Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane

Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane

Katika pitapita zangu nimepitia shule hizi nyingi nikitaka kujua kama kweli watoto wanajua kiingereza hata cha kawaida tu. Nichokikuta ni kituko na ubabaishaji tu, watoto hawajui kuongea kiingereza fasaha, wanaongea kama walimu wao ambao wengi ni hawahawa ngumbaru wasiojua kikutafuna kiingereza vizuri. Walimu wao hawana misamiati ya kutosha kuweza kufundisha kiingereza fasaha. Walimu wenyewe ni form six plus diploma na wengine ni form four plus certificate ya ualimu, wapi wamejua kuongea lugha ya kiingereza? Ni ubabaishaji tu unaofanyika kwenye shule hizo za kiingereza. Wazazi wengi wenyewe tu lugha ya kiingereza hawaijui wanafikiri watoto wao wakijua kutamka dady, mom ndiyo tayari wamejua kiingereza. Wanaojua kiingereza ni wale wanachokitumia muda mwingi hata wakiwa nje ya shule
Hizi shule nyingi wanafundishwa kwa kingereza lakn watoto wengi hawajui kuongea kingereza.
Zile shule Fee Zaid 3M kdgo watoto wanajitahidi.
 
Mara ya kwanza kuibuka kwa shule hizi mlizishokea na kuziona ni za maana kuliko shule zilizokuwepo, mkadhani watoto wenu wakihitimu huko watajua sana kiiengereza na kufaulu sana kisha kupata ajira kumbe ulikuwa ni ulimbukeni tu. Sasa naona wazazi wengi wanaondoa watoto wao huko na kuwapeleka za kawaida, sijui ni kupunguza gharama au shule hizo zimepoteza umaarufu na hazileti matumaini kwa wahitimu wake
Hujui 7bu lkn una furaha wazazi kutoa watoto kwenye shule za kulipia na kuwapeleka shule za ELIMU BURE. HII ULIYOIONESHA NDIO TABIA HALISI YA MU AFRICA HATA WA TANZANIA.

MAOMBI YAKE MUDA WOTE NI WANAOMZIDI KIUCHUMI WAPOROMOKE ILI WALINGANE AMA WAWE CHINI YAKE ZAIDI (KUWACHUKIA WENYE KIPATO CHA ZIADA KUWAZIDI) BADALA YA KUJIFUNZA NI KWA NAMNA GANI WANAWEZA KUWA NA KIPATO KILE.

ENDELEA KUWACHUKIA WANAO KUZIDI KIPATO ILI MAFANIKIO YAO YAHAMIE KWAKO.
 
Kuna jamaa humu aliwahi kutoa ushauri ambao mimi binafsi ulinifurahisha na nitautumia mbeleni huko. Alisema, badala ya kutoa 1.5m kulipa ada ya mtoto wa chekechea, kama unapenda sana mtoto asome english medium, Weka bajeti ya 1.5m Tshs, ila tafuta basi hata zile za kanisa, zenye ada ya Tshs. 800,000/= kwa mwaka halafu Tshs. 700,000/= nunua viwanja vilivyopimwa vya Halmashauri za Wilaya mikoani huko au nunua ng'ombe wawili wadogo wa kufuga.

Kila mwaka mnunulie mtoto kiwanja 1 au ng'ombe 2, mpaka anamaliza darasa la 7 atakuwa na viwanja 7 ama ng'ombe 14 bila kuhesabu watoto wao. Sekondari asome hizi za umma (serikali) ila uendelee kumnunulia viwanja, mpaka form 6 atakuwa na viwanja 13 au ng'ombe 30 hivi.. huyo tayari ushamuandalia njia nzuri ya kujiajiri. Mtaji upo kwa kuuza viwanja vyake kadhaa au ng'ombe kadhaa.

Sababu kubwa ni kuwa unamwamsha mtoto aende shule huku mdogo wako amelala ndani kwa kukosa ajira na huku ana digrii. Unafanya kitu ambacho matokeo yake huna hakika nayo, unabet. Sasa ya nini kubet kwa kuweka madau makubwa???
Chukua hiyo.
 
Hujui 7bu lkn una furaha wazazi kutoa watoto kwenye shule za kulipia na kuwapeleka shule za ELIMU BURE. HII ULIYOIONESHA NDIO TABIA HALISI YA MU AFRICA HATA WA TANZANIA.

MAOMBI YAKE MUDA WOTE NI WANAOMZIDI KIUCHUMI WAPOROMOKE ILI WALINGANE AMA WAWE CHINI YAKE ZAIDI (KUWACHUKIA WENYE KIPATO CHA ZIADA KUWAZIDI) BADALA YA KUJIFUNZA NI KWA NAMNA GANI WANAWEZA KUWA NA KIPATO KILE.

ENDELEA KUWACHUKIA WANAO KUZIDI KIPATO ILI MAFANIKIO YAO YAHAMIE KWAKO.
mbona kama unatokwa povu?
 
Kuna jamaa humu aliwahi kutoa ushauri ambao mimi binafsi ulinifurahisha na nitautumia mbeleni huko. Alisema, badala ya kutoa 1.5m kulipa ada ya mtoto wa chekechea, kama unapenda sana mtoto asome english medium, Weka bajeti ya 1.5m Tshs, ila tafuta basi hata zile za kanisa, zenye ada ya Tshs. 800,000/= kwa mwaka halafu Tshs. 700,000/= nunua viwanja vilivyopimwa vya Halmashauri za Wilaya mikoani huko au nunua ng'ombe wawili wadogo wa kufuga.

Kila mwaka mnunulie mtoto kiwanja 1 au ng'ombe 2, mpaka anamaliza darasa la 7 atakuwa na viwanja 7 ama ng'ombe 14 bila kuhesabu watoto wao. Sekondari asome hizi za umma (serikali) ila uendelee kumnunulia viwanja, mpaka form 6 atakuwa na viwanja 13 au ng'ombe 30 hivi.. huyo tayari ushamuandalia njia nzuri ya kujiajiri. Mtaji upo kwa kuuza viwanja vyake kadhaa au ng'ombe kadhaa.

Sababu kubwa ni kuwa unamwamsha mtoto aende shule huku mdogo wako amelala ndani kwa kukosa ajira na huku ana digrii. Unafanya kitu ambacho matokeo yake huna hakika nayo, unabet. Sasa ya nini kubet kwa kuweka madau makubwa???
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom