Lissu omba radhi. Kumtukana Nyerere ni kuwatukana watanzania
Kwanini Nyerere hawezi kutukanwa,Nyerere alikuwa mwanasiasa kama wanasiasa wengine,kwanini aseme uongo kuhusu mungano kwanini aseme kuwa "kama wazanzibari watakataa mungano hatowapiga mabomu lakini Aboud Jumbe alipohoji kuhusu mungano akamweka ndani,akamvua uraisi na uanachama wa CCM",,,Nyerere alikuwa sio nabii alikuwa muongo kama wanasiasa wengine,period
Kwa miaka kadhaa sasa nilikuwa naandika humu JF kuwa Nyerere. Ni mwongo. Nyerere ni kiongozi aliyeiletea matatizo hii nchi ya kila aina kwa uongo wake na undumila kuwili wake. Mlikuwa hamnielewi? Au mlikuwa hamtaki tu kuamini?
Nyerere alishakiri, kwanza ni Kanisa lake halafu ni nchi. Na hilo mtakataa tumwage ushahidi humu?
Unaweza kusema mengine yote lakini tukubaliane tu kuwa, Mwl. Nyerere hakuwa mtu wa kawaida. Historia inabainisha hivyo na wala siyo yeye anayebainisha kwenye historia. Think bigger!.
wewe ndo mgumu wa kuelewa,nimeshakwambia rais ali hassan mwinyi kwa nafasi yake kama rais alikubaliana na wazo la G-55 La kuundwa kwa serikali ya Tanganyika,mchakato ulikua ukienda vizuri,nyerere aliposikia alitoka butiama na kwenda dodoma na kuzuia kwa nguvu zote.Jadili kulingana na uzito wa hoja sio kulalama, soma maandishi mekundu tafakali halafu uliza kama hujaelewa.
Kwanza kuendelea kulumbana na marehemu ni jambo la kushangaza. Vipi maiti na wazima kuchangamana?
Hata hivyo alishajisemea baba wa watu kuwa kuna mengi alikosea pengine katika hayo makosa na Muungano ni moja wapo.
Kinachosikitisha ni baadhi ya watu kumtumia Nyerere kama hirizi; wakitaka jambo lisilo na hoja wanakibilia kusema baba wa Taifa alisema: wakiona wanahoja zao bazo Nyerere hakuzipenda basi hao wanajifanya kama vile hawakuwahi kumsikia Nyerere.
Mimi kwanza naona laana ku discuss vitu vya marehemu why cant we forget him and concentrate with our things bila kuhusisha maiti?
wewe ndo mgumu wa kuelewa,nimeshakwambia rais ali hassan mwinyi kwa nafasi yake kama rais alikubaliana na wazo la G-55 La kuundwa kwa serikali ya Tanganyika,mchakato ulikua ukienda vizuri,nyerere aliposikia alitoka butiama na kwenda dodoma na kuzuia kwa nguvu zote.
Hapo usichoelewa ni nini?.
Nimekwambia jk kwa nafasi yake kama rais alikubali mchakato wa katiba na amewaachia wananchi ndo wataamua ni mfumo upi ufuatwe.
mwinyi aliruhu iwepo Tanganyika,moto ukawaka,malecela akaambiwa kamshauri rais vibaya,alisemwa hadi akatungiwa na kitabu.
Mwinyi nae alisemwa hadi zoezi likasitishwa.
Jk nae ameruhusu mjadala na amewachia wananchi waamue mfumo wanaoutaka.
Aliyoyaongea Lissu wala si mapya, UAMSHO wakiyasema kila siku kwenye mikutano yao. Jussa kayasema hayo kwenye mikutano, mkamshambulia humuhumu JF.
Leo kulikoni? Uamsho wabaya kwa kusema hayohayo, Jussa mbaya kwa kusema hayohayo? FaizaFoxy, miaka nenda miaka rudi anayasema hayo hayo humumu JF (nikipata wasaa ntazifukuwa pposts zangu za hayo humuhumu JF) nae ni mbaya?
Jana kayasema Lissu, yeye ni mwema?
Usihangaike kutafuta jibu. Uamsho, Jussa, FaizaFoxy wote ni Waislaam kila kibaya watakachokisema kuhusu Nyerere. Wataonekana wao ni wabaya. Tundu Lissu?
Au huyu tundu nae kasilimu kisirisiri? Maana namuona kila ijumaa anapiga kanzu rasmi kabisa.
1. Je nini ilikuwa/ninafasi ya kikwete, mwinyi na mkapa kama marais.....wajibu, majukum na utekelezaji kama wakuu wanchi?
2. Nini malengo ya kudhibiti vipidi vya uraisi kwa miaka kumikumi............lengo kuu ninini?
3. watanzania waleo wananafasigani katika kuenzi maisha ya babu zetu? tunaendelea kulalia ngozi kwasbabu wao hawakuwa na uelewa na tecknolojia nzuri kuwawezesha? mbona hatulali na mbuzi wala kula mizizi?
-Yale tumeyacha ila ya nyerere tumeshindwa kuyaacha... kama sio lawama za kishenzi na ujinga ninini?
1. Je nini ilikuwa/ninafasi ya kikwete, mwinyi na mkapa kama marais.....wajibu, majukum na utekelezaji kama wakuu wanchi?
2. Nini malengo ya kudhibiti vipidi vya uraisi kwa miaka kumikumi............lengo kuu ninini?
3. watanzania waleo wananafasigani katika kuenzi maisha ya babu zetu? tunaendelea kulalia ngozi kwasbabu wao hawakuwa na uelewa na tecknolojia nzuri kuwawezesha? mbona hatulali na mbuzi wala kula mizizi?
-Yale tumeyacha ila ya nyerere tumeshindwa kuyaacha... kama sio lawama za kishenzi na ujinga ninini?
JULIUS NYERERE-Humanist,Politician ,and Thinker.-POLE SANA TUNDU LISU,HUNA HADHI YA KUMKEJELI BABA WA TAIFA,JIKITE KATIKA KUJENGA HOJA ZAKO TU,UTAELEWEKA.
Swala la dini na muungano halina mahusiano kwani zilizoungana ni inchi na sio dini mbili ziliungana,kwani bara kuna waislam wengi kuliko znz pia ijulikana kuwa kanisa la kwanza africa mashariki ni lile la nzizibar sasa msije mkaleta swala dini kwenye muungano.dini uliyonayo ni yako ww na roho yako wala hakuna aliyewahi kukulazimsha uabudu nn MASWALI KUAMINI TANZANIA MWALIMI ALIWEKA HURU KABISAA abdu un achotaka hata kama ni huo ukuta wa nyumba yako ww UPO HURU KUFANYA HIVYO ili mradi usivunje sheria za inchi SASA WW MWENYE FIKRA FUPI UNASEMA MUUNGANO ULIKUWA WA KANISA .JE?ulishawahi kulazimishwa kuingia kanisani huko kwenu zanzibar? au babu yako au baba yako aliwahi kulazimishwa na chombo chochote cha muungano kutoingia sehemu yake ya ibada MLIKIMBIA UMANDE KWA KUOGOPA KULISHWA NGURUWE JE MWALIMU ALIFANYAJE AKATAIFISHA SHULE ZOTE ZA KANISA ILI MSOME bado mkaendelea kuamini walimu wala nguruwe ni haramu ulitaka mwalimu afanye nn KAMA MLIKIMBIA UMANDE KWA KUOGOPA KUDUNDISHWA NA MAPDRI WAM
Samahani ni 7th April 2014, ntarekebisha.
1. Mwinyi na Mkapa ni vikaragosi vilivyowekwa na Nyerere na alikuwa akiviendesha kwa remote kutokea Bustiama na Msasani.
Kikwete, kathubutu kuanza mchakato wa kuibadili katiba na ndiyo maana unayaona yote hayo yanaibuka. Kikwete ni ngoma nzito.
2. Miak kumi kumi ni mfuno tu wa demokrasia. Nyerere alikaa miaka 24 na hakuna la maana alilofanya ukichanganya na vikaragosi vyake, Mwinyi na Mkapa unapata jumla ya uongozi wake miaka 44.
Utawala wa Kikwete ndio uliothubutu, kuipa uhai mpya nchi hii kwa kuanzisha huu mchakato wa kujipatia katiba mpya. Kikwete anastahili kila sifa kwa hili na mengine mengi tu.
3. Ndio yapo katika kuibuliwa ili yaachwe. Bila kuwa na katiba mpya utayaachaje?
Bila kuwachana na fikra za Nyerere tutabaki kuwa maskini wa kutupwa. Na njia ya pekee ya kuachana nayo ni kuyaainisha mabaya yake yote. Kwa sasa naona yanaanza kuwaingia, maana Uamsho na Wazanzibari wengine wengi na wengineo wa hapa bara walikuwa wakiyainisha haya, wengine tumeyaandika humuhumu JF. Mkatuona hatumpendi Nyerere mkatushambulia. Nakuuliza hivi, mtu uliyemuamini ukajuwa kuwa si muaminifu na ni muonngo, utaendelea kumuenzi?
Mkuu huyu FaizaFoxy ni mdini balaa! Yaani kamwona Pengo tu; Mufti kwake sio issue. Sometimes huyu ni wa kupuuza tu.