Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu



Kumbe na wewe ni kama yeye.
 
Tundu Lissu, kwenye ili la kumponda Nyerere, pro-Chadema wapo kimya masikini.

Natambua sana mchango wa nyerere kwa nchi, lakin haya anayosema lissu si kumponda liko wazi kwa yeyote anaetaka kujiita mkweli na msomi. Hakuna shaka nyerere alikua m2 kama ww, kukosea ama kufanya jambo kwa utashi binafsi ipo hata kwake. Nikuulize tu swali rahis, Unadhani nani kamponda nyerere kwanza, Prof shivji ktk kitabu chake, au dr mwakyembe ktk iyo paper yake? Kama ni muungwana jibu sahihi unalo
 
Katika hoja yako hii. Je, unakubaliana na Mh. Tundu Lissu anaposema Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu.

Tunaweza kucheza na maneno kwa mitindo kadhaa. Binafsi, sifurahishwi na uwasilishaji hoja wa Lissu; una jazba isiyo na ulazima. Bila shaka hiyo ndiyo hulka yake ambayo si rahisi kutibika katika umri aliofikia. LAKINI ana hoja nzito ambayo ni muhimu kwa yeyote yule anayetaka kuwa mshiriki mzuri wa jukwaa hili. Kwanza, katika masuala ya siasa na uongozi hapa duniani mantiki hairuhusu mtu "kuabudiwa" kama wengine wanavyotaka kuwafanya Nyerere, Sokoine, Mandela, n.k. Ukiisha ingiza "ibada ya binadamu" basi umeshakufuru misingi ya mantiki na hata ya Mwenyenzi Mungu (ambaye pekee anastahili kuabudiwa - kwa imani zetu wengine). NA huwezi kuwa na michango ya maana katika jukwaa hili kama unataka kuabudu binadamu.

Pili, mahsusi kwa Mwalimu Nyerere, tukubaliane kuwa alikuwa mkuu (a great person) ambaye aliyekuwa na picha rasmi (vision) ya nchi yake aliyoitaka yeye kwa malengo mazuri kabisa (hata kama picha hiyo ilikuwa na kasoro). Sio kama wengi waliomfuatia waliokuwa wakiangalia zaidi maslahi mafupi hususan ya mifuko yao na familia na marafiki zao. Ili kutimiza picha aliyokuwa nayo akawa mtu wa mikakati. Ukishakuwa mtu wa mikakati basi tukubaliane si nyakati zote utakuwa mkweli na muwazi. Wakati mwingine mikakati huhusisha ulaghai (kwa nia njema) ili malengo yake hatimaye yafikiwe. Manake lengo la mikakati ni "kuwaweka watu sawa" waendane na mipango yako - ama iwe mizuri ama iwe mibaya. Cha maana katika mikakati ni uzuri wa lengo lako la mwisho.

Wengi tunachomheshimu Nyerere ni kuwa mikakati yake haikuwa ya kujenga taifa la kujinufaisha yeye na familia yake binafsi. Hakuwa na tamaa nzito za kibinadamu za mali na mengineyo. Malengo yake bila shaka yalikuwa mazuri kwa wote na kwa taifa zima. Tatizo kubwa la dhahiri ni kuwa na ubinafsi wa fikra uliokithiri; hakuwa tayari sana kukubali mawazo mbadala ya wengine. Ushahidi wa kukosa subira na mawazo mbadala ni mwingi kuanzia kwenye mitafaruku na akina Kambona, Kassanga Tumbo, Jumbe, Mtei, n.k. Wakati mwingine alikuwa sahihi hasa kwa wale waliokuwa na mipango ya kujikweza kwa elimu na nafasi zao lakini ushahidi unaonyesha pia aliishia kujenga uongozi wa kujikomba sana (bootlickers).

Kwamba aliendesha masuala ya muungano kimkakati sana halina ubishi. Aidha hatuwezi kusema kuwa alikuwa na nia mbaya katika muungano huu. Hakuna ushahidi wa "nia mbaya". Tatizo kubwa ni kuwa alitwisha uongozi wa pande zote maudhui yake pekee na kutosimamia taratibu kamilifu na za wazi katika mchakato mzima wa muungano. Ni kama vile kwake yeye hoja likuwa ni "muungano kwa gharama yoyote ile". Ni dhahiri basi kuwa mahangaiko tunayopata leo (kuanzia wakati wa Jumbe) kuhusu muungano ni matokeo (consequences) za mapungufu ya "mikakati" ya Mwalimu katika mchakato aliousimamia. Ukitaka kuwa mkorofi (usiye na mikakati kabisa) kama Lissu unaweza kumpa vigezo vya "uongo na udanganyifu". Lakini ukiwa mtu mstaarabu huwezi kutumia lugha hiyo kwa Mwalimu; utamchukulia kama mtu aliyekuwa na mikakati dhaifu (upungufu wa kibinadamu!).
 
Vip mkuu ni nini kinakuchanganya?
 

Hivi watu wanaelewa nini maana ya PhD? Yanayoandikwa katika PhD siyo vifungu vya bibllia au aya katika korani. Muda unavyoenda tafiti zaidi zaibuka na vitu ambavyo vilidhaniwa ni kweli wakati huo vinaweza kubadilika. ndiyo maana ya sayansi katika utafiti.

Mtu anaweza kuigeuka hoja yake mwenyewe lakini lazima kuwe na sababu za msingi kufanya hivyo na wanasayansi/watafiti wengine wazione hizo hoja.
 
Lissu omba radhi. Kumtukana Nyerere ni kuwatukana watanzania
Acha kutusemea watanzania na akili zao mfu hizo, Nyerere mwenyewe alikili kwa kinywa chake kuwa kuna mambo mengi tu ya kijinga yalifanywa katika utawala wake sasa wewe unamuona kama mungu wa watanzania wote ?
 


1 Kwa kweli inauma mm napenda sana s3 ila sipendi mtu yoyote anaetaka kuvunja muungano wetu huyo tumkabili kwa hali na mali ikibidi tumzibiti hata kwa dola

2 muungano ule liopo duniani lazima ubabe uwepo ndiomana ukienda usa huruhusiwi kuoji muungano wao kwa namna yoyote kwa upole au kwa shari kwa kulinda maslai ya nchi husika na uchumi wake

3 simpendi mtu anaekashifu au kutukana viongozi wetu wote waliojitolea kwa nguvu zao zote kupigania uhuru wa nchi yetu japo na wao walikuwa na makosa yao yakibinadamu lakini si kwa kashfa au tusi siuungwana kwani nae anaeshima na pia na familia yake itajisikiaje kwa kuwakashfu ndugu yao mwenye hadhi ya kitaifa?
 

Very good point,mara nyingi huwa nasema haya mambo,unakuta kuna wazalendo lukuki waliojitoa kupigania uhuru lakini hawakumbukwi kabisa,ni bonge la usaliti.Utasikia,MANDELA DAY...kwa nini hakuna Oliver wa Katambo day? Our leaders are really betrayers! R.I.P mzalendo wa kweli,komrade John Okello,wewe ni mfano wa kuigwa,kwani ni nani awezaye kujitoa tena na si mzaliwa wa nchi husika?

Back to Topic;niaminicho mimi Nyerere alikuwa na dikteta wa kupindukia kwani alikuwa hataki ushauri katika maamuzi yake hivyo hoja ya kamanda Lissu imeshiba sana.Swali ambalo huwa najiuliza,kama Nyerere hakuma fisadi,alishindwa nini kumwajibisha Mkono pasi na kumruhusu akimbie? Ni wizi mtupu,hakuna mwema chini ya jua.
 
Sikutegemea kwa mtu mzima Kama lisu kumtusi muasisi Wa taifa. Alitakiwa kujenga hoja,na kwa njia ta matusi. Tumesononeka sana sisi watanzania,kauli ya mtusi mwalimu haivumiliki. Ningekuwa mimi ndio mkono Wa dola, ningechukua hatua mathubuti.

Si kila kitu kazima useme, pima tumia hâta busara ya kawaida. Tunamheshimu mwl na bado tunampenda. Amani unayoiona si kwa bahati mbaya. Karibu kujizuia kwa baadhi ya mambo. Huwezi hâta kidogo wewe lisu kujilinganisha na mwl. Linda heshima yako na chama chako. Kila kona wanasema umekosea.

KAzi njema.

----------------------------

Maelezo kutoka kwa Mzee Edwin Mtei

 
Mkuu sitaki kupinga au kukubaliana na hoja yako mimi ninakusudia hapo kwenye Red
sijui amani hiyo ni kwa kina nani? Maana mimi natembea na Mkongojo kwani nimewekewa
chuma kwenye mguu wangu baada ya vipigo vya polisi, si hivyo tu kuna ndugu yangu ambaye
alikuwa mjamzito pale Mtwara mjini alipigwa risasi na polisi na akapoteza maisha sijui ni
amani gani unaizungumzia?
 
wewe ndo umekosea na wala kujitoa kwako sdm si jambo lolote, kwani unamsujudia huyo mwl ili iweje? amani iliyoko safrica, botswana angola ghana na sehemu zingine kapeleka mwl watu wenye akili finyu km ya kwako ndo wanadhani kuwa wana amani je wafngwa na mahabusu wako kimya wana amani kiasi gani? hauwezi kutofautisha ukimya unaosababishwa na ujinga wa kutojitambua dhidi ya watu wanaojitambua na kudai haki kamanda Lisu oyeee haujakosea kitu chapa mwendo tunakfuatilia.
 
Barabara nyeupe kama ulikuwa chadema bila kujifahamu. Nendwa huko kunakokupasa.
 
AMANI gani unaongelea katika mgodi wa North mara vijana wapatao 300 wameuawa na askari kwa muda wa miaka 10 tu.
 
Kwa hiyo unaishi kwa kumtegemea hayati mwl. Nyerere? Je wewe lini utaenziwa wewe? Hii ni haki yako kikatiba!
 

Mbona wengine tumeona sawa tu.Alichosema Lissu kilitakiwa kusemwa siku nyingi.Inawezekana ni maneno makali tu aliyotumia lakini siwezi kumlaumu Mwalimu sababu inawezekana alikuwa na sababu zake za msingi za kuficha ukweli,na alisema kuwa kuna mengi walikosea kama viongozi hakusema nini walikosea,sasa kama kuna mtu anasema hayo ndiyo alikosea basi tukiri alikosea,hata kama hakusema ukweli kuhusu Muungano basi waache waliotafiti na kuona kilichotokea tusiwahukumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…