Tetesi: Tundu Lissu kujiunga ACT Wazalendo, Abdul Nondo naye kuula!

Tetesi: Tundu Lissu kujiunga ACT Wazalendo, Abdul Nondo naye kuula!

Status
Not open for further replies.
Tetesi zina mambo mawili kuwa za uongo au ukweli, ila nachokumbuka ni kuwa walikuwa na mazungumzo ya mipango ya muungano wa vyama na kutoa tofauti zao ila la kuhamia chama ACT hilo mmesema nyinyi ngoja tuwe na subira kuona maamuzi ya baadae
 
Ndugu zangu,

Bado ni tetesi lakini hapa JF ni muhimu huu mjadala ukawepo kwa afya ya siasa za nchi.Zitto Kabwe ndiye mwanasiasa pekee aliyemtembelea Tundu Lissu mara tano hospitalini,mara tatu Ubelgiji mara mbili Nairobi.Inasemekana ziara za Ubelgiji zaidi zilijawa na mazungumzo kuhusu hatma ya Lissu kisiasa kwa mazungumzo ya wiki mbili zilizopita kuna uwezekano mkubwa Tundu Lissu akajiunga na ACT Wazalendo ili kuendelea na shughuli za siasa.

Bado haijaeleweka kwanini Lissu anafikiri kuondoka Chadema hizi ndio siasa na mauzauza yake,huenda kuna alama za nyakati zimesomwa.

Zaidi ya hilo kijana Abdul Nondo ambaye miezi michache alitumika na Mbowe ili kufifisha nguvu za Zitto Kigoma sasa rasmi ACT Wazalendo ambapo wakati wowote atapewa majukumu ndani ya chama hicho baada ya kumaliza masomo yake UDSM.

Habari nyingi huanza kama tetesi hapa JF mwishowe hubainika kuwa ni za kweli.
Ukiwa kwenye siku zako huwa unapata tabu sana dawa yake ubebe mimba tu.
 
Mkuu Kaka Wakudadavua, kwanza naunga mkono hoja, ila duh...!. Kiukweli hii kali!.

Hata hivyo asante Kaka Wakudadavua, kutudadavulia hii, umetupakulia ikiwa ya moto moto, kwa jinsi unavyopata taarifa za ndani za vyama, nakuvulia kofia, Musiba atasubiri!, hongera unafanya kazi nzuri Kaka Wakudadavua. Asante tena. Na kiukweli nakukubali sana...basi tuu, kwa vile wewe ni Kaka, ungekuwa Dada, uvumilivu ungenishinda!.

P
Huyo mbona sigara nyota, wewe tu.
 
Acacia wamesimamia na kufadhili vikao vya Kuwaunganisha Zitto na Lissu

Lissu, Zitto, Jussa, Seif Sharif, Nyalandu ni Muungano hatare kwa Maslah ya Taifa na Chama uangaliwe kwa macho makini

Dola isimame na Chadema dhidi ya ACT

ACT ni kirusi cha Mabeberu kinachonenepeshwa kwa kasi ya ajabu

Mkuu hamna la ajabu hapo kisiasa maana China ndio imewajengea ccm ukumbi wa mikutano hapo Dodoma. Hiyo dola ilikuwa likizo haikujali maslahi ya taifa kwa chama cha siasa kujengewa ukumbi wa mikutano? Au hilo jengo ndio ilikuwa fumba macho ili wachina wapate miradi mbalimbali ya serikali na kuishia kujenga substandard projects?
 
Lisu washamtoa mchezoni kispycholojia hayupo sawa ikiwa mtu tu aliyekoswa na lisasi anachanganyikiwa je aliyepigwa risasi mwilini lisu ndio basi tena katika siasa za bongo

Msishangae tu akaunga juhudi mh rais hapo ndio mtaishiwa pause maana washamvuluga

Hakuna la ajabu hapo maana hata Slaa yuko ccm na aliishia kwenda huko na mkewe. Hata Lissu anaweza kwenda popote na atapata support yetu iwapo tu ataongea lugha moja na sisi.
 
Mkuu hamna la ajabu hapo kisiasa maana China ndio imewajengea ccm ukumbi wa mikutano hapo Dodoma. Hiyo dola ilikuwa likizo haikujali maslahi ya taifa kwa chama cha siasa kujengewa ukumbi wa mikutano? Au hilo jengo ndio ilikuwa fumba macho ili wachina wapate miradi mbalimbali ya serikali na kuishia kujenga substandard projects?

Ukumbi wa Ccm Dodoma haukujengwa na Serikal ya China

Umejengwa na Chama Rafiki Chama tawala cha China
 
Hujui siasa wala huwajui wanasiasa. Kwani maalim seif ambaye aliungana na chadema na akaungwa mkono urais kupitia ukawa mbona alihamia ACT kabla ya chadema? Kwani chadema walimfanya nini?

Maalim Seif kuhamia ACT ni bora kwa kudumisha upinzani kwa kukipa nguvu chama kingine cha upinzani.

CHADEMA walkwisha kuwa na wafuasi kiasi visiwani na ingeleta mvutano kati ya CDM wahamiaji na CDM asili. ACT ni kama mwari visiwani kwa hiyo wahamiaji hawakujiona wageni na kusimangwa.
 
Ninachokiona mimi ni Zitto kuwa mgombea mwenza wa Lissu come 2020

Hawezi kuwa mgombea mwenza wake maana wote wanatokea bara. Mgombea mwenza anapaswa kutoka Znz. Vyovyote iwavyo, Zito ndio anafaa zaidi kugombea urais kwani anamudu uchumi, mambo ya kijamii na demokrasia na ana misimamo ya wastani, shida yake haaminiki. Lisu pia anafaa lakini amejikita kwenye sheria zaidi kuliko uchumi na ana siasa za misimamo mikali. Lissu akiwa rais tunaweza kukutana na tatizo lililopo sasa hivi kuwa na rais anayesimamia jambo moja tu na kusahau maeneo mengine.
 
Ninachokiona mimi ni Zitto kuwa mgombea mwenza wa Lissu come 2020
Inaonesha huna kabisa habari ya kinachoendelea kwenye siasa. Zitto na Tundu wanatoka bara MGOMBEA MWENZA LAZIMA ATOKE UPANDE WA PILI WA MUUNGANO na kuna sheria kwamba ukihamia chama kipya kaa miaka miwli ndo ugombee cheo cha kisiasa.
 
Ndugu zangu,

Bado ni tetesi lakini hapa JF ni muhimu huu mjadala ukawepo kwa afya ya siasa za nchi.Zitto Kabwe ndiye mwanasiasa pekee aliyemtembelea Tundu Lissu mara tano hospitalini,mara tatu Ubelgiji mara mbili Nairobi.Inasemekana ziara za Ubelgiji zaidi zilijawa na mazungumzo kuhusu hatma ya Lissu kisiasa kwa mazungumzo ya wiki mbili zilizopita kuna uwezekano mkubwa Tundu Lissu akajiunga na ACT Wazalendo ili kuendelea na shughuli za siasa.

Bado haijaeleweka kwanini Lissu anafikiri kuondoka Chadema hizi ndio siasa na mauzauza yake,huenda kuna alama za nyakati zimesomwa.

Zaidi ya hilo kijana Abdul Nondo ambaye miezi michache alitumika na Mbowe ili kufifisha nguvu za Zitto Kigoma sasa rasmi ACT Wazalendo ambapo wakati wowote atapewa majukumu ndani ya chama hicho baada ya kumaliza masomo yake UDSM.

Habari nyingi huanza kama tetesi hapa JF mwishowe hubainika kuwa ni za kweli.
Rubbish, waziri mzima unaandika "mavi" kiwango hiki. Acha utoto wewe ni mtu "mkubwa", tunategemea hekima toka kwako siyo utumbo wa hivi!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom