Tundu Lissu aitaka Serikali ya Kenya Kuingilia kati kutekwa kwa Maria Sarungi

Tundu Lissu aitaka Serikali ya Kenya Kuingilia kati kutekwa kwa Maria Sarungi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
1736750034870.jpeg

Taarifa yake iliyonukuliwa na Vyombo vya Habari hii hapa

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)-Bara, Tundu Lissu ameitaka Serikali ya Kenya kuingilia kati katika madai ya kutekwa kwa mwanaharakati Maria Sarungi.

Taarifa za kutekwa kwa Maria zimesambaa leo Jumapili Januari 12, 2025 baada ya mtandao wa kimataifa wa haki za binadamu-- Amnesty International kuripoti taarifa hiyo.

Soma Pia: Mwanaharakati Maria Sarungi adaiwa kutekwa na watu wenye silaha Nairobi, wakiwa na Noah nyeusi

“Maria alikuwa amekimbilia uhamishoni nchini Kenya tangu kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 ambapo amekuwa akiendesha televisheni ya mtandaoni ya Mwanzo TV, inayotoa maudhui ya kuunga mkono demokrasia.

“Ingawa tunatumai na kusali kwa ajili ya maisha na usalama wa Maria, ni lazima tutoe wito kwa Serikali ya Kenya na watu wote wenye nia njema kutoka duniani kote kuingilia kati, kuhakikisha usalama wa Maria,”ameandika Lissu.

Mwananchi
 
😂😂 Awapambanie waliotekwa chini ya utawala huu nchini kwake
 
Nasikia ilikuwa ni kiki tu kama ile ya Abdul Nondo😁
Sidhani ila bila shaka Kenya serikali isingeruhusu litokee kwenye ardhi yake baada ya kutekwa kwa Kiiza Besigye na kuibuka uganda basi kama hili maria angeibuka TZ au akafa ingezidi kuwatia doa kimataifa. Ngoja akizungumza kesho itafahamika kwanini kaachiliwa mapema
 
Sidhani ila bila shaka Kenya serikali isingeruhusu litokee kwenye ardhi yake baada ya kutekwa kwa Kiiza Besigye na kuibuka uganda basi kama hili maria angeibuka TZ au akafa ingezidi kuwatia doa kimataifa. Ngoja akizungumza kesho itafahamika kwanini kaachiliwa mapema
Serikali ya Kenya imekataa kutumika kuua watu
 
Kwahy watekaji wa JPM wamevuka mpaka 😂
Dharauu sanaaa.....kuna mtekaji mmj toka PK alikuja kimya kimya......akamteka mtu wake amsafirishe kimya kimya kwenye buti gari.....Mungu bariki....alikamatwa traffick kabla Morogoro....jamaa kwenye buti akagonga sana gari mateke....ngumi...deal ikaishia hapo......jamaa alikaa miaka 2 pale central ....diplomasia ikamuokoa ! Lakini yule mtu alipobea hapo...
 
Back
Top Bottom