Tundu Lissu ameongea na Radio Citizen Kenya asubuhi ya leo, ameleezea hali ya usalama nchini pamoja na suala la Corona

Ukisoma kanuni za uchaguzi, kuna sehemu inayozuia wagombea kushambuliana kwa matusi ya binafsi. Kama unakumbuka, ubunge wa Wassira ulienguliwa baada ya uchaguzi wa mwaka 1995 kwa sababu Wassira alikuwa anaendesha kampeni za kumtukana Waryoba binafsi.

Tatizo sheria hizo ni kwa wabunge tu.
Rais akishinda, hakuna wa kumzuia
 
Serikali imeamua kumpuuza ajimalize mwenyewe....
 
Magufuli (yeye binafsi) hajawahi kutangaza 'waziwazi' kuwa anataka kubaki madarakani. Labda chini chini.

Just sayin.
 
Hapa ndo Tundu lissu huwa ananivunja nguvu mpaka kuwa na wasi wasi na weledi wake.

Amezungumza kwamba raisi alisema wazi wazi kwamba watabadilisha katiba ili awe rais wa maisha. Sasa jamani lini magufuli alitamka hili.....wafuasi walilisema na nakumbuka jinsi bushiru alivyo licrush hili suala.

Pengine ni pale alipozungumzia kuhusu corona. Kama yeye anawasiwasi na jinsi serikali alisimamia hili jambo jwa nini havai mask, kwa nini anafanya na anakwenda kwenye mikutano ya hadhara yenyewe mikusanyiko mingi. ? , kwa nini alirudi nchini akijua fika kwamba hali ya korona ni mbaya na serikali inaficha. Na pia kwa nini yeye hachukui hatua binafsi za kukabiliana na hili jambo.

Tundu lissu jitathmini. Siasa za Tanzania si za kukapakana matope bila akili kama kenya. Soma alama za nyakati. Unajiharibia mwenyewe.
 
Kama Hali ya corona ni Nzuri Kwa nini serikali wamebadilisha masharti kwa wasafiri wanaotoka na kuingia nchini??

Hivi hujui kuwa Magufuli anataka kujiongezea mda hao kina bashiru wanatumwa kupima upepo tu????
 
Rc
Magufuli (yeye binafsi) hajawahi kutangaza 'waziwazi' kuwa anataka kubaki madarakani. Labda chini chini.

Just sayin.
Anavyosema hakuna zaidi yake anayeweza kufanya anayoyafanya alafu kina Kessy na speaker yake ndugai wanasema atake asitake bunge lijalo wanamuongezea muda wewe unaelewaje????

Au wewe ndo wale mtafuniwe kila kitu???? Kweli CCM walaaniwe kwa kuleta shule za kata zilizoharibu upeo wenu wa kufikiri
 

Ni kweli magu anamapungufu yake ila huyu jamaa anapotosha vingi sijui ni kwamba hajui au ni makusudi mfano tu

- lini serikali imetangaza tanzania hakuna corona.
- mikopo anasema magu kakopa trilion arobain na ushehe sio kweli kabisa
- lini magu kasema atabadili katiba atawale milele.
- magu kaua utalii sio kweli kabisa
-magu kajenga mbuga ya wanyama chato, wakati ni game reaerve imepewa hadhi ya kuwa national park kutanua utalii usibaki kaskazini tuu na sehemu nyingine za nchi
Huyu jamaa anajiamaliza mwenyewe polepole hajui tuu ... First impression its the last impression
 
Tangu nasoma wachangiaji wanasema Lisu anatukana matusi bila kutaja tusi lengewe,najihoji nakosa majibu
 
Sioni ubaya katika hili ila mataga wa Lumumba hapa lazima nyongo iwapasuke! Wanahoji kwanini asitumie vyombo vya ndani? Vyombo vipi? TBC1 ptuuuuuuuu!
Sababu ya TL kufanya hivyo iko wazi. Vyombo vya habari vyote vya ndani vimebanwa. Kuna attempt ya kuvizuia hata vyombo vya inje kufanya hivyo.
 
Yaani mie huyu simuelewi kabisa, hivi wapiga kula wake wako kenya?, Watanzania wangapi wana access na hizo radio za kenya!
Vyombo vya habari vya hapa hm,vyote vimeshikwa makende,vikitangaza mambo ya upinzani,kesho utasikia vinadsiwa Kodi,na madudu kibao.

Ccm, wanatumia polisi, TCRA, jeshi, mgambo, hazina, usalama wa Taifa, Tume ya uchaguzi,
Wapinzani Wana nini?

Unaingia kwenye mechi, Refa, na wasaidizi wake wamechaguliwa na mpinzani wako,wewe una mchezaji mmoja,mwenzio Ana kuminambili!!!

Harafu ukipiga kelele,watu wanakushangaa,
Tuwaonee huruma wapinzani,
Ukweli mchungu ni kwamba,uchaguzi huu ukisimamiwa na UN,ccm kwaheri,hata wao wanajua,Kama wanajiamini kwanini tumesio huru?!!
Vyombo vya habari vinabanwa mbavu,
 
Alishatangaza ye ana damu ya kenya..na damu ndio inaendesha kila kitu mwilini..kwa hiyo jua tu tunadili na mkenya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…