Mwanasiasa machachari wa Tanzania anayeishi mamtoni baaada ya kufanyiwa unyama amekanusha taarifa na kauli ya Igp Sirro kuwa alipigiwa simu na jeshi la polisi ili ahojiwe juu ya madhila yaliyompata.
Kupitia ukurasa wake wa Twita Lissu amedai kuwa taarifa hizo ni za uongo na hazina ukweli wowote.
3) Polisi hawajahoji mtu yeyote wala kutoa taarifa yoyote juu ya uchunguzi wao, zaidi ya kudai wahusika ni watu wasiojulikana na hakuna hata mtu wanayemshuku.
4) Polisi walisema wana footage ya CCTV camera iliyokuwa kwenye jengo nilikoshambuliwa. Hadi leo wako kimya juu ya hilo.
5) Polisi hawajawahi kusema ni nani aliyeondoa walinzi wote kwenye makazi ya viongozi wa serikali ili kuwaruhusu wauaji waingie ndani na kunishambulia kwa risasi.
6) Nilisema hadharani kwamba nilikuwa nafuatiliwa kwa gari na watu waliotumwa na IGP Sirro na Mkuu wa TISS Kipilimba.
Niliwataja IGP Sirro na DG-TISS Kipilimba specifically na kuwataka waingilie kati, na nilitaja gari iliyokuwainanifuata fuata. Majibu yalitolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba aliyepuuza taarifa yangu na kudai gari iliyokuwa inanifuata fuata iko Arusha, sio Dar.
Baada ya shambulio, Jeshi la Polisi lilifanya jitihada kubwa kuzuia wananchi kunipa msaada wowote. Waliojaribu kuniombea makanisani na misikitini walipigwa marufuku. Waliojaribu kujitolea damu walikatazwa. Waliovaa Tshirt zenye picha yangu walikamatwa na kuwekwa mahabusu.
6) Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, chini ya Mwenyekiti wake Balozi Adadi Rajabu (DCI mstaafu), ilifanya uchunguzi wa shambulio dhidi yangu na kuandaa taarifa rasmi. Taarifa hiyo ilizimwa na uongozi wa Bunge masaa machache kabla ya kuwasilishwa rasmi bungeni. Kwa nini?
7) Nilinyimwa haki ya kutibiwa kwa fedha za Bunge kama sheria inavyotaka. Baadae Katibu wa Bunge aliniandikia barua kwamba Rais Magufuli hakutoa idhini ya matibabu hayo.
8) Ni Magufuli aliyesema, saa 2 kabla sijashambuliwa, kuwa wanaopinga vita yake ya uchumi hawastahili kuishi!
9) Mwaka jana nilienda Polisi Dodoma kudai gari yangu ambayo iko polisi tangu niliposhambuliwa. Jibu la RPC Muroto lilikuwa sitapewa gari yangu mpaka nitakapohojiwa juu ya shambulio. Lakini polisi hawakuwa na interest ya kunihoji zaidi ya kupiga mabomu mikutano yangu ya hadhara.
10) Nilikimbia nchi baada ya kupata taarifa kuwa Rais Magufuli alikuwa ametoa amri kwa 'watu wasiojulikana' kuwa niuawe mara baada ya uchaguzi. Nilikamatiwa na polisi wa IGP Sirro nje ya Ubalozi wa Ujerumani na isingekuwa wanadiplomasia wa Kijerumani kuingilia kati ningepotezwa.
IGP Sirro anasema sistahili kupewa ulinzi wowote kwa sababu mimi ni Mtanzania sawa na Watanzania wengine. Lakini sio Watanzania wote waliowahi kushambuliwa kwa risasi 16 wala kutendewa kama nilivyotendewa mimi. Majibu yake ni utetezi wa wauaji wasiojulikana na wale waliowatuma!
... ni hatari sana kwa vyombo vya dola kujiingiza kwenye siasa za majitaka. Taratibu za kipolisi mhusika anapelekewa samansi/hati ya wito na sio kupigiwa simu. Huyu IGP anakosa kuaminika.
..Waziri wa mambo ya ndani, wakati huo Mwigulu Nchemba, alisema kwamba gari yenye namba ambazo Tundu Lissu alidai inamfuatilia ilionekana Arusha.
..Na waziri wa mambo ya ndani akadai kwamba wamewahoji wahusika na wamejiridhisha kwamba gari hiyo haikuwahi kufika D'Salaam.
..IGP Sirro anadai Lissu hakuwahi kutoa taarifa kituo cha polisi kuhusu kufuatiliwa. Vilevile IGP anadai polisi hawana taarifa zozote kuhusu Lissu kufuatiliwa na " watu wasiojulikana. "
..Sasa katika mazingira kama hayo tumuamini nani? Je, Waziri wa mambo ya ndani alidanganya? Je, IGP anadanganya?
Kitendo cha yule Mama kuendelea kumtumia huyu mzee kama IGP nikapoteza imani naye kabisa.
Alipaswa awekwe pembeni maana uovu mwingi Wa Polisi enzi za jiwe hakuna namna hili zee linakwepa lawama.
Isitoshe hoja zake kuhusu shambulio la Lissu ni za kipuuzi sana. Lissu alivyorudi Tanzania alikwenda Polisi kufuatilia gari lake. Mbona hawakumwomba nafasi wamuhoji juu ya shambulio lililopelekea gari lake kuwa mikononi mwao?
IGP alivuka hadhi ya nafasi yake. Angeishia kusema alimpigia Lissu simu hakwenda wenye akili wangemwelewa lakini alipoongeza kwamba Lissu anafurahia/anatumia hali aliyonayo kujipatia fedha, hata wasio na akili wakaona IGP ni ndugu yao.
Mwanasiasa machachari wa Tanzania anayeishi mamtoni baaada ya kufanyiwa unyama amekanusha taarifa na kauli ya Igp Sirro kuwa alipigiwa simu na jeshi la polisi ili ahojiwe juu ya madhila yaliyompata...
Nimeanza kupata mashaka na hii issue ya Tundu Lissu iweje CHADEMA wako kimya juu ya kuishinikiza serikali kuanzisha uchunguzi huru?..iweje wanaharakati wa tweeter hawaweki pressure kwa serikali ili ukweli ueleweke na haki ipatikane?....Au tunaisubiri serikali yenyewe iamue kufanya uchunguzi?
Nilitegemea mambo mazito yalitoikuta CHADEMA kama watu kupotea, kufa na kushambuliwa wanachama na wapenzi wahamasishwe umma ujue ukweli na hatua zichukuliwe kwa wahusika..Sioni harakati zozote zaidi ya mchezo wa paka na Panya CHADEMA na Serikali....kuna vilivyojificha bila shaka..