Uchaguzi 2020 Tundu Lissu, ilani yako na CHADEMA itahitaji msaada zaidi ya asilimia 90, tutarudi utumwani

Kodi rafiki ni zipi na kandamizi ni zipi?

Atatumia mbinu gani kufidia nakisi ya bajeti kutokana kuondoa baadhi ya kodi?
Hatokusanya Kodi kandamizi bali atakusanya kodi rafiki kutoka kwa wafanyabiashara .Acheni kupotosha.
 
Ukweli ndo huo subiria mvua ya matusi na kejeri.
Hakuna cha mvua ya matusi wala nini. Hoja zake zitajibiwa kwa hoja. Mpaka sasa tunakopa, huu mradi wa elimu wa SEQUIP (Secodary Education Quality Improvement Project) tumekopeshwa pesa na Woeld Bank kuboresha elimu. Reli ya SGR ni mkopo wa Waturuki, hata kama tunaaminishwa kwamba ni pesa za ndani. Kiufupi hakuna nchi inayoendelea isiyokopa. Kwa nchi kama Tanzania ambayo vyanzo vyake vya mapato ya ndani ni very limited, kiasi kwamba hatuwezi ku finance bajeti yetu, ni lazima tukope ili tuendeshe miradi ya maendeleo. Leteni hoja zingine
 
Kwa sababu aliahidi kwenye ilani na ni lazima atekeleze, lazima tulifufue shirika letu la ndege, vinginevyo miaka mitano ilopita mlikuwa mkituhadaa maana mliahidi hayahaya anayoyafanya JPM, anaangalia mbali, zitatufaa sana wakati utakapofika, akiondoka hayupo ataefanya, kupanga ni kuchagua, anakusanya kodi ndo maana kaweza kufanya hayo, nyie hiyo mishahara mtailipa vipi bila kodi? fidia mnazowadanganya mtawalipa vipi bila kodi? mnataka kudangisha Taifa baada ya nyie kukubuhu? hatutakubari.
 
Alisema atapunguza utitiri wa Kodi zilizopo na kungenezaazingira rafiki ya uwekezaji ambapo Kama uwekezaji utaongezeka kwa kupunguza utitiri wa Kodi na kuweka ma,ingira wezeshi ya biashara mapato ya serikali yataongezeka na ajira zitaongezeka pia na wafanyakazi watalupa Kodi.
 
Mmachinga analipa kodi ya shilingi 20,000 kwa mwaka hana tozo lingine.

Japo Tundu kaleta upotishaji kuwa wamachinga wanalipishwa kodi wakati wafanyabiashara wenye TIN hawalipi.Kumbuka TIN ni kama akaunti yako ambayo mtiririko wa makadirio na malipo ya kodi kuwekwa. Tundu anataka watu waamini kuwa wamachinga wanalipa kodi kubwa kuliko wenye TIN,sio kweli
..wamachinga wana kipato kidogo sana hawatakiwi kutozwa kodi ya vitambulisho.
 
Ujinga wa ccm wanafikiri lisu akiwa rais ndege, madaraja. Viwanda Barbara, Tiss TRA, na rasilimali nyingine za nchi zitabaki kuwa Mali ya ccm Na magufuri ndio maana wanaona ni vigumu kwa lisu kutekeleza ilani ya chadema,

Lisu akichukuwa nchi hivyo nilivyovitaja ni mali za wananchi hivyo ndivyo atakavyovitumia lisu kuleta maendeleo ya kweli, nyie mtaondoka na mabegi yenu tu hapo ikulu.

Na tausi wetu tutawarudisha maana mnagawagawa hovyo rasilimali za nchi
 
Kwani hizi kodi wakati wa JK zilikuwepo?Na mapato ya hizi fedha yanaeleweka yanapokwenda?
Nenda kaangalie maendeleo ya Mwl Nyerere HEP, nenda katizame SGR, hayo mahospitali ya wilaya zote nchini, vipi vituo vya afya na zahanati hujaziona? bila kodi haya yote usingeyaona na ndo maana hukuyaona hata wakati wa JK, JPM ndani ya miaka mitano kajenga Hospitals mala mbili ya hospitali zote zilizojengwa tangu tupate uhuru.
 

..wewe makuzi yako ya kiuchumi ni ktk falsafa ya kuongeza makusanyo/ mapato kwa kutoza kodi kubwa.

..falsafa ya kikodi ya TL na serikali yake ni kuongeza makusanyo kwa kuwa na viwango vya kodi vinavyolipika, na vinavyovutia wawekezaji wengi zaidi.

..hapa tulipo tunapoteza nafasi ya kuwa na makusanyo makubwa zaidi, kwa hiyo achana na imani kwamba mapato yatapungua.
 
Naam ni mkopo ndio lakini tunarejesha kwa kupitia kodi zetu.Tunakopa kuboresha miundombinu ili kuboresha maendeleo ya watu kisha tunalipa kidogo kidogo kwa kodi kamanda.

Nikupe elimu kidogo, hata hiyo mikopo serikali hupewa shari la kuweka "equity contribution" ya hadi asilimia 40 ya gharama ya mradi
 
Wakudadavua na ccm yake pumbavu sana

Waliwahi kusema Elimu bure haiwezekani enzi za wilbroad slaa

Finally sasa hivi wanafanya kile walisema na kuwaaminisha watanzania hakiwezekani
 
Jenga hoja acha kubwabwaja
 
Kuhusu fidia ni kweli watu wa maeneo ya kimara mpk mbezi walishinda kesi na kulikuwa na zuio la mahakama kubomolewa eneo Hilo mpaka walipqe fidia. Hapo hoja ni kwamba kipindi Cha serikali ya awamu ya tano watu wamebomolewa kwa kisasi na kubomolewa maaana huyo huyo rais alipokuwa mwanza alisema watu wasibomolewe kwa kuwa wamempa kura
 
Jenga hoja acha kubwabwaja na kulialia
Wakudadavua na ccm yake pumbavu sana

Waliwahi kusema Elimu bure haiwezekani enzi za wilbroad slaa

Finally sasa hivi wanafanya kile walisema na kuwaaminisha watanzania hakiwezekani
 
..wamachinga wana kipato kidogo sana hawatakiwi kutozwa kodi ya vitambulisho.
Mtaji wa milioni nne!? kiasi kidogo!? Au silielewi vizuri suala la vitambulisho vya wamachinga alivyotoa Mheshimiwa rais!
 
Kuhusu la mfuko wa mikopo ya elimu ya just majibu ni rahisi sana. Wanafunzi waliingia makubaliano ya kimkataba na serikali kulipa 3% Sasa serikali epuuza makubaliano hayo na kuarise mpka 8% na baadae kubadioi mpk 15%. Tuliosoma na kutumia mikopo hiyo tunafahamu mikataba hiyo na adha tunapata kulipa hiyo hell kwa kiwango hicho kinyume na makubaliano.
Lissu ametanabaisha atarejesha kiwango stahiki kulingana na mikataba. Mbona uelewa madogo tu huo
 

..they should not be charged kupata hivyo vitambulisho.

..wamachinga mitaji yao ni midogo, na biashara yao ni ngumu mno hawatakiwa kubugudhiwa na kutozwa fedha ambazo haijulikani zinakwenda wapi.

..tunatakiwa tufikirie namna ya kuongeza ajira za kudumu ili wamachinga wapungue, na siyo kuwaza namna ya kuwakamua kipato chao kidogo.
 
Joka,hili la wamachinga kutozwa au kutotozwa linahoja lakini muda mwingine mtu akilipia Kodi inampa haki ya kudai huduma bora zaidi hususani kutoka serikalini
 
Loud and clear
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…