Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,909
- 32,414
Amesema viongozi wa dini..Friends and Our Enemies,
Katika mkutano wake na vyombo vya habari leo hii,Makamu Mwenyekiti wa Chadema anasema kwamba mabillion ya mapesa yanahongwa kwa makanisa na maaskofu ili kuzibwa midomo.
Kauli hizi ni kauli za uchochezi na zenye kuleta taharuki sana ndani ya Taifa,Makanisa na Maaskofu kazi yenu ni kushiriki katika vitendo vya Rushwa?
Baraza la maaskofu kupitia katibu wao Padre Kitima Wamekuwa hodari sana wa kutoa matamko ya kulaani na kuikosoa serikali,hapo hapo Tundu lisu anasema kuwa maaskofu na makanisa yamekuwa vinara wa kushiriki vitendo hivyo.
Tunataka Kuskia Matamko kutoka baraza la maaskofu kuhusu kauli hizi za Tundu lisu na chama chake cha chadema.
Sasa sijui unaelewa nini kuhusu "viongozi wa dini"?
Je, unakumbuka juzi tu hapo sheikh wa mkoa wa Arusha kapewa Land rover mpyaaa? Hauoni ile ni moja ya hongo za sa100 kwa viongozi wa dini.