Tunawezaje kuzuia double agents, inazidi na itazidi kuwa changamoto

Tunawezaje kuzuia double agents, inazidi na itazidi kuwa changamoto

Hili jambo la Viongozi wetu kuwa karibu au na mahusiano Na double agent Ni hatari sana. Mwezi huu January nimekutana Na hii ngozi nyeupe Na nikiwa naongea naye akanitajia contacts kibao za viongozi wetu wanao taka kumnyandua...Na anayajua mambo Mengi ya huko Zanzibar...wanamuomba ufafhiri wa kujenga shule bila kujua Ni hohe hahe Kama Yule wa “ mama Samia Nipe uraia” nikachezee taifa stars toka Hemel Hempstead...
Viongozi wa enzi za kifimbo ndio walio kuwa serious Na haya mambo ya Agent, lakini sio hawa wa siku hizi...
 
Nafahamu kuna wengine wachache wameuchukulia uzi huu in a negative way, wala hauko hivyo, niliyoyasema ndiyo kweli yenyewe msiyotaka kuisikia,
Leo hii hata nikikuambia uvuke boda hapo uende Kenya, ukashangae mpaka leo hatuna ubalozi wa kueleweka tumepanga ghorofani tena upande mmoja wa floor [emoji24], nayo utakataa, halafu unategemea ufanye kazi kwa weledi,
Wakuu tuisadie nchi yetu, safari bado ni ndefu sana, tuache u much know na tamaa za mali, mali huisha lakini nchi itabaki, ukielezwa kitu fikiria kwann umeulizwa siyo kubishana
muwe na jumapili njema ndugu zangu.[emoji120]
 
Hili jambo la Viongozi wetu kuwa karibu au na mahusiano Na double agent Ni hatari sana. Mwezi huu January nimekutana Na hii ngozi nyeupe Na nikiwa naongea naye akanitajia contacts kibao za viongozi wetu wanao taka kumnyandua...Na anayajua mambo Mengi ya huko Zanzibar...wanamuomba ufafhiri wa kujenga shule bila kujua Ni hohe hahe Kama Yule wa “ mama Samia Nipe uraia” nikachezee taifa stars toka Hemel Hempstead...
Viongozi wa enzi za kifimbo ndio walio kuwa serious Na haya mambo ya Agent, lakini sio hawa wa siku hizi...
Ngozi ipi hiyo mkuu
 
Ila binadamu kwa namna tulivyojawa na husuda unaweza kukuta maelezo ya kwenye namba 1 na 2 yote hayana maana ila mlengwa wa mleta mada ni huyo "Kumbikumbi" aliyewekwa namba 3 ili tu kumharibia.
It seems so
 
1. Mara ya kwanza nipo Bole International Airport kwenye harakati zangu akanifuata binti mmoja mwenye asili ya Comoro na Zanzibar, nafikiri yule ni mshirazi (mbwera), akaniuliza maneno mawili matatu, nikamjibu nilivyoweza, akaniambia anatoka Zanzibar anaelekea Seychelles(ushelisheli), katika kuzoeana pale wakati tuko transit(almost 2hrs), nikagundua huyu si mtu wa kawaida, akili ikagonga, alikua amevalia hijab na niqab, lakini sura ilikua inaonekana vizuri sababu baada ya story kunoga alitoa niqab kiasi, kutest uhalisia ya yale mambo aliyokua akinieleza nikamuomba tupige selfie kadhaa, mwanzoni akakataa, nikaweka noti, then baadae akakubali, nikaweka noti pia, nikabaki na ukumbusho wa sura maana dunia kijiji kuna siku naweza kutana nae, kuhusu elimu yake kasoma Zanzibar, then Uingereza kwa ufadhili wa serikali ya Zanzibar, ni Pilot na vyeti alinionesha, ila majina alificha, akasema hana kazi, so hua anapenda kusafiri, sasa anaenda kufanya nn ushelisheli, akaniambia mara nyingi hua kuna ndugu zake anaenda kuonana nao, baadae nikagundua ni mtu mwenye mahusiano ya karibu na baadhi ya viongozi wa serikali ya Zanzibar na ushelisheli kwa pamoja, nikanote kitu, possibly anakula huku na huku.

2. Mara ya pili nimeenda kumuona kiongozi fulani wa kisiasa nchi jirani, kwa hisani ya rafiki yangu, ilikua ghafla tu ili kutaka kujua kitu fulani cha kibiashara, nikakutana na kijana namfahamu kabisa, yupo pale ofisini, aliponiona ni kama hakutegemea, eye contact iligoma, kuhusu mwenyeji wangu, yeye hanifahamu vizuri na bahati nzuri kuna wakati utaifa wangu huchachanganya, hasa kwa majina yangu, na ninaweza kuongea lugha kadhaa za ukanda huu, kwa namna alivyoshtuka nikajua aliyokua anayafanya hayana afya kwa ustawi wake na nchi yetu, nikakausha mpaka leo, na wala sina mawasiliano nae, japo tukionana tunafahamiana.

3. Kuna yule kijana mwingine mweupe toka kanda ya kati, mtaalamu wa lugha ya kiswahili, sahivi yuko nchi jirani akitangaza vivutio vya utalii wa nchi hiyo na kusifia kila kilicho mbele yake, ni haki yake kufanya anachotaka na yuko huru kabisa, nafahamu inaweza kua kama nchi tuna manufaa nae lakini nikiongea kwa uzoefu wangu wa kuifahamu kanda hii na maeneo mengine mengi, nishauri wahusika, yule mtu asipewe access ya kujua mifumo na utendaji kazi wa nchi kiundani zaidi, kwa kisingizio cha lugha na diplomasia, hayo anayoyajua yanatosha. kati ya watu ambao instincts zangu zinaniambia si salama basi na yule yumo, tunaweza kuamua kumtumia kama nchi lakini nawaambieni kama hatukufanya hivyo miaka mitatu iliyopita, tumechelewa. Nazungumzia access za mifumo, si uteuzi wa kisiasa, huo uteuzi mtu yeyote anaweza kupata alimradi tu chama chenye nchi wameona unafaa

Lengo la uzi wangu huu ni kukumbusha kua, system zetu ziwe makini zaidi, siyo kila king'aacho dhahabu, vijana tunaowaamini wanafika bei kirahisi sana, kinachotokea wanatumwa kuleta taarifa hii wao wanapeleka kwanza za kwetu walizokusanya, halafu wanarudisha zile ambazo ni obvious kila mtu anaweza kuziona, Wengi wao ni millennials generation, hakuna namna ya kuwaridhisha isipokua tu kua makini, Double agents walikuepo, wapo na wataendelea kuwepo lakini isiwe kirahisi hivyo. Mdau wewe unaona kama nchi tufanye namna gani tafadhali?

Mbarikiwe nyote ndugu zangu.
Sisi sio watu wa bidii sana. Zamani ndio tulikuwa na cha kuficha hasa mipango ya wapigania Uhuru wa ukanda wa SADC, makazi yao, majina yao, future yao.
Tuna nini cha kuficha sasa? Hata viongozi sioni kama tunawaandaa.
Tuna nini cha kupelekwa Kenya au Rwanda?
Hatupangi ushawishi dhidi ya serikali za nje. Tuna nini cha kuficha?
Tunafanya ujasusi wa kisasa utakaousadia nchi?
Vitu tunavyovifanya vingi ni vya kawaida ambavyo havihitaji double agents ila observation ya kawaida tu na trend reading.
Chombo cha kulindwa nchi hii ni CCM as party na zile organ zake.
Ujasusi wa CCM unatakiwa kuwa imara kuliko ujasusi wenyewe wa ngazi ya Taifa.
CCM inatakiwa kutunza siri kuliko hata inayotunzwa katika ngazi ya kitaifa.
CCM inatakiwa kutunza mifumo kuliko kawaida.
Mipango ya CCM ndio mipango ya Tanzania.
 
Kati ya vitu ambavyo nchi yetu na walio kwenye nafasi za uongozi vimekosekana.
1. Ukosefu wa Uzalendo
2. Uadilifu na utawala bora.
3. Miiko ya utumishi
Mambo haya yanachochea kutumia yeyote kwa vyovyote wakati wowote ili mradi tu mtu huyo afanikiwe kuwa sehemu ya upigaji kwahiyo wageni wanaweza kuwa recruited kama wapambe waleta taarifa au vyovyote
Pia watu wananunulika ukitaka kujua kuwa iko hivyo angalia vyama vya siasa huyu alikuwa huku ghafla bin vuu yuko kule. Kwahiyo watu wako tayari kuwa chochote kama kuna chochote kitu.
Mipaka ya uongozi wala maadili hayapo yaani kila mtu ni kambale hii haipo.
Mi sijawahi kumkubali yule mswahili wa dar kwa kweli nauna uso wake uko kwenye maigizo tena ya wazi kuwa eti mpenda taifa. Tunaweza kusema tuna nini ambacho hawakijui spying sio lazima iwe kwa kivita kiuchumi au kiutamadani na jambo baya kuliko ni pale utamaduni wenu unapohujumiwa huo ndio utu wetu unaweza kujenga mifumo bora ya kiuchumi na kiulinzi.
 
Leo hii hata nikikuambia uvuke boda hapo uende Kenya, ukashangae mpaka leo hatuna ubalozi wa kueleweka tumepanga ghorofani tena upande mmoja wa floor [emoji24], nayo utakataa, halafu unategemea ufanye kazi kwa weledi,
Nimecheka kama mazuri vile! Kwahiyo UBALOZI WA TANZANIA umepanga OFISI YA UBALOZI kule KENYA 🇰🇪 🙌🏼😂
 
Mkuu licha ya umasikin wetu ila elimu yetu ni duni sana. Yawezekana tukawa miongoni mwa nchi zenye mifumo mibovu ya elimu.
Kenya ni maskini sana lakini elimu yao inawafichia aibu .
Bahati mbaya sana mpaka kufikia sasa watawalavktk nchi hii tu hawapendi wanachi wake waelimike
 
Back
Top Bottom