Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, huku ni kutafuta wadhamini au ni kampeni?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, huku ni kutafuta wadhamini au ni kampeni?

Ndugu zangu,

Kipekee, napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa uhai siku ya leo.

Mh. Tundu Lissu namfuatilia kwa umakini sana, tangia aanze kuzunguka mikoani kutafuta wadhamini, ni kama vile anafanya kampeni tayari. Japo mimi siyo mwanasheria, ila kwa kumsikia tu, ndugu huyu anafanya kampeni tayari. Na kwa kadri siku zinavyooendelea ndiyo anazidi kujinadi kabisa.

Kwa mfano, alipokuwa Morogoro leo, ameahidi akiingia madarakani ataanzisha : ninamnukuu “a taxper’s bil of right, maana yake nini? Haki ya mlipa kodi”

().​


Kwa mwenendo huu, na tetesi tunazozisikia za ndugu huyu kukatwa kwa sababu ya kuanza kufanya kampeni kabla ya wakati, NEC itakuwa imekosea? Sambamba na hili, nimejiuliza maswali yafuatayo:
  • Kwanini wagombea wengine wanatafuta wadhamini kimya kimya?
  • Je, yawezekana kuna kipengele kinawafanya wagombea hawa watafute wadhamini kimya kimya, ila TL hakijui?
  • Au TL amejifanya much know, akawa na tafisri yake? Yaani mwanasheria nguli katoa boko?
  • Kwanini TL kwa kadri siku zinavyozidi kusongea ndiyo anafanya kampeni kabisa?
  • Au tayari ameshajua kuwa jina lake litakatwa, ndiyo maana ameamua kuanza kufanya kampeni kabisa, yaani, liwalo na liwe?
  • Je, akikatwa Chadema watasusia uchaguzi?
  • Kama wakisusia uchaguzi, vyama vingine navyo vitasusia
  • Kama navyo vitasusia, mwendo utakuwa kama ule wa uchaguzi wa serikali za mtaa?
Kwa tafisri yangu isiyokuwa rasimi, namalizia kwa kusema, kuna asilimia 95% Mh. TL atakatwa kwa sababu anatafuta wadhamini huku akifanya kampeni.

Asanteni,

Nawasilisha

Kejuu

Mwache akatwe ameyataka mwenyewe!
 
Lissu anapita barabarani toka mkoa mmoja kwenda mwingine, huko njiani anakutana na watu wenye shauku ya kumuona, anawasalimia, sasa wewe ulitaka apande ungo au afanyeje?!
Sheria na mwongozo wa NEC unasemaje wakati wa kutafuta wadhamini?
 
Ndugu zangu,

Kipekee, napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa uhai siku ya leo.

Mh. Tundu Lissu namfuatilia kwa umakini sana, tangia aanze kuzunguka mikoani kutafuta wadhamini, ni kama vile anafanya kampeni tayari. Japo mimi siyo mwanasheria, ila kwa kumsikia tu, ndugu huyu anafanya kampeni tayari. Na kwa kadri siku zinavyooendelea ndiyo anazidi kujinadi kabisa.

Kwa mfano, alipokuwa Morogoro leo, ameahidi akiingia madarakani ataanzisha : ninamnukuu “a taxper’s bil of right, maana yake nini? Haki ya mlipa kodi”

().​


Kwa mwenendo huu, na tetesi tunazozisikia za ndugu huyu kukatwa kwa sababu ya kuanza kufanya kampeni kabla ya wakati, NEC itakuwa imekosea? Sambamba na hili, nimejiuliza maswali yafuatayo:
  • Kwanini wagombea wengine wanatafuta wadhamini kimya kimya?
  • Je, yawezekana kuna kipengele kinawafanya wagombea hawa watafute wadhamini kimya kimya, ila TL hakijui?
  • Au TL amejifanya much know, akawa na tafisri yake? Yaani mwanasheria nguli katoa boko?
  • Kwanini TL kwa kadri siku zinavyozidi kusongea ndiyo anafanya kampeni kabisa?
  • Au tayari ameshajua kuwa jina lake litakatwa, ndiyo maana ameamua kuanza kufanya kampeni kabisa, yaani, liwalo na liwe?
  • Je, akikatwa Chadema watasusia uchaguzi?
  • Kama wakisusia uchaguzi, vyama vingine navyo vitasusia
  • Kama navyo vitasusia, mwendo utakuwa kama ule wa uchaguzi wa serikali za mtaa?
Kwa tafisri yangu isiyokuwa rasimi, namalizia kwa kusema, kuna asilimia 95% Mh. TL atakatwa kwa sababu anatafuta wadhamini huku akifanya kampeni.

Asanteni,

Nawasilisha

Kejuu

HIVI HUWAGA HUNA HOJA ZINGINE ZAIDI YA TUNDU LISSU, MBONA TL ANAWAFANYA MNAZIDI KUWEWESEKA.
 
Back
Top Bottom