Uchaguzi 2020 Tundu Lissu hana sifa za kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu hana sifa za kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama

Lissu ni mwanasheria wa chama akiwa bungeni lazima maswala ya kisheria au kanuni atayazungumza sana, yeye na jenista mhagama kwa nafasi zao usishangae wakiwa busy kuomba mwongozo na utaratibu, ndo siasa za mfumo wa vyama vingi kwa hiyo usichanganyikiwe
 
Nimsikia Mhe Tundu Lissu akiwa huko Uingereza kuwa akipata ridhaa ya watanzania na chama chake basi atagombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao wa 2020.

Nimekuwa nikumuangalia Mhe Tundu Lissu alipokuwa mwanaharakati na mtetezi wa madhila waliyokuwa wanapata wananchi katika migodi mbalimbali huko kanda ya ziwa na baadaye kuwa mbunge wa Singida.

Akiwa mbunge katika Bunge la Jamhuri amekuwa ni mchangiaji wa mara nyingi sana na muuliza maswali sana na kuomba kuhusu utaratibu na muongozo wa spika mara kwa mara kiasi cha kusababisha hata kutolwa nje na spika pale anapokataa kutii kiti cha spika.

Nakumbuka hata wakati wa Bunge la Katiba hapo ndipo Mhe Lissu alikuwa mkali kama mbogo kwa baadhi ya taratibu alipoona kama vile zina malengo fulani ambayo hayakuwa na faida kwa baadhi ya makundi.

Kwa ujumla ukimuangalia Mhe Lissu na jinsi anavyochangia mada au hoja na maneno anayotumia kwenye public kiukweli sidhani kama anaweza kuwa sahihi kuwa Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama.

Kwa mtazamo wangu mimi kiukweli nidhamu ya Tundu Lissu katika kuchangia mada au hoja kwa wenzake huwa kuna dharau kubwa sana anaonyesha kiasi cha kutoheshimu michango ya wenzake na kama ndivyo alivyo basi kiti cha uraisi sidhani kama ni size yake.
Ila jiwe yuko vizuri eti eh you are insane
 
Makuzi bora ni kuutetea udikteta wa Bashite na baba yake? au makuzi bora ni kutetea ukandamizaji wa demokrasia unaofanywa na Bashite na baba yake? Kama kigezo cha kulelewa vizuri ni kutetea mbinu za kuwapiga Risasi kuwabambikia kesi Wapinzani basi vigezo vyako vitakuwa vimetisha sana.
Tatizo umekremu eti Demokrasia!! Unahitaji kuelewa hakuna Demokrasia Duniani, ukishajua hilo angalua kiongozi anayeweza kujitoa kwa ajili ya nchi na watu wake.Hao wamarekani wanaoimba Demokrasia hata wao wanajikongoja, Embu fikiria Hillari Clinton alipata kula nyingi kuliko Trump, lakini Trump ndio Rais, Na US vyombo vya usalama vinakiri kuwa Russia waliingilia uchaguzi wao, wanashindwa kusema kweli kuwa mfumo uliingiliwa kuogopa aibu. Mark my word TL will never be a President, Never.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi Zitto ni bora zaidi kuliko Lissu ktk uraisi.

Lisu ni mwanaharakati ila Zitto ni mwana mageuzi, he is very visionary,accountable and dedicated.

Natamani coalition ya upinzani imsimamishe Zitto
Msimamishe Zitto kwenu ccm sio mbaya wapambane na TL
 
kama maneno gani?
Sijui ninyi watu wa mkoa wa kagera mna matatizo gani?! Majanga yote ni huku huku kwenu, mara ukimwi, mara matetemeko, tena huku kwenu kuna sehemu inaitwa katerero, na bado kuna mto unaitwa mto ngono. Haya niliyoandika hapa yalitumiwa kama maneno ya kuwafariji wahanga wa tetemeko kule Kagera.
 
U
Hamna namna sasa kama unajua ni Rais iweje mnahangaika kuwabambikia kesi kuwapiga Risasi Wapinzani si mkae mtulie mle trilion 1.5 na 10% kwenye miladi yote mpaka miaka yenu Utawala wa kifalume itapokwisha?
Hauko juu ya sheria sio mwanasiasa wala nani, ukikengeuka utapelekwa mahakamani. Hamna namna lazima mjifunze siasa za kistaraarabu.
 
Sijui ninyi watu wa mkoa wa kagera mna matatizo gani?! Majanga yote ni huku huku kwenu, mara ukimwi, mara matetemeko, tena huku kwenu kuna sehemu inaitwa katerero, na bado kuna mto unaitwa mto ngono. Haya niliyoandika hapa yalitumiwa kama maneno ya kuwafariji wahanga wa tetemeko kule Kagera.
Kuna tofauti ya ukweli in a form of sacarsm na being cocky, lissu is cocky which is not an ingredient of being a president!
Upgrade your brain processor my friend!
 
Ndio maana kuna kura, waache watanzania waamua wenyewe kwa haki na uhuru. Hayo mawazo yako binafsi unaweza kutawasilisha kwenye sanduku la kura na ikatosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi haendeshwi kwa midahalo, wala haiendelei kwa midahalo na media, Angalia US President ana bifu na media karibu kila siku lakini anafanya vizuri katika uongozi, anaangalia maslahi ya nchi yake Kwanza katika kila kitu, na ndivyo anavyofanya Rais wetu mpendwa, Japo sikubaliani naye kwa kila kitu lakini Magufuli is better much better 10000 times kuliko huyo Kibaraka anafikiria kuwa nchi itaendelezwa na wapuuzi Wa nje.

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha ushamba wako kama midahalo haina maana mbona mlimtuma balozi wenu kilaza kwenda kuongea ujinga kujikanyakanyaga? si mgeacha na kuwa kimya? Rais wako mpendwa sio wa wote mnampenda nyie pekee wananufaika wa trilion 1.5 na tenda za kujenga miladi yote ikiwemo chato Airport, kibaraka vipi? Kwani bila nyinyi na Bashite kumpiga Risasi angefikaje huko? 40% ya Bajeti inatolewa na mabeberu ni pesa ambazo mnazifuja nyie CCM ambao sasa mnawasimanga wafadhili wenu baada ya kuwa michepuko wa china, Marekani kuna uhuru wa Habari ndiyo maana Rais ana bifu nao lakini humkuti akiwafanyia udikteta kama jiwe anavyowafanyia watanzania.
 
Kuna tofauti ya ukweli in a form of sacarsm na being cocky, lissu is cocky which is not an ingredient of being a president!
Upgrade your brain processor my friend!
Kwahiyo anayoyaongea Lissu kuhusu kushambuliwa kwake si ya kweli sio! Ila hiyo faraja iliyotolewa huko Kagera ni kweli in a form of Sarcasm. Hivi unawezaje kumfanyia sarcasm mtu aliyepatwa na janga! Kweli ukiwa upande wa pili, ni lazima utetee kila kisichofaa.
 
Kwahiyo anayoyaongea Lissu kuhusu kushambuliwa kwake si ya kweli sio! Ila hiyo faraja iliyotolewa huko Kagera ni kweli in a form of Sarcasm. Hivi unawezaje kumnyia sarcasm mtu aliyepatwa na janga! Kweli ukiwa upande wa pili, ni lazima utetee kila kisichofaa.
Mshauri mkuu wa Jiwe ni Bashite ambaye hana vyeti unategemea nini hapo?
 
Tatizo umekremu eti Demokrasia!! Unahitaji kuelewa hakuna Demokrasia Duniani, ukishajua hilo angalua kiongozi anayeweza kujitoa kwa ajili ya nchi na watu wake.Hao wamarekani wanaoimba Demokrasia hata wao wanajikongoja, Embu fikiria Hillari Clinton alipata kula nyingi kuliko Trump, lakini Trump ndio Rais, Na US vyombo vya usalama vinakiri kuwa Russia waliingilia uchaguzi wao, wanashindwa kusema kweli kuwa mfumo uliingiliwa kuogopa aibu. Mark my word TL will never be a President, Never.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kanye ulale wewe kiaxi. Huwezi badili mpango wa Mungu kama mlivyoshindwa mauaji. Just for the record mark my words. KAMA BWANA MUNGU AISHIVYO TUNDU LISSU NDIYE RAIS WA SITA WA TANZANIA.
 
km huyu aliyepo kaweza kuwa rais nani atashindwa hata KR MULLER,KIMBUNGA na GIGY MONEY wanaweza maaana aliyepo kaweza nani atashindwa
 
Kwahiyo anayoyaongea Lissu kuhusu kushambuliwa kwake si ya kweli sio! Ila hiyo faraja iliyotolewa huko Kagera ni kweli in a form of Sarcasm. Hivi unawezaje kumnyia sarcasm mtu aliyepatwa na janga! Kweli ukiwa upande wa pili, ni lazima utetee kila kisichofaa.
Lissu ni kweli kapigwa risasi ila aliyempiga risasi mpaka leo hajulikani, huu ndio ukweli hivyo kelele zote hizi ni hisia tu ndio maana hata mtangazaji wa bbc alisema those are merely inflamatory allegations. Ni wapi panasema sarcasm hairuhusiwi kwenye janga? Kama haifanyi kazi kwako, kwa wengi inafanya.
 
Kanye ulale wewe kiaxi. Huwezi badili mpango wa Mungu kama mlivyoshindwa mauaji. Just for the record mark my words. KAMA BWANA MUNGU AISHIVYO TUNDU LISSU NDIYE RAIS WA SITA WA TANZANIA.
Labda Tz yote igeuke kuwa ufipa. Hii fantasy ni zaidi ya muvi ya avatar.
 
Back
Top Bottom