Uchaguzi 2020 Tundu Lissu alikuja CHADEMA ikiwa na wabunge zaidi ya 50, anaondoka, ikiwa na Mbunge 1

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu alikuja CHADEMA ikiwa na wabunge zaidi ya 50, anaondoka, ikiwa na Mbunge 1

CHADEMA ambayo ilikuwa inanufaika na ruzuku ya zaidi ya shilingi milioni 328 kwa mwezi imejikuta katika hali mbaya baada ya ''Mtaalam wa sheria'' kuwaaminisha wanaCHADEMA kuwa anakwenda siyo kuifanya ipate ruzuku zaidi bali pia kuifanya iingie Ikulu.

Matokeo yake amekuwa ni kati ya wanasiasa ambao wameididimiza CHADEMA kimaslahi huku yeye akiamua kwenda kupata ''income support'' nchi za watu.

Kelele za ''mtaalam wa sheria'' kwenye majukwaa zilikuwa ni nyingi huku akiwaaminisha anaenda Ikulu lakini ufanisi ni zero.

Tukumbuke kuwa, Mwaka 2005, ''Mzee wa anga'' aliikuta CHADEMA ikiwa na wabunge 4 na baada ya Uchaguzi akaiacha ina wabunge 5.

Mwaka 2010, ''Baba Paroko'' akaikuta CHADEMA ikiwa na wabunge 5 na baada ya uchaguzi aliiacha ina wabunge 48.

Mwaka 2015, ''Fisadi Papa'' akajitosa na kuikuta CHADEMA ina wabunge 48 na kuiacha ina wabunge 70.

Mwaka huu, ''Mtaalam wa sheria'' ameikuta CHADEMA ina wabunge zaidi ya 50 na ameiacha ina mbunge 1 ambaye kwa aibu hataki kumtambua!

Unaweza kusema lolote au kuchanganua na kuchambua lakini ukweli utabaki palepale kuwa amekuwa ni mmoja wa watu walioiporomosha CHADEMA kimapato na kuikimbia haraka sana!

''Fisadi Papa'' ilimchukua miaka 4 baada ya uchaguzi Mkuu kuikimbia CHADEMA, huyu ''Mtaalam wa sheria'' hata mwezi mmoja baada ya Uchaguzi Mkuu haujaisha ameamua kuikimbia CHADEMA!

Wafuasi wake ''maandazi'' walituaminisha huyu ''mtaalam wa sheria'' sio kama ''Fisadi Papa'' kwa sababu ni jasiri na kwa maana hiyo ''chama cha kijani'' kisimpuuzwe!

Thread zilijazana hapa Jamiiforums za kumsifia ''mtaalam wa sheria'' kwa ujasiri na nguvu za kisiasa alizonazo huku mgombea wa ''chama cha kijani'' akiambiwa ajiandae kukabidhi Ikulu kwa kupenda au kutopenda baada ya Uchaguzi Mkuu.

Mtu mwenye akili timamu atajiuliza, imekuwaje mtu aliyetuambia haogopi lolote akimbie haraka iwezekanavyo!

Hizi ni baadhi ya thread za kumsifia ''mtaalam wa sheria'' ambaye alikimbilia kwenye majengo ya balozi za Ulaya baada tu ya kumaliza kuitisha maandamano yasiyo na kikomo!

Kinachofurahisha zaidi, ameamua kukimbia bila kuwaeleza makamanda ''maandazi'' kama amesitisha maandamano au bado yapo palepale!

LINK>>>
LINK>>>
LINK>>>
LINK>>>
Sijakuelewa! Uchaguzi upi? Kwani mwaka huu Tanzania kulifanyika uchaguzi!

Sent from my itel A11 using JamiiForums mobile app
 
Atarudi 2025 akiwaaminisha tena kuna usalama

Akishindwa atarudi ulaya
Jamaa wakati anakuja aliwaambia haogopi lolote lakini baada ya kupata ''political sucker punch'', kwa sasa anadai hakuna usalama nchini!
 
Mkuu Missile of the Nation, alichoandika Msemaji Kweli ni hitimisho la kile nilichokuwa naamini na kukisitiza humu JF kuwa msumari wa mwisho kwenye jeneza la upinzani Lissu amepigilia.

Mimi ni mpinzani wa demokrasia ya vyama vingi kwenye nchi maskini. Ni moja ya njia inayotumika na mataifa makubwa (mabeberu) kutawala nchi hizo kwa kuwagawa kimawazo, kifikra na kiutendaji - yaani "Divide and Rule”.

Toka kuanzishwa kwa vyama vingi 1992, kumekuwepo na msuguano ukikwamisha maendeleo. Viongozi wa upinzani wakitumika kukwamisha maendeleo. Wengi wao, bila kujitambua au kwa makusudi, waliamini kusifia mazuri yanayofanywa na Serikali ya Chama Tawala ni kukipa kiki ya kisiasa hivyo basi wamejikuta wakifanya kila hila kukwamisha maendeleo. Hili limekuwa bayana katika utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano iliyopiga marufuku siasa za majukwaani ili wananchi wachape kazi. Matokeo yake kila mtu ameona.

Sasa wafuasi wa upinzani, kama wewe Missile of the Nation na wenzio, mtaishia kujaza mitandao ya kijamii na lugha za kulaani, kuomba dua, na kila aina ya kufuru na kafara. Mnapaswa kutambua kuwa, kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa vyama vingi, Tanzania inakuwa salama na maendeleo yatakuwa kwa kasi. Nanyi vizabinazabina mtafaidi matunda yake.

Hatimaye wasaliti wamejitokomeza wenyewe kwa kujilipua kabisa na waliobaki wasamehewe tu makosa yao kwa kuwa wanaishi kwa fikira tegemezi.
Kabla ya vyama vingi tulikuwa na chama kimoja kwa miaka 30, Tulipata maendeleo gani?

Uliuwa na umri gani wakati Mwalimu anang'atuka mwaka 1985, unaijua hali tuliyojuwa nayo kama nchi wakati huo?

Mabeberu wakitaka kuing'oa hiyo CCM yako haiwezi kulast hata wiki moja, wao ndo waliipa TANU serikali na wao wakitaka wanaweza kuijengea mazingira CCM ikang'oka!

Ndiyo maana Jiwe anatuvimbia sisi wananchi lakini Mzungu akikohoa tu chapcha tu anarufi msitarini. Wewe unafikiri bila mzungu kuingilia kati huyo Lissu angeachiwa aondoke?
 
Hivi kweli unaweza kutumia mda wako kuandika ujinga kama huu, wakati dunia nzima inajua jiwe alichokifanya
 
Mmeshinda uchaguzi, kaeni kimya
Kumchagulia mtu mzima nini cha kufanya ni sehemu ya udikteta!

Wewe kama unataka kukaa kimya basi kaa kimya. Waache wengine wafanye wanavyotaka kama hawavunji sheria za Jamiiforums!
 
Mkaambiwa andamaneni kumuondoa huyo wa chato mkajificha uvunguni mwa vitanda

Kuandamana ni njia moja, zipo nyingi sana, ni suala la kuamua itumike ipi na mazingira gani.
 
Haya mambo kama yana ukweli yasiishie kwenye mitandao, mpaka sasa ni kupost Twitter na JF inatakiwa hatua stahiki zichukuliwe tuambiwe ilitokea nini hiyo tar 27/28 mpaka watu wakapigwa risasi.

Ipo tume ya haki za binadamu,mahakama zipo n.k

Hakuna mahakama Tanzania za kuzuia mipango ya dictator.
 
Taarifa za awali zilisema ana tiketi ya ndege ya tarehe za mwezi Desemba, ghafla kapata ya mwezi November! Salary Slip anajuta kumfahamu Antipasu. Alivyomtosa ezi za MIGA na acacia somo hakulielewa...kwa sasa atakuwa amemuelewa Antipasu vinginevyo awe amekodi IQ yake kwa muda huu.
Kuna mwanajamiiforums pale juu amesema, alipokuwa anakuja alituambia haogopi chochote lakini baada ya kupata kipigo cha mbwa koko kwenye sanaduku la kura, amebadilika na kudai maisha yake hayako salama inabidi aondoke haraka!
 
Mmebakiza kilio hicho? Kama ni dikteta mlipata wapi huu uhuru wa kufanya kampeni kisha wananchi wakawakataa?

Kura za kwenye mabeg ndio wananchi au unadhani hatukuona kilichotokea? Kwani kupiga kampeni kunaondoa ukweli vwa udictator?
 
Hawa jamaa niwa kuwapa huruma!

Wamesahau walikuwa wanapiga kelele na kuimba NI YEYE!

Kipi cha ajabu, hata Yesu aliitwa mkombozi lakini aliuwawa na wayahudi. Halafu watu wanashangilia kuwa kwa kifo chake ndio walikombolewa. Toka nje ya box dogo.
 
Kura za kwenye mabeg ndio wananchi au unadhani hatukuona kilichotokea? Kwani kupiga kampeni kunaondoa ukweli vwa udictator?
Mnatengeneza video za uongo ili kudanganya watu kulikuwa na wizi wa kura!
 
Nilisha wahi kuandika mahali ikifika mwezi wa kumi ndio mwisho wa chadema na imetokea.
Jamaa alipotoka Belgium alikuja na mbwembwe nyingi sana nataka maandamano ya kunipokea, nataka nikija Dar isimame na nyingine nyingi.
Ila jana alipokuwa anaondoka hakuwa na tofauti na paka alienyeshewa.
1. Ameagwa na watu wasio zidi kumi
2. Amesindikizwa na Mabeberu.
3. Hata kuwaaga waliompokea kashindwa

Sasa sijuii akirudi tena atakuwa mgeni wa nani. Kwanza amekumbuka kulipa pango la nyumba aliyokuwa anakaa??
 
Itoshe kusema uchaguzi umepita tufanye ishu zingine

NB: Hakuna adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu ktk siasa.
 
Kuna mwanajamiiforums pale juu amesema, alipokuwa anakuja alituambia haogopi chochote lakini baada ya kupata kipigo cha mbwa koko kwenye sanaduku la kura, amebadilika na kudai maisha yake hayako salama inabidi aondoke haraka!

Hujisikia Magu anajisifia yeye ni jiwe na wala hajaribiwi, lakini kila anapoenda walinzi kibao. Kama yeye ni mwamba aje kariakoo bila walinzi kufanya shopping.

Akina Museveni, Kabila baba wote hao hawakuwa waoga, mbona walikimbia nchi zao na kurejea tena kuzikomboa? Au hujui maana ya kutokuwa muoga?
 
Back
Top Bottom