FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Sioni shida yeyote ile kupiga kampeni dhidi ya mgombea wa chama unachoshindana nacho katika Uchaguzi. In fact, mgombea wanayeshindana naye ndio huyo huyo aliyeko madarakani na ndio huyo anayetafuta kuchaguliwa tena kwa muhula mwingine.Lissu na Membe wao wanapiga kampeini za hasira binafsi dhidi ya Magufuli; hilo linajulikana kabisa; siyo kuwa wanashindana na sera za CCM. Sasa awe makini atakapokuwa anatumia vyombo vya nje kumtukana Magufuli kama alivyokuwa anafanya alipokuwa Ulaya. Watangazaji wa Kenya wanaweza kabisa kumwuliza maswali yanayoelekea huko, na akishindwa kuwa makini atajikuta anatoa matusi tena, jambo litakalokuwa inakiuka kanuni za uchaguzi.
Unawezaje kushindana na sera za chama cha mgombea unayeshindana naye bila kumgusa mgombea huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho?
Ni nchi gani ya kidemokrasia ambayo mgombea Urais aliyeko madarakani huwa hashambuliwi kwa maneno na vyama pinzani wakati wa kampeni?
Hata katika nchi zilizoendelea na za kidemokrasia kama vile Marekani ambayo pia inakaribia kwenye Uchaguzi, mgombea wa chama kilichopo madarakani [Donald Trump] anashambuliwa vivyo hivyo kwa maneno na wapinzani wake [Democrats]. Hivyo ndivyo siasa ilivyo hasa katika kipindi cha karibu na Uchaguzi.