Tundu Lissu: Kufuta kesi ya Mbowe sio kuingilia Uhuru wa Mahakama

Tundu Lissu: Kufuta kesi ya Mbowe sio kuingilia Uhuru wa Mahakama

Makamu Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA nchini Tanzania Tundu Lissu anayeishi uhamishoni Ubelgiji ameeleza azma yake ya kurudi nchini Tanzania wakati wowote.

Lissu alisema hayo katika mahojiano maalum na VOA baada ya kukutana na rais wa Tanzania Samia suluhu mjini Brussels Jumanne.

Akizungumzia dai lake la kutaka kesi ya mwenyekiti wa chama cha Chadema Freeman Mbowe ifutwe, Lissu amesema jambo hilo sio kuingilia uhuru wa Mahakama na kwamba kesi hiyo “haina maslahi yoyote na afanye kama alivyofanya kuhusiana na kesi ya mashekhe wa Uamsho wa Zanzibar ambao walifutiwa mashitaka baada ya kukaa gerezani miaka 9 hakuna cha kuingilia mhimili wowote hapa”

Akisisitiza kwamba hajamwambia Rais aongee na Jaji bali mwendesha mashitaka ambaye ni mteule wa Rais na anafanya kazi kama sehemu ya utawala sio sehemu ya Mahakama.

Pia kiongozi huyo wa upinzani na mgombea Urais mwaka 2020 amemwambia Rais kuhusu suala la Serikali kutaka kuwafukuza kwa nguvu wananchi wa wilaya ya Ngorongoro kutoka eneo la mamlaka ya hifadhi kuwa ni jambo la hatari na linaweza kuchafua nchi na akasema Rais amemwambia amelizuia.

Lissu pia amegusia Uhuru wa vyama vya siasa kufanya kazi akisema amemweleza Rais Samia kuhusu zuio aliloliita haramu la vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara na maandamano na madai ya hitaji la katiba mpya nchini humo na mfumo mpya wa uchaguzi.

Itakumbukuwa mbunge huyo wa zamani na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2020 alinusurika katika shambulizi baya la risasi na watu wasiojulikana mwaka 2017 na amemtaka rais ahakikishe anatendewa haki kwa mambo ambayo alinyimwa baada ya shambulizi hilo, mwaka 2019 alivuliwa ubunge na mpaka sasa gari yake iko mikononi mwa Polisi.

Akizungumzia kuhusu sakata la Spika wa bunge Dr.Tulia Ackson juu ya wabunge wa CHADEMA amemwambia Rais kwamba spika Ackson asiwafundishe CHADEMA namna ya kuendesha chama chao yeye anatakiwa afanyie kazi maamuzi ya chama kama wanavyompa taarifa na walishamwambia hao si wabunge wa CHADEMA na yeye kuwaambia mpaka mchakato ukamilike “hayo hayamhusu kabisa Spika huyo na hata kama haujakamilika hawa sio wanachama wa Chadema na kwa maana hiyo kama sio wanachama wa Chadema hawatakiwi kuwa bungeni hata kwa siku moja zaidi” alisisitiza Lissu.

Lissu amesema Rais Samia amewamwambia amemsikia na atayafanyia kazi hayo madai yake.

Lissu pia amesema kuna mazuri yananayofanywa na utawala wa Rais Samia, akisema hasa kurejesha uhusiano na mataifa ya nje na kurejesha mapambano dhidi ya Covid lakini angependa kuona mengi zaidi kama kubadilisha sheria na taratibu ambazo zimeumiza watu wengi nchini humo.

Lakini anasema kwa ujumla hali ya jumla imebadilika tangu aingie madarakani lakini hali hiyo peke haitoshi. Lakini atamuuunga mkono ikiwa atakubali kwamba nchi inahitaji uponyaji aiongoze kuiponya nchi hiyo aliongeza.

VOA Swahili

Hata kama kitendo cha Rais kuamua kufuta kesi ya Mbowe au mtuhumiwa mwingine yeyote sio kuingilia uhuru wa mahakama, obviously, ni kinyume cha misingi ya Rule of Law. Ni kupoka madaraka yasiyokuwa ya kwake!

Mtu pekee mwenye mamlaka ya kufanya uamuzi wa kumshitaki au kutomshitaki mtuhumiwa yeyote ni DPP, na kikatiba, anapaswa kufanya hivyo bila kuingiliwa na mtu yeyote yule.

Tukishaanza kuweka exceptions uchwara za mazingira ambayo Rais anaweza kutoa maelekezo (straight au katika form ya ushauri) kwa DPP kufuta kesi fulani, basi lazima pia tukubali na tutarajie kwamba yatakuwepo mazingira ambayo DPP atafanya uamuzi wa kuwashitaki watuhumiwa fulani kwa maelekezo ya Rais.

Nipo tayari kubaki pekee yangu nikisema hii sio Rule of Law!
 
Makamu Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA nchini Tanzania Tundu Lissu anayeishi uhamishoni Ubelgiji ameeleza azma yake ya kurudi nchini Tanzania wakati wowote.

Lissu alisema hayo katika mahojiano maalum na VOA baada ya kukutana na rais wa Tanzania Samia suluhu mjini Brussels Jumanne.

Akizungumzia dai lake la kutaka kesi ya mwenyekiti wa chama cha Chadema Freeman Mbowe ifutwe, Lissu amesema jambo hilo sio kuingilia uhuru wa Mahakama na kwamba kesi hiyo “haina maslahi yoyote na afanye kama alivyofanya kuhusiana na kesi ya mashekhe wa Uamsho wa Zanzibar ambao walifutiwa mashitaka baada ya kukaa gerezani miaka 9 hakuna cha kuingilia mhimili wowote hapa”

Akisisitiza kwamba hajamwambia Rais aongee na Jaji bali mwendesha mashitaka ambaye ni mteule wa Rais na anafanya kazi kama sehemu ya utawala sio sehemu ya Mahakama.

Pia kiongozi huyo wa upinzani na mgombea Urais mwaka 2020 amemwambia Rais kuhusu suala la Serikali kutaka kuwafukuza kwa nguvu wananchi wa wilaya ya Ngorongoro kutoka eneo la mamlaka ya hifadhi kuwa ni jambo la hatari na linaweza kuchafua nchi na akasema Rais amemwambia amelizuia.

Lissu pia amegusia Uhuru wa vyama vya siasa kufanya kazi akisema amemweleza Rais Samia kuhusu zuio aliloliita haramu la vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara na maandamano na madai ya hitaji la katiba mpya nchini humo na mfumo mpya wa uchaguzi.

Itakumbukuwa mbunge huyo wa zamani na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2020 alinusurika katika shambulizi baya la risasi na watu wasiojulikana mwaka 2017 na amemtaka rais ahakikishe anatendewa haki kwa mambo ambayo alinyimwa baada ya shambulizi hilo, mwaka 2019 alivuliwa ubunge na mpaka sasa gari yake iko mikononi mwa Polisi.

Akizungumzia kuhusu sakata la Spika wa bunge Dr.Tulia Ackson juu ya wabunge wa CHADEMA amemwambia Rais kwamba spika Ackson asiwafundishe CHADEMA namna ya kuendesha chama chao yeye anatakiwa afanyie kazi maamuzi ya chama kama wanavyompa taarifa na walishamwambia hao si wabunge wa CHADEMA na yeye kuwaambia mpaka mchakato ukamilike “hayo hayamhusu kabisa Spika huyo na hata kama haujakamilika hawa sio wanachama wa Chadema na kwa maana hiyo kama sio wanachama wa Chadema hawatakiwi kuwa bungeni hata kwa siku moja zaidi” alisisitiza Lissu.

Lissu amesema Rais Samia amewamwambia amemsikia na atayafanyia kazi hayo madai yake.

Lissu pia amesema kuna mazuri yananayofanywa na utawala wa Rais Samia, akisema hasa kurejesha uhusiano na mataifa ya nje na kurejesha mapambano dhidi ya Covid lakini angependa kuona mengi zaidi kama kubadilisha sheria na taratibu ambazo zimeumiza watu wengi nchini humo.

Lakini anasema kwa ujumla hali ya jumla imebadilika tangu aingie madarakani lakini hali hiyo peke haitoshi. Lakini atamuuunga mkono ikiwa atakubali kwamba nchi inahitaji uponyaji aiongoze kuiponya nchi hiyo aliongeza.

VOA Swahili
Serikali kufuata kesi siyo kuingilia mamlaka ya Mahakama. Hii imefanyika mara nyingi tu kila wakati serikali inapoona haina haja ya kuendelea na kesi.

Hata Maza majuzi kasema wamemfutia Lissu kesi zake zote.
 
Lissu hana mamlaka ya kumwambia rais nini cha kufanya kwahiyo tafsiri sahihi hapo ni kumuomba rais amfutie kesi Mbowe.
Jaribu kuwa mwelewa kidogo. Sijasema nani yuko sahihi kati ya Zito na Lissu. Nimebainisha tofauti yao kwa yale waliyozungumza/waliyoshauri.
 
.....Kuhusu suala la wabunge 19 sikubaliani na mtizamo wa Lissu

Ni mpaka pale uamuzi wa rufaa yao huko kwenye chama utakapohitimishwa

Wabunge 19 wa CHADEMA bado ni wabunge halali.. CHADEMA iache kutumia mabavu itumie haki na demokrasia. Lakini pia CHADEMA haiwezi kuwa mwamuzi wa mwisho dhidi ya wabunge .. baada ya uamuzi huo wabunge 19 wana uwezo wa kuwasilisha pingamizi mahakamani kama ilivyokuwa kwa Zitto Kabwe

Uzoefu unaonesha kuwa CHADEMA haizingatii hata utaratibu wa katiba yao ktk kumfuta mtu uanachama badala yake hutumia mabavu na maamuzi ya watu wachache waliojimilikisha chama

KUHUSU SUALA LA KUINGILIA MAHAKAMA UKWELI NI KUWA CHADEMA KTK HILI INAINGILIA UHURU WA MAHAKAMA.. KUFANYA EXTERNAL INFLUENCE JUU YA KESI ILIYOPO MAHAKAMANI NI KUINGILIA UHURU WA MAHAKAMA PIA. SEMA KWA SABABU JAMBO HILI LIMEWAGUSA WAO NA NDIYO MAANA INAONEKANA SIYO KUINGILIA UHURU WA MAHAKAMA

KWA mtizamo wangu naona kuwa suala la kesi ya Mbowe kwa kuwa tayari lipo mahakamani; tuwaachie mahakama kazi hiyo ya kutafsiri sheria na tuwaamini kuwa watafanya uamuzi wa haki.

Endapo maamuzi ya mahakama itaonekana kutoridhika upo utaratibu wa kukata rufaa
Hakika wote tungependa taratibu zifuatwe ikiwa ni pamoja na kuona maamuzi ya mahakama inachukua nafasi na hata ikibidi rufaa ikatwe baadaye.
Lakini kwa mifumo ya tawala kandamizi za kidekteta kama hapa Tanzania; ni sawa na kusema the right delayed is equal to right denied.
Haikutegemewa kuona kwa kiongozi aliyepata kuwa Kiongozi Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni leo hii awe anasota gerezani kwa kesi za kubambika.
Hakuna asiyejua utawala wa Hayati JPM ulivyokuwa mbaya kiutawala, wizi wa kura, kubambikia watu kesi za michongo, watu kupotea na kuuawa bila kujulikana asili na sababu za mauaji na vikosi vya watu wasiojulikana.
Hivyo leo unapoona kiongozi anashitakiwa kwa makosa yaliyojengwa kipindi cha vuguvugu la Uchaguzi Mkuu wa 2020, mtu huwezi kukosa kuamini kwamba hizi zilikuwa ni moja ya kesi kisiasa tena zenye nia kupooza upinzani nchini.
Sasa hata serikali ya sasa itaonekana ya kikandamizaji,.kwa sababu misingi ya kesi imejengwa tokea kwenye vuguvugu la uchaguzi Mkuu uliopita.
Na bahati mbaya kuwekwa ndani kwa Mh FAM ni katika za:
a) Kuruhusu utawala wa sasa kujitanua bila ya kuwepo na mpinzani makini;
b) Kumdhoofisha Mh FAM katika harakati zake nyingi za kisiasa kama mwenyekiti wa CHADEMA, alizozipata kuzifanya kipindi hiki.
Kwa ujumla, inasikitisha sana hadi katika maendeleo jamii iliyopiga, bado inadhaniwa kwanza ili mtu ajitanue sawasawa ni kumfunga mpinzani wake korokoroni.
 
Kwa muktadha wa swala la Mbowe lilivyo, Haitaji msamaha, na wala sio sahihi kutumia neno msamaha sababu hana kosa alilofanya ambalo yahitajika aombe au aombewe msamaha.

Jaribu kuzitafakari hizi kauli mbili, Na utaona mantiki ya swala la Mbowe.
---
“mwenzetu hayupo hapa kwa sababu ana changamoto za kisheria, itafutwe namna, ASAMEHEWE” - Zitto Kabwe

“kesi ya mwenyekiti Mbowe ni 'ubatili mtupu na ushahidi ni wa uongo' na hailisaidiu taifa kwa lolote, IONDOLEWE
- Tundu Lissu

#76
Naungana na comment yako, akiomba msamaha maana yake anakiri kosa indirect, tuache hili jambo limalizike mahakamani ili tujue mbivu na mbichi
 
We jamaa ni mental staff, hivi umemwelewa lissu?
elewa Lissu hajamuombea Mbowe msamaha bali amemuagiza rais afute mashtaka yasiyo na tija yaan ya mchongo tofauti na kibaraka wenu zitto
Wewe ndo bure kabisa, yaani tundu amuagize mh rais afute kesi ya Mbowe? Una akili kweli?
Nyumbu hovyo kabisa.
 
Lissu hajaomba mbowe asamehewe acha uzito wa kufikiri yeye ametaka kesi ifutwe. Kesi kufutwa na kusameheana ni vitu viwili tofauti. Kusamehewa ni mpaka ahukumiwe
Sasa wale pingapinga FC mliompinga zitto kuomba kwa rais gaidi amsamehewe njooni mpige makofi kwa tundu tafadhali.
 
.....Kuhusu suala la wabunge 19 sikubaliani na mtizamo wa Lissu

Ni mpaka pale uamuzi wa rufaa yao huko kwenye chama utakapohitimishwa

Wabunge 19 wa CHADEMA bado ni wabunge halali.. CHADEMA iache kutumia mabavu itumie haki na demokrasia. Lakini pia CHADEMA haiwezi kuwa mwamuzi wa mwisho dhidi ya wabunge .. baada ya uamuzi huo wabunge 19 wana uwezo wa kuwasilisha pingamizi mahakamani kama ilivyokuwa kwa Zitto Kabwe

Uzoefu unaonesha kuwa CHADEMA haizingatii hata utaratibu wa katiba yao ktk kumfuta mtu uanachama badala yake hutumia mabavu na maamuzi ya watu wachache waliojimilikisha chama

KUHUSU SUALA LA KUINGILIA MAHAKAMA UKWELI NI KUWA CHADEMA KTK HILI INAINGILIA UHURU WA MAHAKAMA.. KUFANYA EXTERNAL INFLUENCE JUU YA KESI ILIYOPO MAHAKAMANI NI KUINGILIA UHURU WA MAHAKAMA PIA. SEMA KWA SABABU JAMBO HILI LIMEWAGUSA WAO NA NDIYO MAANA INAONEKANA SIYO KUINGILIA UHURU WA MAHAKAMA

KWA mtizamo wangu naona kuwa suala la kesi ya Mbowe kwa kuwa tayari lipo mahakamani; tuwaachie mahakama kazi hiyo ya kutafsiri sheria na tuwaamini kuwa watafanya uamuzi wa haki.

Endapo maamuzi ya mahakama itaonekana kutoridhika upo utaratibu wa kukata rufaa

..Halima na wenzake wamekata rufaa kufukuzwa uanachama.

..maana yake ni.kwamba sasa hivi sio wanachama wa Chadema.

..Na kama hawana chama hawapaswi kuwa bungeni.
 
Jaribu kuwa mwelewa kidogo. Sijasema nani yuko sahihi kati ya Zito na Lissu. Nimebainisha tofauti yao kwa yale waliyozungumza/waliyoshauri.
Hata mimi nimeeleza tu kilicho sahihi kwamba alichokifanya Lissu ni ombi tu hakina tafsiri nyengine.
 
Bunge halina taarifa

..Bunge walishapewa taarifa kuwa Halima na wenzake wamefukuzwa.

..Spika Ndugai alikataa kuchukua hatua stahiki baada ya kupokea taarifa toka kwa KM wa Chadema kwamba Halima na wenzake wamefukuzwa ktk chama hicho.
 
Taifa linahitaji kufanyiwa maombi ili Mungu aliponye maana limezungukwa na jitu ya Ovyo sana eg Lissu
 
Hao wanawake 19 sio wanachama wa chama cha Chadema kwani walishafukuzwa na kamati kuu unless wawe reinstated na Baraza Kuu kufuatia rufaa waliokata.
Chama kinachojinasibu kupigania haki za watu, leo mwaka wa pili hakijasikiliza rufaa za watuhumiwa 19. Kama si udikteta ni nini?
 
Ipo haja ya wote waliobumba kesi hii ya uongo wachukuliwe hatua. Wakiwemo siro, kingai, mahita jumanne gudlack majaji na mahakimu wote waliojiingizia pesa haramu kama posho mbalimbali za kushiriki kesi ya uongo na kuitia hasara kodi yetu.
Hio gharama ya kuendesha kesi si ingenunua hata madawati.
 
Back
Top Bottom