Tundu Lissu awataja Majaji wa Kikwete wasio na Sifa (Kazi ndio inaanza)

"Mtu anachaguliwa kwa mujibu wa katiba alafu anashindwa kuilinda katiba....hatufai kabisa....aende shambani kwake akalime"Nyerere.
Ila sinakumbukumbu kama kweli rais huyu alichaguliwa kwa mujibu wa katiba.Huenda ndio maana anaichezea.
 
Tundu na zito hawatofautiani kitu katika kujitafutia umaarufu binafsi,tofauti yao ni kuwa tundu anabebwa na dini yake mbele ya pro chadema,wanampenda na ujinga wake

nashindwa kuelewa kama umeisoma vizuri hoja ya Lisu kwa aina ya mchango unaotoa katika hoja hii.Sikufikiri kama kuna watanzania wanaoweza kutoa michango ya aina hii kwa hoja nzito kama hii.
Tunao wengi, akina Mulugo na yule mganga mkuu wa mkoa fulani hapa Tanzania ambaye pia hoja yake ililetwa humu humu kwenye JF.
 
Huyo Tindu Lissu ni Mdini tu.Amewalenga waislamu ili awachafue.Christian Democratic Movement in Action. Sio aliyewateua ndio mdini. Hatahivyo kuna waislam wengi wenye sifa zilizotajwa na Mh. Tundu Lissu.
 
Kama madai ya Lissu ni sahihi basi hatuko salama!
Kwanini yasiwe sahihi wakati wajibu hoja hujibu kwa ujumla badala ya hoja kwa hoja.. kwamfano mtu katajwa kwa jina na tuhuma unapojibu lazima umtaje kwa jina na utetezi (hoja) wako sio kusema kwa jumla tu kwamba taratibu hufuatwa.
 
Huyo Tindu Lissu ni Mdini tu.Amewalenga waislamu ili awachafue.Christian Democratic Movement in Action. Sio aliyewateua ndio mdini. Hatahivyo kuna waislam wengi wenye sifa zilizotajwa na Mh. Tundu Lissu.
Hebu fafanua udini umekaa vipi hapo.. yani kuitaka serikali kufanya kazi kwa mujibu wa katiba ni udini.. kweli unakazi. Mwenyewe unakiri kuwa wapo waislamu wenye sifa, sasa kwanini asiwateue hao anakwenda kuteua wenye walakini?
 
Lissu na ateue wake; Raisi ameteua kwasababu wanasifa zinazotakiwa hata leo hii Lissu akiteuliwa wapo watu watasema Lissu hana sifa; sasa kama huyu mwanaharakati wenu Lissu na atue jopo lake la majaji.

Mkuu hujaji kitu hoja ya lissu ipo wazi vigezo umepewa sasa mbona hujibu hoja.
 
Kwa kifupi kabisa kipengele hii peke yake inatosha kum-impeach Rais Kikwete kwa kuvunja na kuendelea kuvunja katiba ya Jamhuri ya Tanzania:

"Lissu alifafanua kuwa, katika hoja zake alisema kuna baadhi ya majaji waliteuliwa bila kuwa na sifa maalumu kama zilivyobainishwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara 109, kipengele cha 6, 7 na 8.

“Ibara hiyo ya 109 kipengele cha 6-8 kinasema; mtu anaweza kuwa Jaji iwapo tu ana shahada ya sheria kutoka katika chuo kinachotambuliwa kisheria, awe ameshakuwa hakimu, awe ameshakuwa wakili na kusajiliwa na sifa zote hizo ziambatane na utumishi wa miaka kumi mfululizo.

“Lakini sifa zote hizo lazima mtu anayeteuliwa kuwa Jaji awe nazo kwa miaka kumi mfululizo. Sasa badala ya kuzungumzia masuala hayo kwa ujumla jumla, ningependa wanaonijibu watamke wazi wazi Jaji Mbaruku Salumu Mbaruku alisoma chuo kipi na akapata shahada ya sheria iliyompa sifa ya kuwa jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar kabla ya kuteuliwa kuwa jaji wa Mahakama ya Rufaa hadi sasa,” "

Wananchi sisi ni waoga lkn hii ni skendo kubwa ajabu tena ya kimataifa. Kisheria hii ni kosa kubwa kuliko Clinton kudanganya kuhusu Monica Lewinsky .. hii ni unconstitutional, deliberate and direct interference of executive branch in the judiciary branch! Huu ni uvunjaji wa misingi ya demokrasia!
 
"Nchi hii inanuka udini..... yaani mtu leo hii anaongelea udini! Badala ya kuongelea ujenzi wa nchi..." Nyerere
Maoni yangu ni kwamba siasa siku zote natokana na maslahi ya watu wachache sasa katika ulimwengu wa leo dini+ siasa ndo vitaivuruga democrasia badala ya kuijenga!!
 

My friend Mwita...siasa kuingizwa kwenye utendaji ni kosa kubwa sana sana. JK alichoangalia ni ushkaji, u ccm, uswaiba...bila kijali taaluma. Kuna haja katiba mpya itenganishe hivi vitu.

Hawa jamaa hawatakaa wajitokeze kujibu hoja kwa jinsi unavyotaka. Kinachotakiwa ni mipango ya kichama ktk kushughulikia hili jambo. Tuanze na bungeni...likishindikana tulirudishe kwa wananchi kwa kutumia nguvu nyingi ya pamoja. Haki haiombwi bali inadaiwa.
 
Mkuu hujaji kitu hoja ya lissu ipo wazi vigezo umepewa sasa mbona hujibu hoja.

Lissu katoa vigezo vyake anavyotaka yeye; Raisi anateua majaji kwa mujibu wa katiba inavyomruhusu; sasa yeye Lissu kama haradhiki na uteuzi wa majaji huo ni mpango wake; mpaka sasa hakuna aliyelalamika na maamuzi ya majaji husika na kwa utaratibu wa maamuzi ya mahakama kuu na rufaa ni jopo la majaji ndilo linalotoa maamuzi; Lissu na atueleze ni wapi Raisi amekiuka madaraka yake kuteua hao majaji.
 

Mfano kunajaji hana shahada ya sheria sasauivi ndio anasoma open mkuu nani moja ya vigezo,mwingine ni mgonjwa kateuliwa akiwamgonjwa inamaana Jk hakujua anateua mgonjwa?
 
Mfano kunajaji hana shahada ya sheria sasauivi ndio anasoma open mkuu nani moja ya vigezo,mwingine ni mgonjwa kateuliwa akiwamgonjwa inamaana Jk hakujua anateua mgonjwa?

Je kuna kipengele cha katiba kilichikiukwa? Katiba inasemaje kuhusu mamlaka ya Raisi kwenye kuteua majaji?
 
Hebu fafanua udini umekaa vipi hapo.. yani kuitaka serikali kufanya kazi kwa mujibu wa katiba ni udini.. kweli unakazi. Mwenyewe unakiri kuwa wapo waislamu wenye sifa, sasa kwanini asiwateue hao anakwenda kuteua wenye walakini?
ahsante mchape na bakora kama ataendelea kuandika upuuzi
 
Bado sasa hivi wako busy wanatafuta vyeti vya kughushi katika vyuo vya nje au vya ndani, wanabadilisha miaka ya kumaliza vyuo, wanatafuta kesi kadhaa za kughushi ili ionekane wameshauri na kuamua kesi nyingi tu kwa miaka 10 na wana degree zao...BAADA YA HAPO WATAJITOKEZA KUJIBU HOJA YA TUNDU LISSU, sasa hivi si unawaona hata watuhumiwa wako kimya sana? Ni nani yuko tayari kutuhumiwa hadharani halafu akawa hana hatia na akakaa kimya bila kuleta ushahidi? Mimi wakijitokeza baadae nitajua tu wameshafanikiwa kughushi nyaraka na vyeti! Nitawashauri wafuatilie uhalali wa vielelezo hivyo hadi mwisho kwa uangalifu!
 



Nadhani ni muhimu yatolewe maelezo ya kina kutoka serikalini kwa hawa waliotajwa na Lissu!!!!!!!!!!!
 
Huyo Tindu Lissu ni Mdini tu.Amewalenga waislamu ili awachafue.Christian Democratic Movement in Action. Sio aliyewateua ndio mdini. Hatahivyo kuna waislam wengi wenye sifa zilizotajwa na Mh. Tundu Lissu.
Mkuu pole sana naona kweli umefilisika kimawazo na kiakili. Umebakia kukimbilia kwenye udini na ukabila. Jitahidi kuukumbatia mpaka siku utakapopata akili ya kuelewa na kuchambua mambo
 
Pole sana mheshimiwa ningekuwa ni ww na nina mawazo km yako nadhani ningesimama kusema ndugu wanajf naombeni radhi kwa mawazo yangu maana hayana maana ktk ujenzi wa taifa bali katika maana ya kulibomoa taifa. Nadhani unatakiwa kujiunga na wanywa kahawa magengeni na kutoa hoja kama hizo ndugu yangu maana ukumbuke unaowatolea hoja zako hapa co km ww ulivyo na hduma hii ni kwa manufaa ya wengi hivyo basi lenga katika kutoa hoja za ujenzi wa taifa na c kulibomoa na nikikuuliza unaushahidi na usemayo najua huna hata tone kiasi cha chanjo kwa mtoto. Pole sana.
 
Wapendwa Tanzania inaangamia polepole. JK alishashindwa kuongoza kabisa. Sheria ni mhimili mkubwa sana katika kulitegemeza taifa. Sheria imetoweka. Mahakama imebaki kitendawili na viongozi wa nchi wako kwenye usanii tu wakidhani ni utani. JK nchi bila sheria haitawaliki. Wajukuu zako mwenyewe watajakukata mapanga ukiwa kitandani kwenye nyumba wako. Na ndipo utagundua ni kwa jinsi gani ulivyowaharibia nchi yao ambayo kihistoria ilishawahi kuwa kisiwa cha amani. Tuache kejeli. Hili ni anguko kubwa ktk utawala wa awamu ya nne. Mungu ambariki Lisu kwa kutufahamisha wadanganyika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…