Tunasimama na Lissu, alipo tupo

Tunasimama na Lissu, alipo tupo

Mkuu Lissu hapendwi kwa uzuri wa uso wake. Lissu anapendwa kwa ubora, mashiko, uthabiti, dhamira nk ya hoja zake. Huyu ndiyo wale viongozi ambao wakituita tutamwagika barabarani.

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Lissu anabeba uelekeo tunaoutaka. Kama Lissu angeyapinga haya:

Uchaguzi bila katiba mpya wa nini?

Tuna Imani na CHADEMA hii, wala si nyingine

Tungemvaa kama yeyote ayapingaye.

Kama johnthebaptist, Pascal Mayalla , Tulia, Kibajaji, Nape, Wassira, Samia au hata shetani wakiliunga mkono hili la katiba mpya kabla ya uchaguzi tutawaunga na kumpinga Lissu kama atachagua kulipinga.

Kwani mnatuona je?

Habari ndiyo hiyo.
Kusubiri kuamshwa..!!

Kwamba changamoto zetu hatuzijui mpaka aje mwingine atuamshe?!

Hao wanaogoma wameanza kuonesha kwa vitendo changamoto zao wanazijua, hawasubiri kuamshwa, hivyo wanapingana na hii kauli yako hapa.
 
Kusubiri kuamshwa..!!

Kwamba changamoto zetu hatuzijui mpaka aje mwingine atuamshe?!

Hao wanaogoma wameanza kuonesha kwa vitendo changamoto zao wanazijua, hawasubiri kuamshwa, hivyo wanapingana na hii kauli yako hapa.

Hao wanaopigana wana viongozi wao. Hao ndiyo wanaohamasha, fanikisha, ratibu, nk hiyo migomo.

Hakuna mgomo unaokuja bIla viongozi kama mvua.

Hao ndiyo tunaowasuburi. Kama hawafanyi wanachopaswa tutawatoa uongozini Ili tuifanye Kazi hiyo.

Zingatia viongozi hawatoki mbinguni. Wanafanya wajibu wao au tunawapiga chini na kuchukua hatamu za serikali!
 
Sidhani kama Chadema bado wana huo msimamo wa bila Katiba Mpya hakuna uchaguzi mkuu, wanavyoonekana kwa sasa majority wanaviwaza viti vya ubunge zaidi ya chochote kingine.

Hii ndio sababu iliyomsukuma Lissu kuwakumbusha wenzie bila KM hakuna uchaguzi mkuu, bahati mbaya kwangu ameenda kuwakumbushia kwenye jukwaa tofauti, sijui ni kitu gani kilichomfanya asiwatazame usoni awaambie straight wakiwa vikaoni.

Hapa ni either Lissu ameshakata tamaa amewaona wenzake ni watu wasio tayari kubadilika, kama hajawaambia basi ameamua kujikweza na kujiweka juu ya wenzie, au vyovyote vingine.

Muhimu kwa sasa kama Chadema bado wapo kwenye maridhiano, huku Lissu hayataki, na ikiwa ameshindwa kuvumilia au kuwaambia wenzake vikaoni, na kukaa kimya hawezi..

Naona Chadema kwa sasa sio tena sehemu sahihi kwake, kwani kuendelea kubaki Chadema na kuvunja taratibu kwa kusema mambo kinyume na msimamo wa chama, hata kama yanapendwa kusikiwa na wengi, ni mkaidi, anayestahili adhabu, bitter truth.
Hoja ya msingi kabisa.
 
Back
Top Bottom