Tundu Lissu ameongea na Radio Citizen Kenya asubuhi ya leo, ameleezea hali ya usalama nchini pamoja na suala la Corona

Tundu Lissu ameongea na Radio Citizen Kenya asubuhi ya leo, ameleezea hali ya usalama nchini pamoja na suala la Corona

Awe makini kuhusu maswali ya mtego kuhusu Korona.

Wakenya wanataka kumtumia Lissu kipropaganda kuhusu ishu ya Korona ili ionekane sisi Watanzania tumefanya ujinga tulivyopambana na Korona halafu wao Wakenya eti wamefanya vyema na malockdown yao.

Lissu akumbuke tu wapiga kura wake watarajiwa yaani Watanzania wanamuunga mkono sana Magufuli kwenye ishu ya kutoweka lockdown, kwa hiyo asiwape Wakenya wanachotaka yaani "endorsement" kutoka ndani ya Tanzania kwa jinsi wao walivyodeal na Korona. Maana sasa hivi ndani ya Kenya kuna public pressure ya kutaka Kenya ifanye kama Tanzania!.

Swali la Korona inabidi Lissu alijibu kisiasa, ila akijaribu kuiponda approach ya Magufuli alivyohandle hilo suala atapoteza uungwaji mkono nchini. Magufuli alifanikiwa kuvurugavuruga vyanzo vya taarifa rasmi kuhusu Korona, kisha akapiga propaganda kubwa sana kuwa tumeidhibiti Korona kiasi kwamba sehemu kubwa ya umma inakubaliana naye. Kwa hiyo inahitaji akili ya ziada kucrash sehemu kubwa ya approach ya Magufuli katika mapambano dhidi ya Korona
Nimeisikiliza audio amejibu vyema sana kuhusu Covid19
 
Ushamba mwingine. Tangu Lisu aje Tanzania, umeshaona TBC waki-cover shughuli zake? Au mnataka media za Kenya nazo ziwe kama TBC ili msherehekee? Yaani binadamu wengine mnasikitisha sana. Hapa Tanzania mnapiga vyomboo vya habari faini kumzumgumzia Lissu.

Sasa vyombo huru Kenya vinamhoji, pia mnavimba. Kweli hasidi ni hasidi. Ucheke, unune haina tofauti kwake. mmefanya siasa wenyewe kwa mika 5 wakati wengine wakikamatwa na kupigwa mabomu kwa kufanya vikao vya ndani. Bado tu hamjiamini na roho zenu zimepinda kama korosho.
Huyu anataka kuongoza hii nchi.. huku akikimbilia kutuonyesha hataki kutumia.. vyombo vya habari vya nchini.. huyu angeuza nchi yetu kama angebahatika kuchaguliwa kuwa Rais..

Anaonyesha yupo radhi.. media za nchi za nje ziendelee.. kuliko za nchini.. mpenda mabeberu.. hajali uchumi wa nchi yetu.. wala kusaidia kutengeneza ajira.. kwa sababu kawaona bora Kenyans waendelee.. poleni washabiki wake wafwu..

Magufuli 💯 Mzalendo
 
Kaidanganya mahakama kuwa yupo karantini kumbe anazurura kila mahalo atakap. Siku akikum ana na rungu la mahakama aslete deama.
Kama covid ipo mbona hachukui hatua kujizuia asiambukizwe? To
View attachment 1532649

Hii ndio taarifa mpya inayozagaa mitandaoni kwa sasa .

wote mnakaribishwa

===


Mgombea wa Urais, kupitia Chama cha Upinzania CHADEMA Tundu Lissu, alivyohojiwa na Citizen Online Radio Station, kutoka Nairobi Kenyan Tundu Lissu aongea mengi kuhusu mustakabali wa Tanzania, ambae anagombania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020

Katika mahojiano hayo Waandishi wa habari Vicent Ateya na Meody Sinzore wa kipindi cha Jambo Kenya wamemuuliza masuala mbalimbali ya Kinchi na uchaguzi kwa ujumla.

Wakiuliza kuhusu suala la usalama kwa wagombea wa Upinzani Tundu Lissu amesema "Kama ambavyo nimesema mara nyingi hali ya nchi ya Tanzania sio suala lenye afya hata kidogo. Ukizungumzia sisi wa Chadema, viongozi wetu, wanachama wetu wameuawa katika mazingira ambayo hakuna uchunguzi wa Polisi hakuna chochote kilichofanyika."

"Kuna watu wetu wametekwa nyara miaka zaidi ya miwili mwandishi wa habari Azory Gwanda alichukuliwa nyumbani kwake na hajilikani alipo". Ben Saanane hajulikani alipo tangu Novemba 2016. Watu wameumizwa sana. Mimi nimeponea chupuchupu nimepigwa risasi 16. Mwenyekiti wangu amevunjwa mguu kama mwezi mmoja na ushehe uliopita, hali imekuwa mbaya kwelikweli.

Kwahiyo tunapozungumza kuwa Tanzania ina hali mbaya tuna maana hiyo. Hali ya haki z binadamu imeporomoka sana. Sio sisi tu tunaolalamika bali hata mashirika ya haki za binadamu ya nchini na kimataifa yanasema hivyo hivyo.

Sasa tunakwenda katika uchaguzi Mkuu ambao utakuwa ni wa kihistoria. Rais Magufuli na Chama chake wamesemahadharani bungeni kwamba wakishinda watabadilisha katiba kuondoa ukomo wa madaraka. Maana yake ni kwamba tutakuwa na Rais wa Maisha. Sasa sisi ambao Mwalim Nyerere alisema hatuwezi kuwa na Rais wa Maisha kama ilivyokuwa kwa kiongozi wa Malawi Kamuzu Banda, atuwezi tukakubali kurudi kwenye utawala wa aina hiyo.

Rais Magufuli mwenyewe alitangaza tarehe Febuali 6,2016 kwamba anataka kuangamiza vyama vya upinzani ifikiapo mwaka 2020. Sisi hatutokubali kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja. Uchaguzi huu utaamua mambo mengi sana katika nchi yetu na tunaamini kwamba watanzania hawatamkubalia Magufuli na ajenda yake na Chama chake ya kuturudisha katika miaka ya giza ya utawala wa chama kimoja.

Aidha, wakimhoji jitihada za Tanzania katika kukabili Covid 19 Lissu ameeleza kuwa Majirani zetu wote wana Corona, Tanzania ukitangaza kuwa kuna Corona ni kosa la jinai. Katika hili Lissu amesema "Sasa serikali inayoamini kwamba hakuna Corona na inawatangazia watu hakuna Corona haijatoa taarifa yoyote ya maambukizi, ya waliofariki, ya waliopona tangu tarehe 29 mwezi wa nne mwaka huu, wanaamini kwamba tukinyamaza basi Corona itapotea. Tusiposema chochote kuhusu Corona maana yake Corona hamna. Huo ndio msimamo wa serikali yetu.

Mwisho, Tundu Lissu amewashukuru Redio hiyo ya Kenya kwa kumhoji na kuweka bayana kuwa tangu amefika nchini mpaka leo hakuna kituo chochote cha habari kilichomwita na kumhoji kwa sababu viombo hivyo vinaogopa kuzuiliwa.
 
Wapambe siyo wagombea; iwapo wapambe wa CCM ndio walikuwa wanamtukana wao siyo wagombea na wala tume haishughuliki nao. Tatizo ni pale mgombea mwenyewe ndiye anayerusha matusi.
Ndiyo sheria inasema hivyo!!? Sasa zile push up zilikuwa na malengo gani... Si ndiyo matusi ya rejareja hayo.
 
Ndiyo sheria inasema hivyo!!? Sasa zile push up zilikuwa na malengo gani... Si ndiyo matusi ya rejareja hayo.
Push up siyo tusi ingawa inaweza kuwa ni kejeli lakini siyo tusi linaloweza kulalamikiwa mbele ya sheria. Matusi yantolewa kwa maneno ambayo yakihusisha utambulishi wa anayetukanwa na yanaweza kuthibitishwa mbele ya sheria.
 
Push up siyo tusi ingawa inaweza kuwa ni kejeli lakini siyo tusi linaloweza kulalamikiwa mbele ya sheria. Matusi yantolewa kwa maneno ambayo yakihusisha utambulishi wa anayetukanwa na yanaweza kuthibitishwa mbele ya sheria.
Embu mkuu niambie kuna tusi gani katukana kweny hii audio???
 
Mwaka huu mtavimba hata mtapasuka.

Mwambieni Meko aache ukandamizaji kwa vyombo vya habari vya Bongo la sivyo Lissu atatumia hata CNN kufikisha ujumbe kwa watanzania.

Asubuhi tarehe 28.10.2020 kabla ya jogoo wa kwanza Lissu anaukwaa Urais wa Tanzania
 
Kaidanganya mahakama kuwa yupo karantini kumbe anazurura kila mahalo atakap. Siku akikum ana na rungu la mahakama aslete deama.
Kama covid ipo mbona hachukui hatua kujizuia asiambukizwe? To
Nje ya mada
 
Embu mkuu niambie kuna tusi gani katukana kweny hii audio???
Audio sijaisikiliza; nitafanya hivyo baadaye. Hayo uliyokwoti ni mtililiko wa maswali na majibu yaliyotokana na tahadhari niliyotoa jana kabla hajafanya inteview; nilisema ajizuia asitumie lugha yenye kuwa kutafsiriwa kuwa ni mtusi kwa Magufuli kwani itakuwa ni kinyume cha kanuni za uchaguzi. Kama ali-heed na kujizuia kutoa matusi au kuzusha mambo yasiyo kweli kwa nia ya ku-embarass mgombea mwenzake, hiyo ni sawa.
 
Yaani mie huyu simuelewi kabisa, hivi wapiga kula wake wako kenya?, Watanzania wangapi wana access na hizo radio za kenya!
Sasa ndugu yangu ili umuelewe ulitaka akaongelee wapi? sisi watanzania wagumu sana kuelewa jaman, unaambiwa media zote za kibongo zimegoma kumpatia coverage sasa ww ulitaka akaongelee kwenye media gan? wakati mwingine tuweke unazi pemben jaman maendeleo hayana vyama
 
Akishindwa kwenye uchaguzi...(100% atashindwa mapemaa) namshauri pia maandamano ya kupinga "wizi"wa kula yaanzie Kenya maana wao wana uzoefu wa kuandamana!
Mchekeshaji mmoja wa Kenya aliwahi kusema kuwa wakati wa vurugu za baada ya uchaguzi kuna kabila moja liling'oa reli ili CNN na Aljazeera wapate "picha" nzuri huku kabila jingine likiokota vyuma vilivyong'olewa na kwenda kuuza kama chuma chakavu na kupiga hela saafi!
Lissu anatumia "akili" za kabila la kwanza!
 
Ukweli ni kwamba wananchi wengi wamemuelewa sana rais jinsi amedeal na issue ya corona, sasa Lissu akipuyanga kwenye hilo atapoteza mvuto.
Apuyange mara ngapi, ameishaharibu upande ule huku hawa wenzake wakimuacha tu!
2414618_24gvpqh.jpg
 
Kuzuia vyombovya habari vya Tanzania kumhoji Lissu hakutawasaidu chochote sanasana Ni kumpiga teke chura ,kumuongezea mwendo ,awamu hii hebu punguzeni ushamba ,miaka mitano bado washamba tu na malimbukeni.
 
Awe makini kuhusu maswali ya mtego kuhusu Korona.

Wakenya wanataka kumtumia Lissu kipropaganda kuhusu ishu ya Korona ili ionekane sisi Watanzania tumefanya ujinga tulivyopambana na Korona halafu wao Wakenya eti wamefanya vyema na malockdown yao.

Lissu akumbuke tu wapiga kura wake watarajiwa yaani Watanzania wanamuunga mkono sana Magufuli kwenye ishu ya kutoweka lockdown, kwa hiyo asiwape Wakenya wanachotaka yaani "endorsement" kutoka ndani ya Tanzania kwa jinsi wao walivyodeal na Korona. Maana sasa hivi ndani ya Kenya kuna public pressure ya kutaka Kenya ifanye kama Tanzania!.

Swali la Korona inabidi Lissu alijibu kisiasa, ila akijaribu kuiponda approach ya Magufuli alivyohandle hilo suala atapoteza uungwaji mkono nchini. Magufuli alifanikiwa kuvurugavuruga vyanzo vya taarifa rasmi kuhusu Korona, kisha akapiga propaganda kubwa sana kuwa tumeidhibiti Korona kiasi kwamba sehemu kubwa ya umma inakubaliana naye. Kwa hiyo inahitaji akili ya ziada kucrash sehemu kubwa ya approach ya Magufuli katika mapambano dhidi ya Korona

Lisu hajielewi na anafikiri hao ndio voters. Wewe ulikuwa una campaign watu wanyimwe misaada leo umewapenda uwatumikie?

Hiyo reference ya Mwl Nyerere alishasema hapo nyuma mwalimu aliishi kiujanja ujanja which means was not credible. Leo tena kawa reference.
Yet huwezi chukua dora kwa kuvitukana vyombo vinavyotakiwa vikulinde.

Hao Wazungu anaofikiria yeye na Membe eti watatusaidia kukuletea maendeleoni kutokujielewa kabisa.
Hao Kenyas anafikiria wanampenda sana nooo ni interest zao tuu.

Good luck waiting to see what next after seeing Magu's land mark winning.
 
Lisu hajielewi na anafikiri hao ndio voters. Wewe ulikuwa una campaign watu wanyimwe misaada leo umewapenda uwatumikie?

Hiyo reference ya Mwl Nyerere alishasema hapo nyuma mwalimu aliishi kiujanja ujanja which means was not credible. Leo tena kawa reference.
Yet huwezi chukua dora kwa kuvitukana vyombo vinavyotakiwa vikulinde.

Hao Wazungu anaofikiria yeye na Membe eti watatusaidia kukuletea maendeleoni kutokujielewa kabisa.
Hao Kenyas anafikiria wanampenda sana nooo ni interest zao tuu.

Good luck waiting to see what next after seeing Magu's land mark winning.

Sisi Wakenya hatuna interest yoyote kwa Lissu, na asilimia kubwa ya Wakenya hata hawana habari ya nani huyo anaitwa Lissu, ni ile kwamba
- Sisi ndio taifa pekee kando na Tanzania ambapo tunatumia Kiswahili kama lugha ya taifa
- Maana kwamba atakayoyasema huku kwetu yataeleweka na Watanzania wenzake
- Mumemfungia media zote huko hana airtime wala uwezo wa kuhojiwa popote
- Media za Kenya huwa na uhuru wa kuhoji na kuuliza maswali ya kila aina, hivyo kwa saa nzima lazima alifunguka yote
- Media za Kenya hususan hiyo Citizen airwaves zake hufika hata Tanzania, hivyo anatumia hii fursa kujaribu kuwafikia mashabiki wake
- Kwetu hapa ni vigumu kuingilia media, leo hii hata Magufuli akimpigia rais Uhuru simu akimuomba azuie, wala hamna kitakachofanyika maana rais Uhuru hana uwezo huo, tunatumia katiba mpya na bora kuzidi zote ukanda huu, rais hawezi kuthubutu kufungia media yoyote ile kisa kiongozi kahojiwa hapo.
- Hapa labda niwashauri CCM mtumie mbinu nyingine, kama vile kupambana naye hoja kwa hoja, maana kufungia media zenu huko hakutasaidia kwa vile atatumia za Kenya, na hatuna namna ya kuwasaidia, atasikika Tanzania yote, labda sijui mzuie frequency zisifike huko.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] sasa mnashiriki uchaguzi kwa nini kama mnajua mtaibiwa kura.
Kushiriki ni haki hata watoto tunazaa japo tunajua hawataishi milele.
 
Back
Top Bottom