Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Mkimchagua Magufuli, ana lengo la kubadili Katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya kutawala

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Mkimchagua Magufuli, ana lengo la kubadili Katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya kutawala

Tatizo Lissu hajui vizuri siasa za majukwaani,laiti angefanya tathimini ya hotuba zake kabla ya kuzitapika.
Wapo wasaidizi wake wanammaliza haraka kwa kill me quick pills
Akiendelea kusema sema mbovu wapiga kura watamrarua bila huruma kwenye sanduku la kura.
Wamrarue mara ngapi..? Alipowaaminisha watu kwa nguvu atagombea watu walijua ana kitu kipya tofauti..sera zake zimeegemea zaidi watu wa mjini tena waliojiriwa.. ukimuambia mkulima au mfugaji nitaongeza mshahara wa miaka mitano atakuelewa nini? Sana sana ni kama unamtenga maana yeye hana pa kuongezewa mshahara.

Unamueleza mtu bima ya afya kabla hujamjengea hospital na kumletea wataalam hiyo bima atajitibia kwa mganga wa kienyeji?

Kuna mambo ambayo watu yanawagusa kwa pamoja..ukisema uboreshaji wa usafiri wa ndege, maji, reli na barabara nzuri tayari umegusa kila kundi, ukisema elimu bure, ujenzi wa madarasa, mikopo elimu ya juu, viwanda na ajira hapa umegusa wote, ukisema zahanati, vituo vya afya, hospital za mikoa..hapa napo umegusa mtu wa kijijini hadi wa mjini...ukisema uhakika wa maji..hapa umegusa mjini na kijijini..uhakika wa umeme (JNHPP) na REA..hapa umewagusa wa mjini na vijiji..

Ukianza kusema ooh kingereza ndio lugha, ooh bima ya afya, ooh nitaongeza mishahara, ooh maendeleo sio vitu wakati mkulima wa ndizi bukoba kule alikuwa anasafiri tani ya ndizi kwa 120000 na leo anasafirisha tani hiyo hiyo kwa elf 25 baada ya kupelekewa kitu ambacho ni meli..sidhani kama jamii itakuelewa.
 
Ivi anayefikiri kuongeza mishahara ya watumishi kama motisha ili apendwe kisiasa anapima mzani kwa dhati kweli?

Yaani aanze na kusema atatoa wapi fedha za kuongeza, kama chanzo ni Kodi kutoka kwa hawa wananchi wadogo, basi sio hoja kiviiiiile!!!

Sisi si ni matajiri
Tuna mihela mingi
Sasa kwa nini tuwe makatili tuvunjie watu nyumba kikatili wakati kuna zuio la mahakama kisha tusiwalipe?
 
Kumsema mtu wako kuwe na ukweli sio tu kumsema mfano mimi nasema mkutano wa hadhara kuwa Lisu ni kichaa unataka vyombo vya habari viandike hilo wakati havijaona cheti cha daktari na ushahidi wa hilo nililosema?

Waandishi wetu wa sasa ni wasomi sio makasuku wa kuripoti chochote anachosema mtu

Narudia tena, hivyo vyombo vya habari haviko huru ndio maana wanaogopa kuandika yanayosemwa na Lisu dhidi ya Magufuli. Siasa sio hesabu useme 2+2 ni 4, na ukiweka jibu lingine ni makosa. Hilo suala la Magufuli kutaka kujiongezea muda wa kukaa madarakani halina kificho, linasemwa wazi wazi hadharani na hata bungeni. Mfano rais Mstaafu Mwinyi amewahi kulisema, waziri mkuu mstaafu Pinda amewahi kulisema, huko bungeni ni zaidi ya mara moja limesema, tena kibaya zaidi limesemwa na spika na wabunge wa ccm. Kwa dalili kama hizo kwanini Lisu asitoe tahadhari kwenye kampeni?

Ifahamike kwenye kampeni ni pamoja na kusema mapungufu ya mpinzani wako, hasa hayo ya mifumo ya kiutawala kupitia katiba. Ingekuwa vyombo vya habari viko huru vingeandika, maana hiyo ni tahadhari halali kwa wapiga kura, labda kama hujui siasa ni nini?
 
Toka lisu akiwa bungeni mpaka Leo, zaidi ya kutengeneza maigizo na KIKI ,kunalolote la maanaa ambalo ameliibua la kulisaidia selikali na watanzania kwa ujumla?
Taja hata hoja yoyote ambayo lisu ameshachangia bungeni au kuibua likawa msaada kwa taifa.

Omba Hansard za bunge, kisha fuatilia sakata la Escrow. Ukishamaliza kusikiliza uje tuendelee na mjadala.
 
Raisi katiba ikimtaka aendeleze vipindi zaidi ya 10 hawezi kukataa.

Spika kwenye hili ana nguvu kuliko raisi maana yeye kupitia wawakilishi wa wananchi ndio wanaweza kusema miaka kumi haitoshi au inatosha.

Raisi yeye anatii. Kwa sasa raisi hawezi kusema ataongeza muda maana katiba haimruhusu na si kazi yake kubadili katiba, hiyo ni kazi ya wananchi kupitia wawakilishi.

Katiba itakapobadilika, Raisi ni ngumu kusema hapana ikiwa nchi inamuhitaji na atakapokubali haitamaanisha kuwa alisema uongo kuwa hatoongeza muda, maana anafata matakwa ya wananchi.

Swali ni, wananchi wanatakaje? Jibu litapatikana pale ambapo Raisi atachaguliwa tena na mswada ukaletwa bungeni na mambo yakabadilika halafu wananchi wakaafiki na wakatulia. Kimya maana yake hakuna tatizo. Propaganda kuwa wananchi ni waoga wa polisi na jeshi hazitakuwa na maana wala hazitabadili uhalisia.
Nyie kila siku mnasema muhimili wa bunge hauna nguvu..sasa hivi tena unasema spika akitaka..ina maana hata kama magufuli hataki spika akitaka itakuwa hivyo..

Basi muifute ile kauli yenu ya kusema ooh bunge dhaifu..halina nguvu ya maamuzi..vinginevyo mtakuwa mnajitekenya wenyewe na mnacheka wenyewe.
 
Omba Hansard za bunge, kisha fuatilia sakata la Escrow. Ukishamaliza kusikiliza uje tuendelee na mjadala.
Inje ya kupayuka payuka na KIKI zake hajawahii ibua lolote la maana ambalo limekua msaada kwa taifa. Sasa hivi hana Sera yoyote zaidi ya kulazimisha apewe uraisi kama kifuta machozi .

Wapo mashujaa kama akina zito kabwe, kafulila na wengine wengi, waliibua ufisadi wa taifa hili hadi mtoto mdogo akafaham. Sasa huyo jamaa yenu inje na kushuhudia KIKI zake za miujiza ana lipi la maana kwa taifa letu?
 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii




chama chenyewe mmeshindwa kuchagua mwenye kiti mpya
 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii


Mzee anapanic mpka kaamua kujificha Shato kwanza
 
Raisi katiba ikimtaka aendeleze vipindi zaidi ya 10 hawezi kukataa.

Spika kwenye hili ana nguvu kuliko raisi maana yeye kupitia wawakilishi wa wananchi ndio wanaweza kusema miaka kumi haitoshi au inatosha.

Raisi yeye anatii. Kwa sasa raisi hawezi kusema ataongeza muda maana katiba haimruhusu na si kazi yake kubadili katiba, hiyo ni kazi ya wananchi kupitia wawakilishi.

Katiba itakapobadilika, Raisi ni ngumu kusema hapana ikiwa nchi inamuhitaji na atakapokubali haitamaanisha kuwa alisema uongo kuwa hatoongeza muda, maana anafata matakwa ya wananchi.

Swali ni, wananchi wanatakaje? Jibu litapatikana pale ambapo Raisi atachaguliwa tena na mswada ukaletwa bungeni na mambo yakabadilika halafu wananchi wakaafiki na wakatulia. Kimya maana yake hakuna tatizo. Propaganda kuwa wananchi ni waoga wa polisi na jeshi hazitakuwa na maana wala hazitabadili uhalisia.

Kwa taarifa yako rais kupitia vyombo vya dola ana nguvu zaidi ya 80%, hiyo kuwa wananchi ndio wenye maamuzi ni porojo za kinadharia. Ukitaka kujua ninachosema, angalia sasa hivi ni wakati wa kampeni, ni wapi rais anajibu maswali ya wananchi zaidi ya kuwahutubia? Hao wabunge angalia kwenye kampeni, mkutano una masaa matatu, masaa mawili ni burudani, nusu saa ni wapambe wa mgombea wanaongea, kisha dakika 10-15 mgombea anaongea akitakacho bila kuulizwa swali lolote. Kisha dakika zilizobaki ni kuagana na Viroja.

Huo ndio mfumo wa kupata viongozi waitwao wawakilishi wa wananchi, na wanachoenda kujadili huko bungeni ni utashi wa rais aliye madarakani. Chochote atakacho rais, ndio kinapewa kipao mbele na viongozi waliopatikana kutokana na matamasha ya burudani. Wananchi wanaweza kupiga kura tu, tena hakuna uhakika wa matokeo ili kuhalalisha rais kuendelea kukaa madarakani, lakini hawana maamuzi yoyote ya kumuweka kiongozi madarakani, labda walete machafuko. Hizo porojo za kuwa wananchi ndio wanaweka viongozi madarakani ni porojo kwa wasiojua lolote.
 
Kwanini kule chadema kila anayegombea uenyekiti anafukuzwa au kuhama au kufariki? Kwanini asianze ndani ya chama chake kuleta huo Uhuru, demokrasia na ukomo wa uongozi ndo aje atoe shutuma zisizo na ushahidi ambazo ni za kudhania tuu kwamba eti Magufuli atabadilisha katiba aongoze Kama Mbowe.
Aache kuropoka Mambo ya kubuni.
sawa kabisa mkuu aanzie kwa mwenyekiti wake kumuuliza kwanini hana kikomo jpm alishasema hataongeza hata siku moja yeye hayo maneno anayatoa wapi aache wendawazimu wake amuulize mbowe atang'atuka lini uenyekiti
 
Inje ya kupayuka payuka na KIKI zake hajawahii ibua lolote la maana ambalo limekua msaada kwa taifa. Sasa hivi hana Sera yoyote zaidi ya kulazimisha apewe uraisi kama kifuta machozi .

Wapo mashujaa kama akina zito kabwe, kafulila na wengine wengi, waliibua ufisadi wa taifa hili hadi mtoto mdogo akafaham. Sasa huyo jamaa yenu inje na kushuhudia KIKI zake za miujiza ana lipi la maana kwa taifa letu?

We robot hebu rudi studio wakakuprogram upya, au ufanyiwe updates ya taarifa kisha uje tuendelee na mjadala.
 
Mzee anapanic mpka kaamua kujificha Shato kwanza

Alikuwa anakimbizana na kasi ya Lisu, baada ya kuona kuwa kuna mgawanyo wa awamu za kampeni, na yeye kaona afanye hivyo. Huko sasa wale wazee wa gamboshi lazima waitwe, yapigwe Mazindiko ya hatari.
 
We robot hebu rudi studio wakakuprogram upya, au ufanyiwe updates ya taarifa kisha uje tuendelee na mjadala.
Matusi hayaondoi uhalisia wa kitu, kiukweli jamaa yenu inje ya KIKI hanamchango wowote kwa taifa hili, zaidi ya kuliangusha na kujipendekeza kwa mabebeluu.
 
Nyie kila siku mnasema muhimili wa bunge hauna nguvu..sasa hivi tena unasema spika akitaka..ina maana hata kama magufuli hataki spika akitaka itakuwa hivyo..

Basi muifute ile kauli yenu ya kusema ooh bunge dhaifu..halina nguvu ya maamuzi..vinginevyo mtakuwa mnajitekenya wenyewe na mnacheka wenyewe.

Udhaifu wa bunge ni hivyo kushindwa kuhoji wanayoletewa na serikali wanageuka rubber stamp. Hii maana yake ni kuwa azma ya Jiwe ya kuongeza ukomo wa madaraka kama alivyotudokeza Ndugai itapita tu
 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii


Ingekuwa vizuri, akawambia hata atakapotoa pesa ya kuyafanya hayo anayowaahidi.
 
Nzi wa kijani watabisha weee. Ila siku yakitimia, Hataonekana hata mmoja kwenye huu uzi.
 
Katiba tutaibadilisha sisi wananchi ili awe president wa milele...

Na ni haki yetu kutoa maoni

Viva JPM
Mgombea Urais kupitia Chama cha Chadema ndugu Tundu Lissu, amewaasa wananchi wa Bagamoyo kuwa, Magufuli ana lengo la kubadili ukomo wa vipindi vya utawala na ndiyo maana Hilo Suala lilizungumzwa bungeni na Spika Ndugai.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, Ndugai asingeweza yeye binafsi kulizungumza hilo bila kufahamu kinachoendelea kwenye mipango ya Magufuli.

Lissu akawaambia wananchi kuwa, wafikirie hali ngumu za maisha, ukatili na uonevu uliotokea katika kipindi hiki cha miaka mitano halafu eti Magufuli aongezewe miaka mingine.

Lissu amesema, serikali ya Chadema itakuwa ni Serikali ya Haki, Uhuru na Maendeleo. Itakuwa serikali itakayoheshimu watu tofauti na hii ya Magufuli yenye kudhalilisha watu hususan wanawake.

Lissu akasema kujenga miundo mbinu siyo hoja ya kunyima haki za watu kama vile nyongeza za mishahara zilizoko kisheria. Akasema kuwa hata mkooni alijenga reli, lakini hiyo haikuwa sababu ya kwa nini Tusimpinge, Akasema kuwa tulimpinga mkoloni kwa sababu hakuwa anatutendea HAKI.

Lissu akasema kuwa Nyerere alijenga reli ya TAZARA, tena ndefu zaidi lakini hakudhulumu stahiki za wafanyakazi

Kwa taarifa zaidi juu ya hoja nzito za Lissu tazama video hii

 
Wamrarue mara ngapi..? Alipowaaminisha watu kwa nguvu atagombea watu walijua ana kitu kipya tofauti..sera zake zimeegemea zaidi watu wa mjini tena waliojiriwa.. ukimuambia mkulima au mfugaji nitaongeza mshahara wa miaka mitano atakuelewa nini? Sana sana ni kama unamtenga maana yeye hana pa kuongezewa mshahara.

Unamueleza mtu bima ya afya kabla hujamjengea hospital na kumletea wataalam hiyo bima atajitibia kwa mganga wa kienyeji?

Kuna mambo ambayo watu yanawagusa kwa pamoja..ukisema uboreshaji wa usafiri wa ndege, maji, reli na barabara nzuri tayari umegusa kila kundi, ukisema elimu bure, ujenzi wa madarasa, mikopo elimu ya juu, viwanda na ajira hapa umegusa wote, ukisema zahanati, vituo vya afya, hospital za mikoa..hapa napo umegusa mtu wa kijijini hadi wa mjini...ukisema uhakika wa maji..hapa umegusa mjini na kijijini..uhakika wa umeme (JNHPP) na REA..hapa umewagusa wa mjini na vijiji..

Ukianza kusema ooh kingereza ndio lugha, ooh bima ya afya, ooh nitaongeza mishahara, ooh maendeleo sio vitu wakati mkulima wa ndizi bukoba kule alikuwa anasafiri tani ya ndizi kwa 120000 na leo anasafirisha tani hiyo hiyo kwa elf 25 baada ya kupelekewa kitu ambacho ni meli..sidhani kama jamii itakuelewa.
Amekurupuka angesubiri 2025, kwa sasa ajipange upya kujenga chama.
 
Back
Top Bottom