Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Kamati Kuu itakaa kutoa msimamo rasmi juu ya Mbunge wa Nkasi, Aida Khenan

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Kamati Kuu itakaa kutoa msimamo rasmi juu ya Mbunge wa Nkasi, Aida Khenan

Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
Usione huruma chadema
Ccm mumeshinda kwa kishindo
Kajengeni arusha iwe carlifonia
 
Aida Khenan mbunge mteule wa Nkasi amesema, yeye ni mbunge pekee aliyetangazwa na katika mkoa wake amepata madiwani 10.

Lakini amesema amesikia kwenye mitandao kuhusu msimamo wa chama chake lakini yeye hajapewa taarifa rasmi eidha ya simu au barua, anadai anaamini chama chake ni taasisi kubwa hivyo anategemea atapewa taarifa rasmi.

Amesema jimboni kwake na mkoani kwake mpaka sasa kuna taharuki kubwa, wananchi wana taharuki kubwa.

Amesema mpaka sasa ametishiwa maisha na wananchi kwa kuwa wao waliamua kuvunja rekodi ya kutoa Mbunge mwanamke kwa mara ya kwanza hivyo wanadai yeye akifuata msimamo wa chama atakuwa kawasaliti wananchi ambao wapo walioumia ili yeye ashinde, pia amesema kuna kesi kama 18 za watu waliokamatwa walipokuwa wanapigania yeye ashinde.

Amedai wananchi wanamwambia kuwa machozi yao hayawezi kwenda bure asipokwenda kuwatumikia bora maisha yake wananchi wayamalize hapo.

Amedai kuwa anaomba chama chake warudie upya kutazama maamuzi yao, na kama waliyatoa kwa jazba kulingana na yaliyotekea kwenye uchaguzi basi waangalie upya na waelewe kuwa yeye hana amani anatishiwa maisha na amedai hawezi kuhama Rukwa na hawezi kuhama Nkasi.

Amedai kuwa kwa mara ya kwanza kwenye jimbo lao wamepata Mbunge mwanamke na Mbunge wa kutoka upinzani hivyo asipokwenda kuwawakilisha wananchi madhara yake ni makubwa sana kwake aidha hata kama viongozi wake hawatayaona.

Amesema alisharipoti Polisi kuhusu kutishiwa maisha na pia msimamo huo si wake peke yake bali ni wake na viongozi wa mkoa wa chama cha CHADEMA.

Amesema katika ngazi ya taifa hakuna kiongozi yeyote aliyemtafuta hata kwa simu aweze kujua amani yake au usalama wake.

Amedai kuwa alipoomba nafasi ya Ubunge aliomba peke yake na wala hawakuomba 2 wala 3 hivyo atakwenda bungeni kama yeye Aida na atakwenda kuwasilisha sauti yake yeye peke yake kwa niaba ya wananchi wa Nkasi japo atakuwa mpweke ndani ya bunge. Anasema alipokuwa mbunge wa viti maalum alijifunza kutoka kwa wabunge waliomtangulia lakini kama wabunge wa Viti Maalum watakwenda kipindi hiki atapata faraja lakini wasipokwenda itakuwa mpweke lakini faraja atapata kwa wananchi waliomchagua anaowawakilisha.

Tundu Lissu nae anena haya
Tundu Lissu anena kuwa, keshokutwa watakaa kamati kuu na ndio itatoa msimamo wa jumla wa chama, msimamo ambao waliusema wiki iliopita ni msimamo wa viongozi wakuu wa chama, lakini lazima kamati kuu itoe baraka zake au ikatae kutoa baraka zake.

Tundu Lissu amedai kuwa wao hawakua na wajibu wa kuuliza yeye Aida anafikiriaje kwa kuwa wao viongozi wakuu wana majukumu mengine ndani ya chama, amedai kuwa wao walitoa msimamo wao kuwa huo haukuwa uchaguzi.

Amedai kuwa kama chama kikisema kuwa huo ndio msimamo wa chama basi itabidi atafute utaratibu mwingine wa kuwatumikia wananchi wa Nkasi kwa kuwa Tanzania hakuna mbunge binafsi bali ni wabunge wa chama hivyo wabunge ni lazima wafuate utaratibu wa chama.

Usikute mbowe na Lissu hawajampa hongera dada
 
Aaweza kwenda bungeni under protest huku akiwa na msimamo wa chama chake bungeni.
Hii ya kupiga picha na bashiru au kwenda Dodoma kuspishwa Magufuli au kusema aliomba ubunge peke yake inaonekana wazi hajitambui na hana msimamo au kanunuliwa tayari au hio nafasi alipewa tu kwa malengo maalum ya ccm
 
Mbona 2015 mlisema pia mmeibiwa kwenye Urais?
Kwanini akina mbowe na lisu walienda bungeni?
Kwanini wasisuse ili kuonyesha msimamo??
Kumbe umejua kwamba na wao wapo kinaslahi eeh??
Yaani wao ni waroho wa hizo posho ila wanataka mwenzao asiende kisa wao wameshindwa.

Huu ni ujinga sana
Mkuu mbona unashindwa kujiongeza kidogo? Wizi wa kura mwaka huu haujawahi kushuhudiwa kokote ulimwenguni yaani walifanya wizi wa kitoto mno bora wangefanya wa kisayansi afadhali.

Mwaka huu naamini mwana ccm halisi amejisikia aibu sana kwa kilichotokea ingawaje hawezi kusema hadharani.
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
Naona buku7 wa Lumumba mnakiri waziwazi kwamba CCM ni wezi wa kura!
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
jamaa wananishangaza sana. Wanasema wanataka democrasia lkn kwanin hawatak kumpa mtu nafas ya kufanya maamuzi yake. Wanatak ku dictate kile wanachokiwaza wao ndio kiwe hiko. Muda huo wenye nguvu zaidi yao wakifanya hivo, wanaandamana.

Siasa ni uhun
 
Mkuu mbona unashindwa kujiongeza kidogo? Wizi wa kura mwaka huu haujawahi kushuhudiwa kokote ulimwenguni yaani walifanya wizi wa kitoto mno bora wangefanya wa kisayansi afadhali.

Mwaka huu naamini mwana ccm halisi amejisikia aibu sana kwa kilichotokea ingawaje hawezi kusema hadharani.
Mbona hujajibu maswali yangu sasa?
 
Mbona hujajibu maswali yangu sasa?
Hawez kujibu , mtu amepata kura million 1 dhidi ya Mili 12 , hata kama umeibiwa ndo kura mil 11, mi niliwaambia kama walikuwa na mawakala , wachukue taarifa za mawakala wao watiifu toka kwenye vituo na watumie kama sample tuone kama Lissu alishinda.....
Mtu mwenyewe kwenye vituo kibao Tu kapata kura 0 alaf mijitu inaropoka ooh tumeibiwa
 
Lengo lao limekamilika wameachia jimbo moja ili kuleta haya yanayotokea sasa.
Naungana na wewe katika mengi lakini kwa hili nakukatalia. AIDA hakupewa ili kubalance game, CCM walitaka kusiwe na Mbunge hata mmoja wa upinzani, ila mbinu za wizi zilizotumika maeneo mengine kama vile vijana wa CCM kuingia na kura mifukoni zilidhibitiwa na vijana wa CDM Nkasi.

Fomu fake za matokeo zilikamatwa kwenye vituo vya majumuisho. Kule Mkuu wa wilaya aliingia kila Kituo lakini alifukuzwa na mawakala ambao waliwekwa kila Kituo, hakukuwa na Kituo kisichokuwa na Wakala wa CDM. Huko kuna Kituo Magufuli kapata kura 13 dhidi ya 200+ za Lissu. Huyu binti wamuache tu, aliwapanga vizuri watu wake na wlimtii na kufanya yanayostahili.
 
Hawez kujibu , mtu amepata kura million 1 dhidi ya Mili 12 , hata kama umeibiwa ndo kura mil 11, mi niliwaambia kama walikuwa na mawakala , wachukue taarifa za mawakala wao watiifu toka kwenye vituo na watumie kama sample tuone kama Lissu alishinda.....
Mtu mwenyewe kwenye vituo kibao Tu kapata kura 0 alaf mijitu inaropoka ooh tumeibiwa
Mimi kuna ndugu yangu alisimamia huo uchaguzi na ni mwanachadema kindakindaki.
Nilimuuliza kuhusu hizi tuhuma za wizi alisema kura zimehesabiwa kihalali kabisa na ameyasimamia hayo mabox Hadi yamefikishwa mahali husika.. Anasema labda km sehemu nyingine wamefanya hivyo lakini alipokuwapo yeye mawakala wote walikuwepo.

Anasema upinzani tukubali kuwa safari hii tumedondoka.
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
Kweli aisee wanayumba ni kuwanyima haki wananchi wa nkasi
 
Aida Khenan mbunge mteule wa Nkasi amesema, yeye ni mbunge pekee aliyetangazwa na katika mkoa wake amepata madiwani 10.

Lakini amesema amesikia kwenye mitandao kuhusu msimamo wa chama chake lakini yeye hajapewa taarifa rasmi eidha ya simu au barua, anadai anaamini chama chake ni taasisi kubwa hivyo anategemea atapewa taarifa rasmi.

Amesema jimboni kwake na mkoani kwake mpaka sasa kuna taharuki kubwa, wananchi wana taharuki kubwa.

Amesema mpaka sasa ametishiwa maisha na wananchi kwa kuwa wao waliamua kuvunja rekodi ya kutoa Mbunge mwanamke kwa mara ya kwanza hivyo wanadai yeye akifuata msimamo wa chama atakuwa kawasaliti wananchi ambao wapo walioumia ili yeye ashinde, pia amesema kuna kesi kama 18 za watu waliokamatwa walipokuwa wanapigania yeye ashinde.

Amedai wananchi wanamwambia kuwa machozi yao hayawezi kwenda bure asipokwenda kuwatumikia bora maisha yake wananchi wayamalize hapo.

Amedai kuwa anaomba chama chake warudie upya kutazama maamuzi yao, na kama waliyatoa kwa jazba kulingana na yaliyotekea kwenye uchaguzi basi waangalie upya na waelewe kuwa yeye hana amani anatishiwa maisha na amedai hawezi kuhama Rukwa na hawezi kuhama Nkasi.

Amedai kuwa kwa mara ya kwanza kwenye jimbo lao wamepata Mbunge mwanamke na Mbunge wa kutoka upinzani hivyo asipokwenda kuwawakilisha wananchi madhara yake ni makubwa sana kwake aidha hata kama viongozi wake hawatayaona.

Amesema alisharipoti Polisi kuhusu kutishiwa maisha na pia msimamo huo si wake peke yake bali ni wake na viongozi wa mkoa wa chama cha CHADEMA.

Amesema katika ngazi ya taifa hakuna kiongozi yeyote aliyemtafuta hata kwa simu aweze kujua amani yake au usalama wake.

Amedai kuwa alipoomba nafasi ya Ubunge aliomba peke yake na wala hawakuomba 2 wala 3 hivyo atakwenda bungeni kama yeye Aida na atakwenda kuwasilisha sauti yake yeye peke yake kwa niaba ya wananchi wa Nkasi japo atakuwa mpweke ndani ya bunge. Anasema alipokuwa mbunge wa viti maalum alijifunza kutoka kwa wabunge waliomtangulia lakini kama wabunge wa Viti Maalum watakwenda kipindi hiki atapata faraja lakini wasipokwenda itakuwa mpweke lakini faraja atapata kwa wananchi waliomchagua anaowawakilisha.

Tundu Lissu nae anena haya
Tundu Lissu anena kuwa, keshokutwa watakaa kamati kuu na ndio itatoa msimamo wa jumla wa chama, msimamo ambao waliusema wiki iliopita ni msimamo wa viongozi wakuu wa chama, lakini lazima kamati kuu itoe baraka zake au ikatae kutoa baraka zake.

Tundu Lissu amedai kuwa wao hawakua na wajibu wa kuuliza yeye Aida anafikiriaje kwa kuwa wao viongozi wakuu wana majukumu mengine ndani ya chama, amedai kuwa wao walitoa msimamo wao kuwa huo haukuwa uchaguzi.

Amedai kuwa kama chama kikisema kuwa huo ndio msimamo wa chama basi itabidi atafute utaratibu mwingine wa kuwatumikia wananchi wa Nkasi kwa kuwa Tanzania hakuna mbunge binafsi bali ni wabunge wa chama hivyo wabunge ni lazima wafuate utaratibu wa chama.
Chadema wanakuwa wajinga kila kuchwao, na hawataki kujifunza,akili yao ni akili ya Mbowe,wekeni vikwazo kwa huyu mdada nae ataenda CCM kwa raha zake na kurudi tena mjengoni. Huyu dada hata akienda chama cha mzee wa ubwabwa atapata kura kibao na kushinda tena.Endelea kujishau tu wakati munalala kwa balozi wa Ujerumani,utadhani hamna makwenu.
 
Nusara itumike .
Huyo dada aachwe mana amefanya kile alichotumwa na chama chake.
Hivi kwa mfano Mdee angeshindaje wakati alikua anaongea bangi majukwaani badala ya mikakati na mipango mizuri ya maendeo?

Hivi Lema angeshinda kwa hoja ipi aliyokuwa nayo?

Kama yupo mbunge wa Upinzani alieshinda na hakutangazwa sheria iko wazi aende Mahakamani?
Hawana ushahidi wowote wa kisayansi japo kweli kura zilipigwa kihuni .
Mdee msomi wa sheria mzima anakamata kielelezo cha kura feki halafu kwa bangi zake kichwani anazichoma moto kupoteza ushahidi tena kumsaidia mtuhumiwa asipatikane na hatia.

Sasa kama unakua na wagombea ubunge hopeless kama Mdee unategemea usiibiwe na wasanii kama Gwajima wanaofanya mazingaumbwe na kuwadanganya waumini kuwa wamefufua wafu kisha kukusanya mabilioni ya pesa ? Utamshindaje Mtu mdanganyifu kama Gwajima anayemdanganya mpaka Mungu na kuwaibia watu kwa ridhaa yao?

Wapinzani acheni kurushiana maneno kwenye mitandao na badala yake kusanyeni ushahidi mlio nao upelekeni hata mahakama ya kimataifa kisha mpeleke kwenye nchi wahisani ili wao waone kama kuna wanaloweza kulisemea au kuliwekea vikwazo.

Vinginvyo kama hamna ushahidi basi kaeni kimya uchaguzi umeisha . Aliyetangazwa ndiye aliyeshinda mana hana pingamizi la kisheria.

Kumfukuza Uanachama kutaleta mjadala mkubwa sana na kuwakatisha tamaa wananchi na wapiga kura wote wanaolinda kura na kuhakikisha ushindi unapatikana. Awe ni mfano wa namna ya kulinda kura.

Aachwe atakuja kujichanganya mwenyewe huko mbeleni na kujikuta anajawa na kiburi wakati huo wananchi watakua wameshasahau na jazba zao kupoa hapo ndipo atatimuliwa bila kupepesa macho.

Kwa sasa aachwe awe ni mbunge aliyepingana na maelekezo ya chama kidemokrasia.
Mkimfukuza mtawatoa wananchi kwenye Reli ya uchaguzi haramu badala yake waramjadili mtu mmoja kuwa ameonewa. Watu watamuunga mkono kuwa ameonewa na chama chake na sio tume.
 
Imagine scenario hii:

Aida ang’ang’anie kuingia Bungeni, CHADEMA wamfukuze uanachama, Aida ahamie CCM,
Uchaguzi mpya uitishwe na CCM wamsimamishe Aida.

CHADEMA wagome kushiriki uchaguzi kwa kuwa hawana imani na Tume, Aida apite bila kupingwa then arudi Bungeni kwa kishindo.

Tutakuwa tumeachieve nini?
 
Back
Top Bottom