Tunaomiliki usafiri na kukerwa na ambao tunawabeba lakini hawabebeki

TZ-1

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2020
Posts
4,321
Reaction score
7,501
Habari wadau, poleni kwa namna mambo yalivyo sasa maisha magumu na agenda za kipuuzi ambazo shetani anataka kuingiza katika maisha ya binadamu sisi.

Hapa naendelea wakati tunaishi na kujarbu kutatua changamoto zetu za maisha kama kujenga na kumiliki usafiri ambao utatoa point A kwenda point B sisi ambao tumeishi maisha ya mjini tulishazoea maisha haya kwamba jirani yenu ana miliki pikipiki au Gari asubuhi anawasha anasepa hakuna cha lift wala nini

Sasa upande huu wa mikoani shida ipo kwa watu ambao tunafanya nao kazi eneo moja. Nimekutana na mshikaji rika sawa na mimi na wote tukiwa wageni katika kituo tulichohamia sambamba tunaishi maeneo ya karibu kimakaiz ila ofisi zipo mbali. Mimi nina usafiri both Gari na pikipiki ila nikitaka kwenda job namchek twende au namkuta njiani namchukua huyo job (go and return ).

Tatizo moja lipo hapa jamaa huwa hajiongezi, siku alipe na siku isilipe na akilipa hatatoa 2000 kama ni pikipiki na kama gari 3,000/- hapo ni mwendo wa KM 32+ gari 1.8L na njia sio ya lami. Kilichonikera zaidi wiki 2 nyuma nimetoka kutengeneza pikipiki kwa almost tshs 200,000/- baada ya block na center cluch kufa lakini yeye alitoa 10,000/- na akaidai dah!

Mbaya zaid haitoi siku zote na akitoa anatoa kidogo sana na kikiharibika ni mimi.

Mimi kama binadamu nataka nimtue tuu kwa amani zote maana nishaona Watanzania hawezi hisani, mimi nimeweza kutumia vyombo vyangu vya usafiri zaid ya miaka 5 sasa bila ushirika wowote.

Mnaweza kuchangia mawazo au changamoto kama hizi.
 
Umeandika kwa lugha ya kihunihuni utadhani unawasiliana na masela wakuletee bangi getho kwako.Hapa upo uwanja mkubwa.Kuna baba,mama,wajomba,shangazi,shemeji na wapwa zako.Jitahidi lugha uandikayo iwe ina "akili"!Sichangii kitu.
 
Naomba ni kuulize swali.
Hivi usipo mpakia mtu yoyote kwenye gari lako au pikipiki huwa unatumia mafuta kidogo? Au hivyo vyombo vyako huwa havialibiki? Hivi wakati unanunua hivyo vitu ulikuwa unajua kuna mtu wa kukusaidia kutengeneza?
 
[emoji16][emoji16]
Umeandika kwa lugha ya kihunihuni utadhani unawasiliana na masela wakuletee bangi getho kwako.Hapa upo uwanja mkubwa.Kuna baba,mama,wajomba,shangazi,shemeji na wapwa zako.Jitahidi lugha uandikayo iwe ina "akili"!Sichangii kitu.
 
Ndio watu kama nyie ninao wajadili hapo, ushawahi kukamatwa na traffic ukiwa uliyempa lift hajafunga mkanda au kuvaa helements or any accident

You buy free for cost
Naomba ni kuulize swali. Hivi usipo mpakia mtu yoyote kwenye gari lako au pikipiki huwa unatumia mafuta kidogo? Au hivyo vyombo vyako huwa haviharibiki? Hivi wakati unanunua hivyo vitu ulikuwa unajua kuna mtu wa kukusaidia kutengeneza?
 
Kikubwa ni kuwa muwazi katika mambo yako yote, ukifanya hivi utakuwa na amani kabisa. Mueleze mtu jinsi ambavyo ungetaka achangie, kama sivyo kama unavyotaka basi msaada uishie hapo, ukiacha kufanya hivyo unakaribisha mashaka katika akili yako kuhusu msaada.

Kuwa muwazi.
 
Gari yangu ya kwanza nilinunua 2012 nikiwa na 21 years nikiwa chuo, aisee nilipata wenge kama miezi 4 ila nikazoea, namshukuru Mungu kuanzia hapo naonaga gari kama kitu Cha kawaida sana, mleta mada utakua umenunua gari hivi karibu I😂😂😂
 
Ndio watu kama nyie ninao wajadili apo , ushawahi kukamatwa na traffic akiw urempa lift ajafunga mkand au kuvaa elements or any accident

You buy free for cost

kwanini umuache hajavaa mkanda/helmet wakati ukiendesha? kama hajui je!!?
 
Wenge la gari ya kwanza ni balaa[emoji38][emoji38] nilikua nalala huku nacheka..nilinnua nikiwa na umri kama huo, napandisha vioo naongea peke angu tena kwa nguvu "Kwahiyo hii ndio gari yangu" [emoji38][emoji38][emoji38]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…