CHADEMA tunashukuru kwa mrejesho wa ziara ya siku 12 ya Tundu Lissu na mgombea mwenza kutafuta wadhamini iliyowafikisha mikoa 16 ya Tanzania bara mikutano mikubwa sana na wananchi.
Kila mkoa sheria ya uchaguzi inataka watia nia Urais kupata wadhamini wasiopungua 200 kutoka kila mikoa 10 ya Tanzania bara na Miwili ya Zanzibar.
Ziara hiyo imewaonesha kuwa upinzani umekua zaidi na una nguvu kuliko ulivyokuwa 2015.
Mkurugenzi wa Uchaguzi yeyote anayegoma kutoa fomu za uchaguzi ni kosa na hivyo msimamizi wa uchaguzi anastahili kufutwa kazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi maana hawafai wala kutosha kusimamia mchakato mzima wa uchaguzi.
CCM wana hofu ndiyo maana kunatokea matukio mengi ya kuingilia mchakato wa uchaguzi ili wagombea wa CCM wapite bila kupingwa.
Mwaka 1958 mwl. Nyerere alihukumiwa kesi ya uchochezi ktk mahakama ya kihistoria ya Kisutu. Miaka 62 baadaye Tundu Lissu pia amekuwa mhanga wa kuitwa ktk Mahakama hiyo maarufu ya Kisutu na ametakiwa kutokea mbele ya Hakimu tarehe 26 Agosti 2020.
Siku ya tarehe 26 Agosti 2020 wamepanga nini mahakamani Kisutu, ni mwendesha mashitaka kuomba mbele ya Hakimu kuwa Tundu Lissu asomewe mashtaka mapya ili asipewe dhamana.
Njama ya kuitwa Kisutu tarehe 26 Agosti 2020 yabainishwa kwa kuwekwa hadharani leo
23 Agosti 2020 mkutano na waandishi wa habari Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA
Source: CHADEMA MEDIA TV