Tunaomiliki usafiri na kukerwa na ambao tunawabeba lakini hawabebeki

Well said
 
Ingependeza zaidi kama ujumbe huu ungemfikishia muhusika moja kwa moja..ulichofanya hapa ni KUMSENGENYA na kumfedhehesha kwa jamii ingawa hujamtaja kwa jina
 
Acha roho mbaya wewe , yaani unanua usafiri kwa ajili ya kuendea kazi kwako unategemea jirani akuchangie mafuta? Kwani ukienda peke yako na ukipakia mtu mafuta yataenda mengi?
 
Piga chini kichomi hicho
 
Naomba ni kuulize swali.
Hivi usipo mpakia mtu yoyote kwenye gari lako au pikipiki huwa unatumia mafuta kidogo? Au hivyo vyombo vyako huwa havialibiki? Hivi wakati unanunua hivyo vitu ulikuwa unajua kuna mtu wa kukusaidia kutengeneza?
Acha kupenda mteremko wewe
 
Mafuta yanaenda mengi?
Ndio, kuchukua mtu kwenye gari au pikipiki yako kunaweza kusababisha matumizi zaidi ya mafuta. Hii ni kwa sababu mzigo wa ziada unahitaji nguvu zaidi kuweza kusonga na kuendesha gari au pikipiki.

Kulingana na sheria za fizikia, uzito wa gari na pikipiki ndio unaoathiri matumizi ya mafuta. Uzito wa ziada unaongezwa na abiria mwenye uzito wa 70kg utasababisha gari au pikipiki yako kutumia mafuta zaidi kwa sababu inahitaji nguvu zaidi kuweza kuhamisha mzigo huo.

Kwa hiyo, ikiwa unapenda kuokoa mafuta, ni muhimu kupunguza uzito wa gari au pikipiki yako kwa kupunguza mzigo wa abiria na mizigo mingine isiyohitajika. Hii itasaidia kuongeza ufanisi wa matumizi ya mafuta na kuokoa gharama zako za mafuta.
 
Mtoa mada sioni kosa lako pengine watu wanajibu kihisia zaidi lakini tuache hilo kwa sababu kila mtu yupo huru kutoa maoni yake,kimsingi huyo jamaa unaempa lifti ya kila siku kwenda na kurudi kazini anatakiwa afanye maamuzi ya mtu mzima anejielewa na anatambua kuwa kuna kulipa bill kwenye maisha japo wewe ulifanya kama msaada ila sasa inaonesha unakuumiza jaribu kuwa mjasiri mueleze tu itasaidia
 

Ulishawahi kufanya tathmini ya ulaji wa mafuta ukimbeba hhuyo jirani yako na siku ambayo haujambeba? mfano kama haujambeba lets say unaweka afunane ukimbeba unaweka afukumi?
 
Acha kupenda mteremko wewe
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Katika watu ambo hawapendi mteremko nami nimo ila namwambia mtoa mada ukitoa msaada usitake malipo kama vipi amwambie huyo jamaa atoe nauli ili neno lift lisiwepo. Huwezi kutoa lift alafu ukadai pesa.

wewe unaona sawa mtoa maada anadai mpaka kuchangiwa pesa ya matengenezo ya chombo chake?
Ila kwakuwa hatujiuani niishie hapo.

Nikipata muda nitaandika story ya kumsaidia mtu kwenye DISSERTATION upande wa chapters: RESEARCH METHODOLOGY and SIMULATION RESULTS AND INTERPRETATION, bure kabisa na akataka anilipe nikataa kutokana na jinsi alivyo kuja kuomba na sikujua ana hadhi gani nilichojua kuwa ni mganga njaa mwenzangu anaye pambana apate master's, ila badae alikuja kunitafutia scholarships nje kupitia shirika la UN alilokuwa anafanyia kazi.
 
Sawa mkuu Umeongea vyemaa
 
Mimi nipo nje ya mada kidogo
Kwanini utembee Km 32 kwenda kazini na kurudi??

Mbona msiamie karibu na eneo la kazi ?? Especially huyo hasie na usafiri tena ni mkoani

Mimi nikiwa mikoani kikazi nakodi room 40000/50000 master nakaa karibu na kituo ambapo hata nikisema nitumie usafiri ni Tsh 1000 bodaboda jioni natembea kunyoosha miguuu
 
Usafiri ni wako afu unataka uchangiwe pesa ya service na mafuta???kisa unatoa lift ,[emoji848][emoji848][emoji848]???mambo madogo madogo kama hayo.
Sorry to say this bro,kinachokutesa ni roho mbaya na choyo.
Kwani wakati unanunua ukujua kuwa kuna mambo service na fuel?
 
Kuna kaz za ziada na ninaish kwangu
 
Hi dunia kwani ni yetu, Jifunze kupotezea baadhi ya mambo itakusaidia sana ulinnunu Gari lako ukijua utalimudu mwenyewe kumsaidia huyo mwamba ni kama umetoa sadaka tu.

Jamn mimi ndo maana sipendi lift za watu basi tu shida zinatudhalilisha
 
Mtoa mada mwambie huyo jamaa kuwa kuna mtu mwingine ameomba awe anachangia nauli ya usafiri wako ndio uko na sintofahamu maana pia unataka kupunguza gharama za usafiri na upande mwingine kuna yeye muomba lift. Hapo ataamua azike au asafirishe. Tabia za utegemezi hizo achana na wote wanakwambia eti una roho mbaya
 
Aksnt
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…