka hapo hali yetu ya uchumi itakapokuwa katika hali nzuri" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1982​
"Serikali inasimamia bei, lakini Serikali yetu itakwenda mpaka itasimamia bei ya mhogo, dagaa na bei ya kila kitu? Haiwezekani, vitu vingine ni lazima vizalishwe kwa wingi ili bei yenyewe iweze kujirekebisha" - Edward Moringe Sokoine, 24 Septemba 1983​
"Wajibu wa kila Mtanzania, kila familia na kila anayekula ni kujilisha mwenyewe. Si wajibu wa Taifa kumlisha mtu. Unaweza ukasaidiwa unapopatikana na janga. Lakini kama hakuna janga ni wajibu wa kila mtu aweze kujitosheleza kwa chakula na atoe ziada kwa Taifa" - Edward Moringe Sokoine, 4 Oktoba 1983​
"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asumuulize mwanae, 'mali hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983​
"Katika nchi inayojali haki na usawa, majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya walio wengi. Na kamwe hayaruhusiwi kuwa ni chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao na kusahau maslahi ya walio wengi" - Edward Moringe Sokoine, 1Februari 1977​
Nionavyo mie ni kwamba tuna mengi zaidi tunahitaji kujifunza kutoka kwa viongozi wetu waliotutangulia mbele za haki ama kwa kupitia kwenye hotuba zao au kwa kupitia kwenye maandiko mbalimbali.Na kwa kuwa jamii forum ni mojawapo ya maktaba muhimu kwenye uhifadhi wa habari muhimu za ujenzi wa Taifa letu la TANGANYIKA basi ninaona ni heri wote tuisome na kuitafakari kwa pamoja.

dahhh ama kweli moringe sokoine alikuwa tofauti sana na lowassa, alikuwa na vision kubwa rip sokoine Nchi uliyoipigania ipo mbioni kugawanyika kigoma kuwa jamhuri, mtwara na lindi mbioni kuwa jamhuri, kilimanjaro mbioni kuwa nchi huru, haya yote yanatokea sababu ya rasilimali kutogawanywa kwa usawa na ufisadi wa viongozi na wananchi
 
"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asumuulize mwanae, 'mali hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983

KAZI KWENU MNAOTAKA SERIKALI IWAOJI VIJANA WAMEPATA WAPI MALIII?WAZAZI WAWAJIBIKE KWA HILO... KWAKUWATAJA WACHACHE NI.........MTOTO WA NGOMBALE,MWANASIASA ZITTO KABWE NK WENGINE TAJENI WADAU....
 
"Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na WANANCHI peke yake.

Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu" - Edward Moringe Sokoine, 26 Machi 1983
 
Nani alimuua Moringe? Motives zake ilikuwa ni nini?

Hebu tujiulize, laiti kama Edo angekuwa hai mwaka 1985+, Kambarage angempatia nani kijiti?

Naomba maelezo kwa wale wanaojua.

Maana tunapowajadili wale watu wa Kariakoo Gerezani kwa jinsi walivyoleta Uhuru wa Tanganyika huku wakimsaidia masikini Nyerere kwa kumpatia nauli ya kununua chakula Kariakoo, pia tumjadilki mtu huyu aliyekufa April 12, 1984 na sisi kizazi cha vita ya Idd Amin hatujapata maelezo ya kutosha mpaka leo tuko Ilimu ya Juu.
 
images1.jpg


Leo ni miaka 23 tangu Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine atutoke ghafla na kuacha simanzi na wingu la huzuni. Siku ile ya machozi na majonzi imebakia katika kumbukumbu za Watanzania wengi kama vile jana. Mfano wake ni kumbukumbu ya Wamarekani waliposikia habari za kuuawa kwa Rais John F. Kennedy. Kila mtu aliyekuwa mtu mzima wakati ule anakumbuka vizuri siku hiyo alikuwa wapi na alikuwa anafanya nini. Je pengo aliloliacha marehemu limeanza kuzibwa?

Je kuna kiongozi yoyote ambaye anakaribia sifa na utendaji kazi wa Marehemu Sokoine? Leo tunamkumbuka Edward Sokoine.

Pata kidogo chini hapa toka kwa mkuu Kyoma:

hii mada napendekeza ipelekwe Sticky
 
Mada nzuri hii, vema kujikumbusha,itatusaidia pia kuunganisha dots za yanayotokea leo!
 
Back
Top Bottom