Pre GE2025 Tundu Lissu amteua Lema kuwa wakala wake uchaguzi CHADEMA

Pre GE2025 Tundu Lissu amteua Lema kuwa wakala wake uchaguzi CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mgombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa na makamu mwenyekiti anayemaliza muda wake, Tundu Lissu, amemteua Godbless Lema kuwa wakala wake katika uchaguzi unaofanyika leo.
View attachment 3209003
Kuteuliwa kwa Lema, ambaye si mjumbe wa mkutano mkuu kwa sasa, kumetangazwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, leo Jumanne, Januari 21, 2025 katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

"Nimepokea barua toka kwa Tundu Lissu akimchagua Godbless Lema kuwa wakala wake kwenye uchaguzi Mkuu, Miongozo ya katiba inamruhusu" - John Mnyika

View attachment 3209007
Akitoa tangazo hilo muda mchache kabla ya uchaguzi huo kuanza, Mnyika amesema suala hilo halivunji kanuni za uchaguzi.

Soma, Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA nafasi ya Mwenyekiti & Makamu Mwenyekiti 2025: Ni Mbowe au Lissu?
Wakala wa Mbowe ni Nani? Ni Ramadhani?
 
Safi, hii imekaa kimkakati zaidi.
Lissu anacheza na akili za wajinga.
FAM na TAL wanajua wanachokifanya.
Hii itaepusha malalamiko, endapo FAM akishinda.
Na kuepusha mpasuko
ila hotuba zao hasa ya lissu imeshusha temper ya wafuasi wake kuwa tayari kupokea matokeo wasiyoyatarajia!
 
Kwa jicho pevuu huu uchaguzi una ngumi hapo baadae kama sahivi tu kwenye kuhakiki majina watu wanazozana hivi asbuhi wapiga kura walitangazwa kuwa906 kufikia sahivi idadi imepiga u turn ni1007 Mpaka matokeo kutangazwa jumla ya kura ni2000
Vyovyote iwavyo, Chama wasimpe mshamba tu. Hiyo ndo Rai yangu kama mzoefu na mtaalamu wa siasa.
 
"Nimepokea barua toka kwa Tundu Lissu akimchagua Godbless Lema kuwa wakala wake kwenye uchaguzi Mkuu, Miongozo ya katiba inamruhusu" - John Mnyika
Si walisema hawataki kumuonaeneo hilo!!
 
Safi, hii imekaa kimkakati zaidi.
Lissu anacheza na akili za wajinga.
FAM na TAL wanajua wanachokifanya.
Hii itaepusha malalamiko, endapo FAM akishinda.
Na kuepusha mpasuko
Wananchi sio WAJINGA kiasi hicho wanashuhudia jinsi Mbowe navyogawa RUSHWA kama karanga na akishinda Watanzania wengi wanaenda kuipuuza CHADEMA na watasema...kunatofauti gani kati ya CCM wakati CHADEMA nao ni wala RUSHWA...
 
Wananchi sio WAJINGA kiasi hicho wanashuhudia jinsi Mbowe navyogawa RUSHWA kama karanga na akishinda Watanzania wengi wanaenda kuipuuza CHADEMA na watasema...kunatofauti gani kati ya CCM wakati CHADEMA nao ni wala RUSHWA...
Una uhakika kwamba CCM ni wala rushwa?
 
Back
Top Bottom