Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Mkimchagua Magufuli, ana lengo la kubadili Katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya kutawala

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Mkimchagua Magufuli, ana lengo la kubadili Katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya kutawala

TOO MUCH LIES
Halafu wanalalamika kuwa vyombo vya habari hawaandiki habari zao

Jana tu walitoa press release kuwa TCAA imezuia Helukopta kuruka kwa sababu zisizoeleweka!!! Nashukuru press waka wa ignore wakijua hawako reliable taarifa zao wakaenda TCAA wenyewe wakaambiwa rubani mrusha helikopta kapita umri wa kisheria na hilo ndilo likatangazwa TV zote lile la uongo likatupiliwa Mbali

Kifupi chadema wamepoteza Truth Reliability kwenye media tofauti na enzi za Dr Slaa.Alikuwa akiongea anashusha ushahidi wa ukweli na uhakika usio na chembe ya shaka
Kiasi kuwa media policies hazihangaiki my counter check wanajua kuwa alichotamka kiko sahihi

Lisu sio presidential material anaongea vitu vya kuokoteza na kutunga kama mswahili tu wa mtaani

Umeandika maelezo marefu, lakini ukweli ni kuwa vyombo vya habari kwa sasa chini ya Magufuli haviko huru. Hayo uliyosema eti vyombo vya habari enzi za Slaa vilikuwa vinatoa habari maana vilijua ni kweli asemacho, si kweli bali vyombo vya habari vilikuwa vina uhuru wa kuridhisha wakati huo kuliko sasa. Kuna siku Slaa alisema kuwa kuna container lina kura zilizopigiwa ccm tayari, lakini ilifahamika baadae kuwa sio kweli, na habari ile ilitangazwa.

Ni hivi, vyombo vya habari kwa sasa haviko huru chini ya dictator, hivyo sio rahisi kwa mkosoaji wa dictator kuruhusiwa habari zake za kweli kutangazwa. Hilo la kuwa Magufuli ana mpango wa kubadilisha katiba ili akae madarakani zaidi, hilo wala halina kificho. Liko wazi peupe.
 
Lissu watu hawataki kusikia hayo,wanataka kujua ukichaguliwa wewe utaletaje maisha bora?
Hata lissu akichaguliwa hakuna garantii kwamba hataongeza muda,atasema ccm imetawala miaka 50,acha na sisi tutawale miaka 20 hakuna uchaguzi,na kwa vile anaungwa mkono na mabeberu watamshangilia tu

Uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara.
 
Mkimpitia Magufuli mtalimia meno. Watumishi wengine wa umma nafasi zenu haziwapi hata fursa ya kupata elfu kumi kwa siku nje ya mshahara. Twende na Magu mpaka nimalizie Nyumba yangu ya pili. Huu wakati una upepo wa pesa sana
 
Gadafi alikua dikteta lakin libya waliishi kwa raha

Waliishi kwa raha, hakuna maisha ya raha chini ya dictator, zaidi ya maisha ya ukondoo. Ukitaka uishi kwa raha chini ya dictator unatakiwa uweke mkia matakoni na kumsifia basi. The same applies to here.
 
Umeandika maelezo marefu, lakini ukweli ni kuwa vyombo vya habari kwa sasa chini ya Magufuli haviko huru. Hayo uliyosema eti vyombo vya habari enzi za Slaa vilikuwa vinatoa habari maana vilijua ni kweli asemacho, si kweli bali vyombo vya habari vilikuwa vina uhuru wa kuridhisha wakati huo kuliko sasa. Kuna siku Slaa alisema kuwa kuna container lina kura zilizopigiwa ccm tayari, lakini ilifahamika baadae kuwa sio kweli, na habari ile ilitangazwa.

Ni hivi, vyombo vya habari kwa sasa haviko huru chini ya dictator, hivyo sio rahisi kwa mkosoaji wa dictator kuruhusiwa habari zake za kweli kutangazwa. Hilo la kuwa Magufuli ana mpango wa kubadilisha katiba ili akae madarakani zaidi, hilo wala halina kificho. Liko wazi peupe.
Uhuru wa vyombo vya habari ni kuandika ukweli sio uongo

Tatizo chadema ni kudhani uandishi wa habari kazi yake tu ku report kama kasuku bila kuangalia ukweli wa hiyo habari
 
Amesikia sana ila anafanya makusudi ndio maana watu na vyombo vya habari vinazidi kumpuuza..hivi unaweza kuandika au kurusha maneno ya udaku kama hayo..

Na yeye tukisema katumwa ili agombee na hatimaye akipita mabeberu waje kuendeleza ubebaji wa rasilimali itakuwaje..? Yaani magufuli asimame aseme tundulissu katumwa tuna uhakika wa blah blah blah
Tatizo Lissu hajui vizuri siasa za majukwaani,laiti angefanya tathimini ya hotuba zake kabla ya kuzitapika.
Wapo wasaidizi wake wanammaliza haraka kwa kill me quick pills
Akiendelea kusema sema mbovu wapiga kura watamrarua bila huruma kwenye sanduku la kura.
 
Hii ni dalili tosha ya mfa maji. Hana sera. Badala ya kusema atawafanyia nini Watanzania anakuja na mambo ya kufikirika. Mwaga sera TL kama huna basi kaa kimya.

Amemwaga Sera kibao, ila mleta mada kaleta kipande hiki tu. Ukitaka nenda mwenyewe kwenye mikutano yake ukasikie kila kitu.
 
Lissu anakosa hoja, yeye aseme akiwa raisi atawafanyia nini watanzania kupitia kodi wanazolipa. Yeye amekuwa prophet kusema yajayo?
 
Uhuru wa vyombo vya habari ni kuandika ukweli sio uongo

Tatizo chadema ni kudhani uandishi wa habari kazi yake tu my report kama kasuku bila kuangalia ukweli wa hiyo habari

Uko sahihi kuwa uhuru wa habari ni kuandika ukweli na sio uongo. Ila hapa kwetu kwa sasa, tatizo ni kuandika ukweli unaomkera Magufuli na serikali yake. Hili liko wazi, hatusemi hakuna uhuru wa habari kwakuwa tunataka habari za uongo, bali tunataka habari za ukweli bila kujali zinamuumiza nani. Tatizo la sasa ni habari ziwe zile zinazoiufurahusha serikali tu.
 
Lissu anakosa hoja, yeye aseme akiwa raisi atawafanyia nini watanzania kupitia kodi wanazolipa. Yeye amekuwa prophet kusema yajayo?

Lisu ameongea hoja nyingi sana kwenye huo mkutano, ila ww unajadili kipande hiki. Dalili ya mvua ni mawingu, kwani ukisema mvua itanyesha ni makosa kwakuwa wewe sio prophet?
 
Uko sahihi kuwa uhuru wa habari ni kuandika ukweli na sio uongo. Ila hapa kwetu kwa sasa, tatizo ni kuandika ukweli unaomkera Magufuli na serikali yake. Hili liko wazi, hatusemi hakuna uhuru wa habari kwakuwa tunataka habari za uongo, bali tunataka habari za ukweli bila kujali zinamuumiza nani. Tatizo la sasa ni habari ziwe zile zinazoiufurahusha serikali tu.
Kumsema mtu wako kuwe na ukweli sio tu kumsema mfano mimi nasema mkutano wa hadhara kuwa Lisu ni kichaa unataka vyombo vya habari viandike hilo wakati havijaona cheti cha daktari na ushahidi wa hilo nililosema?

Waandishi wetu wa sasa ni wasomi sio makasuku wa kuripoti chochote anachosema mtu
 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii


Baada ya kiki za miujiza kubuma, amebaki kuwa mtabiri kama nabiii Tito.
Aaache kuweweseka , kipigo chake kiko palepale.
 
View attachment 1565776
ukilinganisha na kauli zake,jibu unapata. Huu ukorofi na kutisha watu huwezi kuondoka kizembezembe tu halafu nani atakulinda. Hawa kina M7 wanapenda wapumzike ila wanaogopa maisha baada ya uraisi

Exactly.. lazma aogope maisha baada ya kudhulumu, kunyanyasa watu. Huyu haki ya Mungu lazima ang’ang’anie tena kuongoza. Na hapo atamtumia huyo huyo Speaker uchwara.
 
Lissu ndiye Rais wetu. Hiyo October ifike tumalize mambo. Mwandalieni Mzee wa Chato makao huko kijijini.
 
Lisu ameongea hoja nyingi sana kwenye huo mkutano, ila ww unajadili kipande hiki. Dalili ya mvua ni mawingu, kwani ukisema mvua itanyesha ni makosa kwakuwa wewe sio prophet?
Toka lisu akiwa bungeni mpaka Leo, zaidi ya kutengeneza maigizo na KIKI ,kunalolote la maanaa ambalo ameliibua la kulisaidia selikali na watanzania kwa ujumla?
Taja hata hoja yoyote ambayo lisu ameshachangia bungeni au kuibua likawa msaada kwa taifa.
 
Hii ni dalili tosha ya mfa maji. Hana sera. Badala ya kusema atawafanyia nini Watanzania anakuja na mambo ya kufikirika. Mwaga sera TL kama huna basi kaa kimya.
Chadema inarusha mateke ya mwisho kabla ya kukata roho
 
Ivi anayefikiri kuongeza mishahara ya watumishi kama motisha ili apendwe kisiasa anapima mzani kwa dhati kweli?

Yaani aanze na kusema atatoa wapi fedha za kuongeza, kama chanzo ni Kodi kutoka kwa hawa wananchi wadogo, basi sio hoja kiviiiiile!!!
 
Eti kwamba anaiamini zaidi kauli ya ndugai kuliko ya magufuli mwenyewe ambaye amekuwa akisisitiza kuiheshimu katiba katika kuongoza..

Kwamba ameanza kumuamini sana ndugai..ila ndugai akimueleza yeye ukweli anakuja juu..
Raisi katiba ikimtaka aendeleze vipindi zaidi ya 10 hawezi kukataa.

Spika kwenye hili ana nguvu kuliko raisi maana yeye kupitia wawakilishi wa wananchi ndio wanaweza kusema miaka kumi haitoshi au inatosha.

Raisi yeye anatii. Kwa sasa raisi hawezi kusema ataongeza muda maana katiba haimruhusu na si kazi yake kubadili katiba, hiyo ni kazi ya wananchi kupitia wawakilishi.

Katiba itakapobadilika, Raisi ni ngumu kusema hapana ikiwa nchi inamuhitaji na atakapokubali haitamaanisha kuwa alisema uongo kuwa hatoongeza muda, maana anafata matakwa ya wananchi.

Swali ni, wananchi wanatakaje? Jibu litapatikana pale ambapo Raisi atachaguliwa tena na mswada ukaletwa bungeni na mambo yakabadilika halafu wananchi wakaafiki na wakatulia. Kimya maana yake hakuna tatizo. Propaganda kuwa wananchi ni waoga wa polisi na jeshi hazitakuwa na maana wala hazitabadili uhalisia.
 
Back
Top Bottom