Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, huku ni kutafuta wadhamini au ni kampeni?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, huku ni kutafuta wadhamini au ni kampeni?

Kejuu

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2020
Posts
645
Reaction score
906
Ndugu zangu,

Kipekee, napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa uhai siku ya leo.

Mh. Tundu Lissu namfuatilia kwa umakini sana, tangia aanze kuzunguka mikoani kutafuta wadhamini, ni kama vile anafanya kampeni tayari. Japo mimi siyo mwanasheria, ila kwa kumsikia tu, ndugu huyu anafanya kampeni tayari. Na kwa kadri siku zinavyooendelea ndiyo anazidi kujinadi kabisa.

Kwa mfano, alipokuwa Morogoro leo, ameahidi akiingia madarakani ataanzisha : ninamnukuu “a taxper’s bil of right, maana yake nini? Haki ya mlipa kodi”

().​


Kwa mwenendo huu, na tetesi tunazozisikia za ndugu huyu kukatwa kwa sababu ya kuanza kufanya kampeni kabla ya wakati, NEC itakuwa imekosea? Sambamba na hili, nimejiuliza maswali yafuatayo:
  • Kwanini wagombea wengine wanatafuta wadhamini kimya kimya?
  • Je, yawezekana kuna kipengele kinawafanya wagombea hawa watafute wadhamini kimya kimya, ila TL hakijui?
  • Au TL amejifanya much know, akawa na tafisri yake? Yaani mwanasheria nguli katoa boko?
  • Kwanini TL kwa kadri siku zinavyozidi kusongea ndiyo anafanya kampeni kabisa?
  • Au tayari ameshajua kuwa jina lake litakatwa, ndiyo maana ameamua kuanza kufanya kampeni kabisa, yaani, liwalo na liwe?
  • Je, akikatwa Chadema watasusia uchaguzi?
  • Kama wakisusia uchaguzi, vyama vingine navyo vitasusia
  • Kama navyo vitasusia, mwendo utakuwa kama ule wa uchaguzi wa serikali za mtaa?
Kwa tafisri yangu isiyokuwa rasimi, namalizia kwa kusema, kuna asilimia 95% Mh. TL atakatwa kwa sababu anatafuta wadhamini huku akifanya kampeni.

Asanteni,

Nawasilisha

Kejuu
 
Siyo kampeni hiyo bali anafanya siasa.

Na haki ya kufanya siasa ipo kwa mujibu wa katiba.

Haki hiyo ya kufanya siasa na freedom of speech and right to assembly haiondoki kwa ratiba za NEC

Katiba ya nchi imempa mtu haki ya KUCHAGUA na KUCHAGULIWA, na vigezo vya mtu kuchagua au kuchaguliwa vimeelezwa vizuri kwenye katiba.

NEC haina power za kumnyima mwananchi haki ya kisheria ya kuchagua au kuchaguliwa kwa kutumia vikanuni uchwara ambavyo havina uzito wowote juu zaidi ya kikatiba na sheria!
 
Hapo sawa

Kejuu,
Hapo sawa, hajamtukana Magufuli Wala hajasema maneno ya uongo, hajabeba marungu na Bondo kutumia jeshi la Police ndivyo tunataka.
 
Huyu ndo Lissu kama Lissu!!! Umesikia hoja hizo zilivyo zamoto???? Mtamwezea wapi?????

Lazima mvue nguo mwaka huu. Eti Lissu hana hoja, akitema madini mnakimbilia kaanza kampeni. Na bado CCM mtaongea lugha zote mwaka huu!!!! 😀😀😀😀
We jitoe ufahamu, atakatwa yule, amejifanya much know, kawaingiza chaka nguli wa sheria, katoa bonge la boko
 
Hapo sawa

Hapo sawa, hajamtukana Magufuli Wala hajasema maneno ya uongo, hajabeba marungu na Bondo kutumia jeshi la Police ndivyo tunataka
Uzi wangu umeusoma vizuri?
 
3464404B-D34F-431B-A3C3-5427B23F7200.jpeg
CF9558FF-0883-480A-A858-40A7E2CB4406.jpeg

Na Mgombea wenu anavyopost hivi kwenye pages zake za Facebook anafanya nini? Sio kampeni hii?

CCM Mtaongea yote mwaka huu. Itoshe kusema kuwa hoja za Lissu ni zamoto sana kiasi kwamba hamuwezi kuzigusa au kuzijibu bali kuleta ulalamishi tu.

Nimemsikia hadi Majaliwa wenu analia mbele ya wafanyabiashara wenu wa dini mnaowaita viongozi wa dini leo Eti watu wanatafuta huruma.

Mwambie nae atuambie wapo wapi waliompiga risasi Lissu?
 
Back
Top Bottom